Mzazi wakati unasomesha usisahau kuwekeza kwaajili ya kesho yako

Mzazi wakati unasomesha usisahau kuwekeza kwaajili ya kesho yako

Judithkaunda

Member
Joined
Aug 21, 2022
Posts
90
Reaction score
231
Habari wana JF,

Asilimia kubwa humu wazazi wetu wameishia elimu ya msingi na wengine hawakusoma kabisa, lakini wamepambana kwaajili yetu na kwakiwango kikubwa wamefanikiwa tumesoma sekondari na wengine mpaka chuo.

Hata wewe hapo ulipo unapambana mwanao afikie elimu ambayo wewe hukufika na ili kufanikisha hilo utatakiwa kumsomesha shule nzuri itakayomuandaa kufika huko.

Wakati unapambana na kujinyima ili upate ada na mahitaji yake, usisahau kujilipa na wewe kwa kuwekeza kwenye miradi itakayokuja kukuingizia pesa bila kufanya kazi wakati ambao hautakuwa na nguvu ya kupambana na kazi kama sasa.

Tena kuna wengine wanasomesha shule za gharama wakati wako kwenye nyumba za kupanga, hilo siyo tatizo lakini ni hatari sana kama mtoto akifeli halafu bili zimeisha na mwenye nyumba anataka kodi yake.

Tuwasomeshe kama jukumu letu na siyo kuweka malengo ya kula matunda yao. Mfano mzuri jitafakari wewe ni asilimia ngapi mpaka sasa mzazi wako amekula matunda yako?;Mfikirie yule baba na mama yako waliohangaika kwaajili yako wamenufaika nini kwako?

Na mpaka umri huu wa utu uzima kuna wengine tukikwama bado tunaomba msaada kwao. Tangu anazaliwa anakutegemea mpaka anafika chuo, akimaliza tayari ni mtu mzima anaoa au kuolewa anaanza majukumu kama mzazi, niambie hapo bado unatarajia matunda gani na hali ilivyongumu?

Tuwekeze wapendwa tusije kuwa ombaomba kwa watoto wetu, matokeo yake tutaanza kutia huruma kwa watoto waliotakiwa kutuheshimu. Huyo unayempigania leo, kesho atapigania familia yake kwanza kabla yako. Utapanda wewe lakini utakuwa wa mwisho kuvuna.

Wakati wewe unaishi kwenye nyumba ya tope, mwanao anaishi geti kali halafu anakwambia maisha magumu sana. Tujiandae tusije kuwalaumu watoto wetu na kuwapa laana. Na bado ukifa atarithi hicho kidogo chako, lakini yeye akifa unaweza usipate kitu.

Elimu ni muhimu sana lakini wakati tunapambana tusisahau kupanga maisha yetu ya baadae.
 
Ni kosa kusomesha mtoto shule ambayo unaumia kulipa ADA

Tujikune uwezo wetu ufikiapo, huku tukiangalia ya kesho

Si lazima mtoto aajiriwe
Si lazima mtoto alipe ada maana serikali inatoa elimu bure
Kuigana kwingi
 
Habari wana JF,

Asilimia kubwa humu wazazi wetu wameishia elimu ya msingi na wengine hawakusoma kabisa, lakini panga maisha yetu ya baadae.
Somo zuri sana! Katika ukoo wetu tunaandaliwa kuwa hakuna kurithi! Mtoto akiwa tumboni anaanza kuhubiriwa kuwa hakuna kurithi tafuta vyako! Maana yake ni kuwa hata wewe usitegemee kutunzwa na mtoto wako!

Juzi nilisoma pahala mtoto wangu alikuwa anahojiwa akajibu:

‘I remember as kids dad once said “me I don’t want my kids to ever financially depend on me, I’ll take care of myself, they should take care of themselves and not ask"
 
Ukitaka kuishi kwa raha ndani ya dunia hii kubali msemo unao sema binadamu hatulingani na hatutokuja kulingana.

