TANZIA Mzee Kavana (alishiriki Maasi ya 1964) afariki dunia!

TANZIA Mzee Kavana (alishiriki Maasi ya 1964) afariki dunia!

Kufuatana na taarifa ya Kashmiri, hicho cheo cha 'meja' alichopewa hakikuwa 'formal'. Hivi ni vyeo alivyo shinikizwa Kambona avitunuku wakati huo wa maasi. Kashmiri, anasema Kambona alipandishwa juu ya meza kutangaza hivyo vyeo kwa maofisa walio kuwepo kwenye tukio hilo kwenye kambi ya'Colito'.
Sarakikya hakuwepo kwenye tukio hilo, yeye alikuwa Tabora.

..ngoja nianze mbali kidogo, nitakuomba uwe nami.

..Mkuu wa Tanganyika Rifles alikuwa mzungu Brigadier.Patrick Sholto Douglas.

..maasi ya Tanganyika Rifles yalifanywa na non commissioned officer waliokuwa wakidai mishahara, vyeo, na africanization jeshini.

..wakati wa maasi maofisa wote walikamatwa na kutupwa rumande. Maafisa wa Kizungu waliamriwa kurudi kwao Uingereza.

..zoezi la kumpata mkuu mpya wa Tanganyika Rifles lilianza na Alexander Nyirenda alikataliwa alipopendekezwa.

..baada ya hapo ndipo akapendekezwa Luteni Elisha Kavana. Taarifa zinasema alitolewa mahabusu na kupachikwa cheo cha Brigadier badala ya mzungu ambaye alikuwa hatakiwi.

..hata ukisoma vitabu vya historia vinaeleza kwamba Elisha Kavana alionekana kushtushwa na tukio hilo na alilazimishwa na askari waasi kuchukua wadhifa huo.

..maasi hayo yalikuja kuzimwa kwa msaada wa askari toka Uingereza. baada ya hapo Mwalimu Nyerere alivunja jeshi la Tanganyika Rifles, na akaunda jeshi jipya, Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

..Mwalimu pia alimteua Kapten Mirisho Sarakikya kuwa Mkuu wa kwanza wa Jwtz akiwa na cheo cha Brigadier. Siku hizi cheo hicho kinaitwa Brigadier General.

..picha hiyo hapo chini inathibitisha kwamba Elisha Kavana alikuja kuwa Meja ktk Jwtz. Kumbuka kwamba wakati wa maasi Elisha Kavana alikuwa Luteni, na Mirisho Sarakikya alikuwa Kapten.

1723324654378.png
1723324654378.png
 
Labda ni kwa vile marehemu hasemwi vibaya, ila kwa kuweka rekodi sawa nadhani ni sawa kuelezea jambo hili kwa jinsi lilivyokuwa, kwani ni sehemu ya historia ya hii nchi tuliyopo leo na vizazi vyetu.

Kiukweli, kwa namna hadi Luteni Elisha Kavana anapendekezwa kuwa kiongozi badala ya Askari wa Kizungu, tayari wote wasiounga mkono uasi ule walikuwa chini ya Ulinzi, na kubaki waliounga mkono.

Wakati Oscar Kambona amefikishwa kwenye kambi ya Colito, Kavana hakuwa chini ya ulinzi, na alikuwa miongoni mwa waliopiga yowe kumkataa Alex Nyirenda aliyetajwa awali kuwa kiongozi.

Hii ni tofauti na ilivyokuwa kwa Mirisho Sarakikya kwa kambi ya Tabora, ambaye aliteuliwa kuwa kiongozi huku akiwa mahabusu, kwani ilibidi atolewe mahabusu na kupewa taarifa, kisha akatoa amri ya kusitisha uasi.

Lakini, Kavana alitajwa jina lake kwa kupendekezwa huku mwenyewe akiwepo na kuvishwa kofia palepale na kushangiliwa, mbele ya Kambona ambaye wakati huo alikuwa ndiye Waziri wa Ulinzi.

Uamuzi uliompa uongozi Kavana ulifanywa na Kambona kwa shinikizo la Sgt. Ilogi na askari waliokuwako Colito wakati huo, akiwemo Kavana, wakimtisha kumpiga risasi Kambona asipotii matakwa yao.

RIP Mzee Elisha Kavana.

Ova
RIP Mzee Kavana.

