Mwongozo bora na vitu vya kuzingatia katika kuanzisha kuku wa mayai

Mwongozo bora na vitu vya kuzingatia katika kuanzisha kuku wa mayai

Hao wamekuwa maana vifo vingi hutokea siku ya kwanza na pili, na siku zinavyoongezeka vifo hupungua na huisha kabisa.

Fanya kushika ratiba ya chanjo, zingatia usafi na pia wapewe chakula safi na maji safi na hakika utayaona matunda yake siku za usoni.
 
Fanya hivi;

- Siku ya 7 wape chanjo ya mdondo/Kideri kwa njia ya maji au matone
- Siku ya 14 wape chanjo ya gumboro kwa njia ya maji
- siku 21 rudia chanjo ya mdondo/kideri kwa njia ya maji au matone

Zingatia: Baada ya siku 21, utarudia kuchanja kideri baada ya siku 90 ambayo ni sawa na miezi mitatu (3) na unakua unarudia hivyo kila baada ya miezi 3.

- Siku ya 28 rudia chanjo ya gumboro kwa njia ya maji.
- Wiki ya 6-8 chanja Ndui kwa njia ya sindano hii unachoma kwenye utando laini kwenye bawa.
- Wiki ya kumi na mbili (12) chanja Homa ya matumbo ( salmonellosis) hii unachoma kwenye nyama hasa pajani.
Je nitawapa tuu hizi chanjo ,vip kuhusu vitamins za kuchanganya kwenye maji zina umuhimu wowote?
 
Hii inategemea na mfugaji na aina ya ufugaji mtu au hata mazingira ya ufugaji.

Wafugaji wengi wanafanya kuwapa vitastress baada ya kuwapa chanjo hii inasaidia kuwachangamsha kuku maana wanapokunywa wale virusi huwa kuna mabadiliko ya miili yao, so vitamini inafanya kuwa boost kiasi.

Ila wengine pia hawatoi hizo vitastesss na kuku wanakuwa vizuri tu bila shida, so ni wewe mwenyewe kuchagua uwape au usiwape.
Je nitawapa tuu hizi chanjo ,vip kuhusu vitamins za kuchanganya kwenye maji zina umuhimu wowote?
 
Hii inategemea na mfugaji na aina ya ufugaji mtu au hata mazingira ya ufugaji.

Wafugaji wengi wanafanya kuwapa vitastress baada ya kuwapa chanjo hii inasaidia kuwachangamsha kuku maana wanapokunywa wale virusi huwa kuna mabadiliko ya miili yao, so vitamini inafanya kuwa boost kiasi.

Ila wengine pia hawatoi hizo vitastesss na kuku wanakuwa vizuri tu bila shida, so ni wewe mwenyewe kuchagua uwape au usiwape.
Je aloevera,mwarobain na mlonge naweza kuwapa wakiwa na umri gani?
 
Je aloevera,mwarobain na mlonge naweza kuwapa wakiwa na umri gani?
Hizo njia naturally sijafahamu kwa kweli sitaki kukuongopea, lakni ukienda kwenye mitandao utazikuta na wameelezea hadi namna ya kuandaa
 
Msaada tafadhali,vifaranga wangu wameanza kufa,nakuta amelala hawezi kusimama ameishiwa Nguvu kabisa ,chakula hali na maji pia hanywi sijui tatizo itakuwa ni nini.? Naogopa tatizo lisije kuongezeka
 
Msaada tafadhali,vifaranga wangu wameanza kufa,nakuta amelala hawezi kusimama ameishiwa Nguvu kabisa ,chakula hali na maji pia hanywi sijui tatizo itakuwa ni nini.? Naogopa tatizo lisije kuongezeka
Hali ya hewa ndani ya banda iko vipi mkuu? Na msimu huu wa mvua wafugaji wengi huwa wanajisahau wanafunga madirisha yote hivyo kutukuruhusu hewa safi ya oksijeni kuingia ndani ili kuweza kuchukua ya hewa chafu, hivyo yaweza kuwa hilo tatizo.

Fanya kucheza na hali ya hewa, hakikisha kuna mzunguko mzuri wa hali ya hewa ndani ya nyumba ya kuku.
 