Ukisha kubaliana na msemo na kuuishi basi utaishi maisha kwa kuinjoy hata kama ni masikini.
Hakika ni upumbavu na upungufu wa akili kurazimisha kuishi aina ya maisha ambayo hayaendani na kipato chako.

Hivi mtu umepanga vyumba viwili una watoto wanne ww na mkeo mnalala chumbani,watoto wanalala sebureni wamerundikana kama wafungwa na mbaya zaidi unakuta ni jinsia tofauti.

Lakini una razimisha kumpeleka mtoto wako kwenye shule ada ni kuanzia million 2, kisa tu mtoto wa jirani anasoma shule hiyo, jirani ambaye hujui kipato chake na hujui pesa anapataje.
Hiyo ni akili gani zaidi ya ulimbukeni na ushamba?

Kwann usiwapeleke watoto wako kwenye shule ya kawaida ili utumie hizo hela kujengea nyumba nzuri ya kutosha ili watoto wako walale vizuri.

Mtoto hata kama ana soma shule za kawaida akipata mfatiliaji mzuri wa maendeleo yake shuleni atafanya vizuri tu.

WaTz tujifunze kuishi maisha tunayo yaweza tuache ulimbukeni tuta kuja kuwatwisha lawama watu wengine hali ya kuwa makosa tuliyafanya wenyewe.
 
Ni kweli kabisaa mkuu!tujitahidi sana kuwekeza!jukumu la mzazi ni kumsomesha mtoto wake!lakini sio jukumu la mtoto kumtunza mwanae(namaanisha asipokutunza hakuna mahali utampeleka,ila wewe kama mzazi usipomsomesha akikushtaki utahukumiwa)
 
Habari wana JF,

Asilimia kubwa humu wazazi wetu wameishia elimu ya msingi na wengine hawakusoma kabisa, lakini wamepambana kwaajili yetu na kwakiwango kikubwa wamefanikiwa tumesoma sekondari na wengine mpaka chuo.

Hata wewe hapo ulipo unapambana mwanao afikie elimu ambayo wewe hukufika na ili kufanikisha hilo utatakiwa kumsomesha shule nzuri itakayomuandaa kufika huko.

Wakati unapambana na kujinyima ili upate ada na mahitaji yake, usisahau kujilipa na wewe kwa kuwekeza kwenye miradi itakayokuja kukuingizia pesa bila kufanya kazi wakati ambao hautakuwa na nguvu ya kupambana na kazi kama sasa.

Tena kuna wengine wanasomesha shule za gharama wakati wako kwenye nyumba za kupanga, hilo siyo tatizo lakini ni hatari sana kama mtoto akifeli halafu bili zimeisha na mwenye nyumba anataka kodi yake.

Tuwasomeshe kama jukumu letu na siyo kuweka malengo ya kula matunda yao. Mfano mzuri jitafakari wewe ni asilimia ngapi mpaka sasa mzazi wako amekula matunda yako?;Mfikirie yule baba na mama yako waliohangaika kwaajili yako wamenufaika nini kwako?

Na mpaka umri huu wa utu uzima kuna wengine tukikwama bado tunaomba msaada kwao. Tangu anazaliwa anakutegemea mpaka anafika chuo, akimaliza tayari ni mtu mzima anaoa au kuolewa anaanza majukumu kama mzazi, niambie hapo bado unatarajia matunda gani na hali ilivyongumu?

Tuwekeze wapendwa tusije kuwa ombaomba kwa watoto wetu, matokeo yake tutaanza kutia huruma kwa watoto waliotakiwa kutuheshimu. Huyo unayempigania leo, kesho atapigania familia yake kwanza kabla yako. Utapanda wewe lakini utakuwa wa mwisho kuvuna.