Kama na yeye kaandika itakuwa vizuri sana. Hata kama kwa kuandika mambo yachapishwe baada ya yeye kufariki.

Hawa wazee wa 1964 mutiny wameishi kwa kujistukia sana Tanzania.
 
RIP Mzee Kavana.

Kama na yeye kaandika itakuwa vizuri sana. Jata kama kwa kuandika mambo yachapishwe baada ya yeye kufariki.

Hawa wazee wa 1964 mutiny wameishi kwa kujistukia sana Tanzania.
Ni kweli kujistukia kuliwaathiri sana. Hata Nyirenda aliamua kuachana na jeshi kabisa akaenda kuajiriwa na BP, nao wakampeleka Zambia kwenye tawi lao la huko.

Ova
 
..ngoja nianze mbali kidogo, nitakuomba uwe nami.

..Mkuu wa Tanganyika Rifles alikuwa mzungu Brigadier.Patrick Sholto Douglas.

..maasi ya Tanganyika Rifles yalifanywa na non commissioned officer waliokuwa wakidai mishahara, vyeo, na africanization jeshini.

..wakati wa maasi maofisa wote walikamatwa na kutupwa rumande. Maafisa wa Kizungu waliamriwa kurudi kwao Uingereza.

..zoezi la kumpata mkuu mpya wa Tanganyika Rifles lilianza na Alexander Nyirenda alikataliwa alipopendekezwa.

..baada ya hapo ndipo akapendekezwa Luteni Elisha Kavana. Taarifa zinasema alitolewa mahabusu na kupachikwa cheo cha Brigadier badala ya mzungu ambaye alikuwa hatakiwi.

..hata ukisoma vitabu vya historia vinaeleza kwamba Elisha Kavana alionekana kushtushwa na tukio hilo na alilazimishwa na askari waasi kuchukua wadhifa huo.

..maasi hayo yalikuja kuzimwa kwa msaada wa askari toka Uingereza. baada ya hapo Mwalimu Nyerere alivunja jeshi la Tanganyika Rifles, na akaunda jeshi jipya, Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

..Mwalimu pia alimteua Kapten Mirisho Sarakikya kuwa Mkuu wa kwanza wa Jwtz akiwa na cheo cha Brigadier. Siku hizi cheo hicho kinaitwa Brigadier General.

..picha hiyo hapo chini inathibitisha kwamba Elisha Kavana alikuja kuwa Meja ktk Jwtz. Kumbuka kwamba wakati wa maasi Elisha Kavana alikuwa Luteni, na Mirisho Sarakikya alikuwa Kapten.

View attachment 3066470View attachment 3066470
Kavana alipandishwa na kuwa Meja na aliapishwa kuwa Naibu wa Sarakikya.

Ova
 
Alijihusisha na biashara au alipata ajira kuendeshea maisha baada ya jeshi?

Hatma (fate) ya maisha ya mtu ni ya kipekee sana. Huyu na elimu yake hiyo wakati kama huo ungefikiri dunia ilikuwa inamsubiri tu kutengeneza maisha yake zaidi ya hapo alipo ishia. Tukio la muda mfupi tu linaweza kubadili mwelekeo mzima wa maisha.
Nawafahamu watoto wake.....naamini alitafuta kazi mbadala.....maisha yakasonga....ingawa najua enzi zile alikuwa under ......muda mrefu sana......
 
Kiukweli, kwa namna hadi Luteni Elisha Kavana anapendekezwa kuwa kiongozi badala ya Askari wa Kizungu, tayari wote wasiounga mkono uasi ule walikuwa chini ya Ulinzi, na kubaki waliounga mkono.

Wakati Oscar Kambona amefikishwa kwenye kambi ya Colito, Kavana hakuwa chini ya ulinzi, na alikuwa miongoni mwa waliopiga yowe kumkataa Alex Nyirenda aliyetajwa awali kuwa kiongozi.

Hii ni tofauti na ilivyokuwa kwa Mirisho Sarakikya kwa kambi ya Tabora, ambaye aliteuliwa kuwa kiongozi huku akiwa mahabusu, kwani ilibidi atolewe mahabusu na kupewa taarifa, kisha akatoa amri ya kusitisha uasi.