Hali ya hewa ndani ya banda iko vipi mkuu? Na msimu huu wa mvua wafugaji wengi huwa wanajisahau wanafunga madirisha yote hivyo kutukuruhusu hewa safi ya oksijeni kuingia ndani ili kuweza kuchukua ya hewa chafu, hivyo yaweza kuwa hilo tatizo.

Fanya kucheza na hali ya hewa, hakikisha kuna mzunguko mzuri wa hali ya hewa ndani ya nyumba ya kuku.
Dah nimeziba kote kwasababu ya mvua ilikuwa ya upepo inaingia
 
Dah nimeziba kote kwasababu ya mvua ilikuwa ya upepo inaingia
Ndio tatizo hilo, ufanye kufungua madrisha kwa juu ( acha upenyo mdogo) kuruhusu hewa safi kuingia, mambo yatakuwa vizuri tu.
 
Ndio tatizo hilo, ufanye kufungua madrisha kwa juu ( acha upenyo mdogo) kuruhusu hewa safi kuingia, mambo yatakuwa vizuri tu.
Asante nimeshafanya ivyo,hizi mvua za dar nazo hazitabiriki ikanibidi nizibe kote,je na usiku niache kidogo au nizibe maana vipo karibu na dirisha
 
Asante nimeshafanya ivyo,hizi mvua za dar nazo hazitabiriki ikanibidi nizibe kote,je na usiku niache kidogo au nizibe maana vipo karibu na dirisha
Jaribu kuacha huo upenyo masaa 24 mkuu
 
Usijali mkuu kama vile forum hii inavyotaka , tuko hapa kubadilishana mawazo mawili matatu ili kuweza kufanikisha mifugo yetu inakua salama salimini
Kingozi naona unatoa somo zuri la ujasiriamali na mimi nataka niingie kwenye uwo ufugaj. Changamoto zangu kubwa ni aina ya mbegu bora ya vifaranga vya kuku wa mayai na kampuni gani zinatowa Vinatowa mbegu bora
 
...Na kuna mda alishawai kuniambia kuna mbegu ya vifaranga vya kuku inauwezo wa kutaga mara mbili kwa siku ni kweli kuna mbegu kama iyo na inaitwaje
 
Kwa Tanzania ni kampuni tatu tu ninazozielewa sana katika suala zima la uzalishaji wa vifaranga waliobora;

Kampuni ya kwanza ni Silverlands Tanzania inapatikana Iringa vijijini, hawa jamaa vifaranga wao wako vizuri hasa Layers ( Hyline Brown ) maana siku ya kwanza hupewa chanjo zaidi ya tatu ambazo ni Marek's, Newcastle na Gumboro (Faida ya chanjo inayotolewa kwa kuku wao ni very effective amabapo haina haja ya kurudia tena).

Pia chanjo hizo hapo juu hupewa kuku wao aina ya Sasso, maana inategemea na lengo la mfugaji ambapo anaweza kuwafuga kama kuku wa mayai au Nyama.

Mwisho wanazalisha vifaranga vya kuku wa nyama aina ya Cobb 500 ambapo pia wako vizuri hawa hupewa chanjo mbili tu ya Newcastle na Gumboro.

Tukija kwa kampuni ya pili ni Interchick limited hawa wanapatikana hapa Dar es salaam hawa jamaa pia vifaranga wako vizuri pia, wanazalisha vifaranga wa nyama, mayai na chotara ingawa chotara wao anaitwa Kuroiler aina ya TANBRO.

Kwenye suala la chanjo hawa hutoa chanjo ya Marek's pekee tofouti na Silverlands.

Tatu, kwa mahitaji ya kuku chotara aina ya Kuroiler waweza watafuta pia AKM GLITTERS hawa wako Dar es salaam maeneo ya Sinza. Hawa huzalisha Chotara pekee.

Hawa pia kwenye suala la chanjo hutoa Mareks pekee tofouti na silverlands.

NB: Epuka kununua vifaranga kwa watu binafsi maana wanawauzia uzao wa pili hadi wa tatu mwisho wa siku performance ya kuku husikia huwa below 50%

Nimemaliza.
Kingozi naona unatoa somo zuri la ujasiriamali na mimi nataka niingie kwenye uwo ufugaj. Changamoto zangu kubwa ni aina ya mbegu bora ya vifaranga vya kuku wa mayai na kampuni gani zinatowa Vinatowa mbegu bora
 
Back
Top Bottom