Wakati wewe unaishi kwenye nyumba ya tope, mwanao anaishi geti kali halafu anakwambia maisha magumu sana. Tujiandae tusije kuwalaumu watoto wetu na kuwapa laana. Na bado ukifa atarithi hicho kidogo chako, lakini yeye akifa unaweza usipate kitu.

Elimu ni muhimu sana lakini wakati tunapambana tusisahau kupanga maisha yetu ya baadae.
Uko sahihi kabisa Mkuu
 
Wazazi hawataelewa hili.

Wanasema wanawekeza lakini hawajui kua wanambebesha mzigo mzito mtoto wao na kumfanya asiishi maisha yake.
 
Kuna shule mtoto akisoma hawezi kufeli hata kwa dawa, ni wewe tu kuamua mwanao awe na uhakika wa kufaulu au aendelee kumuomba Mungu siku ya mtihani.
 
Na Kuna hili wazazi wa kiafrica na hata mitandaoni utaona tuchukulie ule msiba wa mother wa yule star wa kike ambaye mama ake alikufa huko kwao muheza ila nyumba wakati wanaenda kuzika..Nyumba imechoka ila baadae alikuja kupata shambulio la hatar kwa kusemwa kwamba hpa town anakaa sehemu nzuri sana japo hakujenga ila mother wake yuko ovyo sana huko kwake...sasa ukiangalia kwa nn watu wanamlaumu ..Maisha ya kuunga unaweza kujenga kwenu ila wewe ikawa hauna power au itachukua mda kujenga kwako ..


Ni better kutoa kama sapot kadri ya uwezo wako kama matumizi ,mda mwingine unaweza Kuta una mzigo mara wa kusomesha watoto wengine au wa kwako na familia kabisa ...Behind watu wanakushambulia kujenga kwenu hat uchukue mkopo ukajenge kwenu ni mzigo kwako mfano unatake home ya 450k au 500k then chukua mkopo means utajenga kwenu ambapo hukai na bado unapambana na familia hapa Town kweny nyumba za kupanga na mkopo juu mpaka uje kamilisha kujenga majukumu labda ushakuwa na watoto kama wawili au watatu bado kuwasomesha ..wakati unajenga pia Kuna wazazi kuumwa ,Kuna kusaidia ndugu ..

Ukiangalia unajikuta kwa imagine ya mbele za watu umefanya jambo la maana ila kwa ishu na maendeleo yako binafsi unajila ndanindani mpaka unakuja staafu ndo unaanza ujenzi .
 
Habari wana JF,

Asilimia kubwa humu wazazi wetu wameishia elimu ya msingi na wengine hawakusoma kabisa, lakini wamepambana kwaajili yetu na kwakiwango kikubwa wamefanikiwa tumesoma sekondari na wengine mpaka chuo.

Hata wewe hapo ulipo unapambana mwanao afikie elimu ambayo wewe hukufika na ili kufanikisha hilo utatakiwa kumsomesha shule nzuri itakayomuandaa kufika huko.

Wakati unapambana na kujinyima ili upate ada na mahitaji yake, usisahau kujilipa na wewe kwa kuwekeza kwenye miradi itakayokuja kukuingizia pesa bila kufanya kazi wakati ambao hautakuwa na nguvu ya kupambana na kazi kama sasa.

Tena kuna wengine wanasomesha shule za gharama wakati wako kwenye nyumba za kupanga, hilo siyo tatizo lakini ni hatari sana kama mtoto akifeli halafu bili zimeisha na mwenye nyumba anataka kodi yake.

Tuwasomeshe kama jukumu letu na siyo kuweka malengo ya kula matunda yao. Mfano mzuri jitafakari wewe ni asilimia ngapi mpaka sasa mzazi wako amekula matunda yako?;Mfikirie yule baba na mama yako waliohangaika kwaajili yako wamenufaika nini kwako?

Na mpaka umri huu wa utu uzima kuna wengine tukikwama bado tunaomba msaada kwao. Tangu anazaliwa anakutegemea mpaka anafika chuo, akimaliza tayari ni mtu mzima anaoa au kuolewa anaanza majukumu kama mzazi, niambie hapo bado unatarajia matunda gani na hali ilivyongumu?