Lakini, Kavana alitajwa jina lake kwa kupendekezwa huku mwenyewe akiwepo na kuvishwa kofia palepale na kushangiliwa, mbele ya Kambona ambaye wakati huo alikuwa ndiye Waziri wa Ulinzi.

Uamuzi uliompa uongozi Kavana ulifanywa na Kambona kwa shinikizo la Sgt. Ilogi na askari waliokuwako Colito wakati huo, akiwemo Kavana, wakimtisha kumpiga risasi Kambona asipotii matakwa yao.
Mkuu 'JokaKuu', mimi sijui lolote kuhusu mkasa huu, lakini nina 'interest' ya kutaka kujuwa.
'Version' unayo ieleza wewe, kidogo ni tofauti na hii hapo juu, iliyowekwa na mkuu 'Mdakuzi', (Bandiko #16); taarifa ambayo pia inafanana na ile ya yule Mdosi, ambayo nimekwisha kuelekeza kwake mara kadhaa.

Hizi picha mbili zinazo mwonyesha Mwalimu akikutana na hao makamanda wawili Sarakikya na Kavana, ni kama zilichukuliwa siku hiyo hiyo moja, tofauti tu ni kuwa picha moja wamevalia kofia na picha ya pili hawana kofia vichwani.
Sasa sijui kama hizi picha zilipigwa baada au kabla ya maasi!

Cc: JokaKuu.
 
Mkuu 'JokaKuu', mimi sijui lolote kuhusu mkasa huu, lakini nina 'interest' ya kutaka kujuwa.
'Version' unayo ieleza wewe, kidogo ni tofauti na hii hapo juu, iliyowekwa na mkuu 'Mdakuzi', (Bandiko #16); taarifa ambayo pia inafanana na ile ya yule Mdosi, ambayo nimekwisha kuelekeza kwake mara kadhaa.

Hizi picha mbili zinazo mwonyesha Mwalimu akikutana na hao makamanda wawili Sarakikya na Kavana, ni kama zilichukuliwa siku hiyo hiyo moja, tofauti tu ni kuwa picha moja wamevalia kofia na picha ya pili hawana kofia vichwani.
Sasa sijui kama hizi picha zilipigwa baada au kabla ya maasi!

Cc: JokaKuu.

..hizo ni picha baada ya maasi.

..ukisoma maelezo chini ya picha, Sarakikya, na Kavana, wanatambulishwa kama viongozi ktk jeshi jipya.

..Kielelezo cha pili ni collar ya uniform aliyovaa Mirisho Sarakikya.

..Collar hiyo inafanana na uniform za askari ngazi ya Kanali, Brigedia, kwenda juu.

..Kwasababu Sarakikya alikuwa ameteuliwa kuwa Mkuu wa majeshi na Brigedia ndio maana collar ya uniform yake ikawa tofauti na collar ya uniform ya Kavana.

..pia uniform ya Sarakikya kabla ya maasi isingekuwa na alama ktk collar kwasababu alikuwa na cheo cha Kapten.

..Hakuna mashaka kwamba picha ya Sarakikya na Kavana ni ya baada ya maasi.
 
Mzee Kavana, aliyekuwa Captain Kavana mwaka 1964 na aliyechagulia na askari wa Tanganyika Rifles walioasi ili awe kiongozi wao badala ya wazungu, amefariki jana 9/8/2024.

Captain Kavana wakati huo alikuwa hana hili wala lile huku askari waasi wakishinikiza kuwa kwa vile tumepata uhuru, lazima tuongozwe na muafrika, wakati huo kuna wimbi la Africanisation ya sehemu zote za ungozi nchini.

Hili lilimletea matatizo mzee Kavana maana hakuhusika na maasi wala kuwepo kuyapanga , lakini askari wa chini ndiyo walipenda waongozwe na askari Ofisa mzalendo badala ya wazungu.

Mzee Kavana ameishi kwa utulivu na amani nyumbani kwake Chang'ombe miaka yote.

RIP Mzee Kavana
Hao sasa ndio walikua Vijana jeuri wenye uthubutu, Sio hawa Vijana wa sasa hivi, kuna muda unakaa unawaza weee unajiuliza "sperms zilizotungisha mimba za hawa Vijana wa style hii zilikua zimekomaa kweli? Au zilikua fake maybe au zilikua zina shida gani?" Basi unaishia Tu kuumia.
 
Back
Top Bottom