Mzee Majuto azidiwa tena na kurejeshwa kulazwa Hospitalini

Mzee Majuto azidiwa tena na kurejeshwa kulazwa Hospitalini

Muigizaji na mchekeshaji wa siku nyingi, Amri Athuman maarufu Mzee Majuto, amelazwa tena katika Hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam, baada ya kuzidiwa.

Mke wa mwigizaji huyo, Aisha Yusufu, ameiambia MCL Digital leo Aprili 23 kwamba mume wake walimpeleka hospitalini hapo leo saa 7:00 mchana.

Aisha amesema kidonda alichofanyiwa upasuaji kimeleta shida, hivyo kumpeleka kwa ajili ya uangalizi zaidi.

Majuto alilazwa hospitalini hapo Januari mwaka huu na kufanyiwa upasuaji wa tezi dume.

Source: Mwananchi
Hivi huyu Majuto kama anaumwa kila siku, anapataga wapi muda wa kufanya matangazo ya Neel Salt?
 
Haya ccm green mamba jitokezeni haraka sio msubiri mtu akate kamba ndio mje kubeba sanduku
 
Nilisikia Kikwete kamuahidi kumpeleka India, imefikia wapi?

Pole sana mzee majuto.
 
Kukumis tu..
You are in my Talks
You are in my Eyes
You are in my feelings
You are in my Thoughts
You are in my Work
You are in my Mind
You are in my Breath
You are in my Dreams
You are in my Prayers
You are in my Life
Because you are in my Heart...... And I miss you too [emoji8]
 
Pole Mzee wetu ndo uzee tena huu unakufata na magonjwa, mungu akuponye tunakuombea.
 
Pole Mzee Majuto, Mungu akusaidie. Ila mtoa mada nadhani hili sio jukwaa mujarab kwa uzi huu.
 
Nimekumbuka vile vi shuka anafungaga, kuna MTU anajifunga kama yeye dah nachekaga sana.
 
Dar es Salaam. Muigizaji na mchekeshaji wa siku nyingi, Amri Athuman maarufu Mzee Majuto, amelazwa tena katika Hospitali ya Tumaini jijini Dar es Salaam, baada ya kuzidiwa.

Mke wa mwigizaji huyo, Aisha Yusufu, ameiambia MCL Digital leo Aprili 23 kwamba mume wake walimpeleka hospitalini hapo leo saa 7:00 mchana.

Aisha amesema kidonda alichofanyiwa upasuaji kimeleta shida, hivyo kumpeleka kwa ajili ya uangalizi zaidi.

Majuto alilazwa hospitalini hapo Januari mwaka huu na kufanyiwa upasuaji wa tezi dume.

Source: Mwananchi
Pole mzee wa nil salt
 
Back
Top Bottom