Tuwekeze wapendwa tusije kuwa ombaomba kwa watoto wetu, matokeo yake tutaanza kutia huruma kwa watoto waliotakiwa kutuheshimu. Huyo unayempigania leo, kesho atapigania familia yake kwanza kabla yako. Utapanda wewe lakini utakuwa wa mwisho kuvuna.

Wakati wewe unaishi kwenye nyumba ya tope, mwanao anaishi geti kali halafu anakwambia maisha magumu sana. Tujiandae tusije kuwalaumu watoto wetu na kuwapa laana. Na bado ukifa atarithi hicho kidogo chako, lakini yeye akifa unaweza usipate kitu.

Elimu ni muhimu sana lakini wakati tunapambana tusisahau kupanga maisha yetu ya baadae.
ukitaka usiteseke na hii dunia ya sasa punguza kuzaa hovyo.. zaa watoto unaoweza kuwamudu kwa wakati wa sasa na wa baadae haya mambo ya kuwaza kizamani eti kuwa na watoto wengi ni ufahari na ushababi utakufa huku unanung'unika sana... kuwa na watoto wengi ni mzigo kwa mzazi aliyewaleta.. MAISHA NI KUISHI
 
Habari wana JF,

Asilimia kubwa humu wazazi wetu wameishia elimu ya msingi na wengine hawakusoma kabisa, lakini wamepambana kwaajili yetu na kwakiwango kikubwa wamefanikiwa tumesoma sekondari na wengine mpaka chuo.

Hata wewe hapo ulipo unapambana mwanao afikie elimu ambayo wewe hukufika na ili kufanikisha hilo utatakiwa kumsomesha shule nzuri itakayomuandaa kufika huko.

Wakati unapambana na kujinyima ili upate ada na mahitaji yake, usisahau kujilipa na wewe kwa kuwekeza kwenye miradi itakayokuja kukuingizia pesa bila kufanya kazi wakati ambao hautakuwa na nguvu ya kupambana na kazi kama sasa.

Tena kuna wengine wanasomesha shule za gharama wakati wako kwenye nyumba za kupanga, hilo siyo tatizo lakini ni hatari sana kama mtoto akifeli halafu bili zimeisha na mwenye nyumba anataka kodi yake.

Tuwasomeshe kama jukumu letu na siyo kuweka malengo ya kula matunda yao. Mfano mzuri jitafakari wewe ni asilimia ngapi mpaka sasa mzazi wako amekula matunda yako?;Mfikirie yule baba na mama yako waliohangaika kwaajili yako wamenufaika nini kwako?

Na mpaka umri huu wa utu uzima kuna wengine tukikwama bado tunaomba msaada kwao. Tangu anazaliwa anakutegemea mpaka anafika chuo, akimaliza tayari ni mtu mzima anaoa au kuolewa anaanza majukumu kama mzazi, niambie hapo bado unatarajia matunda gani na hali ilivyongumu?

Tuwekeze wapendwa tusije kuwa ombaomba kwa watoto wetu, matokeo yake tutaanza kutia huruma kwa watoto waliotakiwa kutuheshimu. Huyo unayempigania leo, kesho atapigania familia yake kwanza kabla yako. Utapanda wewe lakini utakuwa wa mwisho kuvuna.

Wakati wewe unaishi kwenye nyumba ya tope, mwanao anaishi geti kali halafu anakwambia maisha magumu sana. Tujiandae tusije kuwalaumu watoto wetu na kuwapa laana. Na bado ukifa atarithi hicho kidogo chako, lakini yeye akifa unaweza usipate kitu.

Elimu ni muhimu sana lakini wakati tunapambana tusisahau kupanga maisha yetu ya baadae.
Uko sahihi kabisa Mkuu,
 
Back
Top Bottom