Mwongozo wa kufanya biashara ya kusafirisha zao la Nyanya

Mwongozo wa kufanya biashara ya kusafirisha zao la Nyanya

Kidodi_88

New Member
Joined
Feb 10, 2022
Posts
4
Reaction score
2
Habari wana JamiiForums, naomba msaada wa mawazo kwa aliyewahi kusafirisha nyanya kutoka Moshi, Iringa, Makambako, e.tc kuleta Dar es Salaam naomba anipe mwongozo wa chochote anachokijua kuhusu hii biashara. Natanguliza shukrani zangu.
 
Nina experience kidogo kwa kutokea makambako

1.Fika makambako eneo linaitwa soko la nyanya hapo, utapata nyanya kutokana na uhitaji wako, yaani Kuna wamama hapo watakutafutia nyanya na watakutafutia vijana wa kupanga kwenye box (mtakubaliana bei ya kukaba nyanya)

2. Being ya box empty la nyanya Ni 1200-1500

3.Kamba + karatasi inategemea na box za nyanya ila karatasi moja Ni tsh 150-200, Rola ya kamba Ni Tsh 12,000/=

4.Usafiri utapata hapohapo sokoni Kuna jamaa anaitwa Mwenye Akili Nick name maarufu sana hapo sokoni, Jamaa wako vizuri sana Kuhusu usafiri pia wanamadalali wao masoko ya Dar, kwahiyo unaweza kupakia mzigo kwao halafu wakakuuzia kutokana na bei ya sokoni Dar. Bei ya usafiri sikumbuki vizuri ila inacheza kwenye 1,800-2,500 kwa box.

Wish you the best, karibu kwa maswali zaidi.
 
Nina experience kidogo kwa kutokea makambako

1.Fika makambako eneo linaitwa soko la nyanya hapo, utapata nyanya kutokana na uhitaji wako, yaani Kuna wamama hapo watakutafutia nyanya na watakutafutia vijana wa kupanga kwenye box (mtakubaliana bei ya kukaba nyanya)

2. Being ya box empty la nyanya Ni 1200-1500

3.Kamba + karatasi inategemea na box za nyanya ila karatasi moja Ni tsh 150-200, Rola ya kamba Ni Tsh 12,000/=

4.Usafiri utapata hapohapo sokoni Kuna jamaa anaitwa Mwenye Akili Nick name maarufu sana hapo sokoni, Jamaa wako vizuri sana Kuhusu usafiri pia wanamadalali wao masoko ya Dar, kwahiyo unaweza kupakia mzigo kwao halafu wakakuuzia kutokana na bei ya sokoni Dar. Bei ya usafiri sikumbuki vizuri ila inacheza kwenye 1,800-2,500 kwa box.

Wish you the best, karibu kwa maswali zaidi.
King Savi nimepata dalali wa kunipeleka shamba Ruaha, je nyanya ya eneo hili ikoje?
 
Nyanya ya Ruaha inachangamoto kiasi

1. Asili ya Ruaha mbuyuni Kuna joto kwahiyo nyanya yake inawahi kurojeka

2.Usafiri: Kama utaweza kujaza gari pekeako itakua poa, ila Kama hutajaza gari inakulazimu uunganishe na wengine sasa hapo ndio changamoto inaanzia
a) Kama nyanya ilikua imechumwa kwenye mvua au imechumwa imeiva, (nimeshakwambia Kuhusu joto la Ruaha mbuyuni) hapa ndio pabakua na changamoto sana

B) Usikubali kupakia na kushusha nyanya ya Ruaha mbuyuni, Kama unaenda kuchumia shambani hakikisha hiyo gari inamzigo wakutosha kuondoka siku hiyo hiyo USIKUBALI KULALA au kupakua na kupakia gari nyingine.
King Savi nimepata dalali wa kunipeleka shamba Ruaha, je nyanya ya eneo hili ikoje?
 
Back
Top Bottom