Elections 2015 Mzee Mkapa: Wanaosema Wanataka Kuikomboa Tanzania ni Wapumbavu na Malofa

Elections 2015 Mzee Mkapa: Wanaosema Wanataka Kuikomboa Tanzania ni Wapumbavu na Malofa

mkapa katutukana si wapinzani tu ila watanzania wote kwa sababu kama ccm walituibia ukianza na meremeta, epa, kiwira, twiga wetu, tembo, migodini rada n.k kote huko hakuna mwizi aliyeshughulikiwa na bado ikashinda 2005, 2010 watanzania wakasema mko safi muendelee kutuongoza kwa nini tusiwe malofa na wapumbavu mkapa kamaliza mzee wa uwaz na ukweli kazi kwetu. habar ndio hiyo

Kila mtanzania ametukanwa na Mkapa
 
watanzania wamepashwa na waelewe kwa kuwa ccm kupitia mkapa ujumbe umefikishwa kwetu kwa mana upinzani walikuwa wanapiga kelele kwamba tunaibiwa na huo ni ukweli kwa hiyo tusi la mkapa ni letu wote hasa wale walioichagua ccm
 
Wasomi na viongozi wa dini wamesikitishwa Sana na kauli ya Mkapa aliposema wenyemawazo mbadala na CCM ni wapumbavu na malofa.Hii kauli imepingwa kila kona ya nchi hii
 
Wagombea wote walitangaza nia mbona magufuli sikumbuki alitangazia nia wap?au alishtukizwa?bc hajajiandaa asubiri kumpa nchi mtu ambae hajajiandaa ndio wale wale wa maisha bora kwa kila mtz
 
Lofa ni neon la kiingereza yaani Loafer. Lofa ni mvivu hivyo viongozi na hasa wale aliowalenga ni wavivu wa kufikiri. Na sio wananchi aliosema. Sisi JF tunatumiwa kusema uwongo na tunafundisha watoto wetu kuwa waongo.
 
Duuu kwani hiyo kauli ina maaana gani kama ci uthalilishaji..
 
Nikutafute wewe utanisaidia nini maishani mwangu? Umekuwa Mungu! Mimi siyo nyumbu kwa taarifa yako!

Kaka au sijui dada,jazba ni alama ya upeo finyu wa kufikiri.
Kwa hoja zako humu,unaonyesha unasimama tu ili uhesabiwe na wewe upate perday ila umefilisika kimtindo!
 
ESCROW walewale wamepeta Vijisenti joka lenye makengeza, Hela ya mboga ,kusaini mikataba mibovu n.k wanategemea kurudi tena kutuongoza malofa na W apumbavu
 
Wadau Salaam,
Ni wazi sasa mgombea urais kupitia UKAWA Mhe. Edward Lowassa amekuja kuwaonyesha aina mpya ya siasa ambayo wapinzani hawakuizoea, siasa ya kukaa karibu na wananchi kwa kuwatembelea katika mazingira yao na kujua shida zao. Kwangu mimi hii ni mbinu kali sana kisiasa, utakumbuka mbinu hii imetumiwa sana na katibu mkuu wa CCM ndugu Kinana hivi karibuni na imefanikiwa kuirejesha CCM angalau kwenye mstari maana ilikuwa ICU.

Hakika Mhe. Lowassa anafanikiwa kwenye hili kwa maana tulizoea upinzani wa kuporomosha maneno makali ya kejeli lakini cha kushangaza mtindo huo wa kejeli tena usio na hoja umehamia kwa jirani zao wa CCM tena ma senior wa chama kama mzee Mkapa ndio vinara wa hili. Mkapa aliamua kuwatukana watanzania wenzake kwa kuwaita WAPUMBAVU na MALOFA kwa sababu tu wanadai UKOMBOZI WA MTANZANIA. Mzee wangu Mkapa amesahau kuwa neno UKOMBOZI ni DHANA na sio lazima limaanishe ukombozi kutoka kwenye ukoloni tu bali mtu unaweza kuhitaji ukombozi katika mazingira mbalimbali ya kisiasa,ki jamii, na hata kiuchumi.

Kwa fikra zangu za kipumbavu na ki Lofa nakiona kifo cha CCM kama itaendeleza siasa za aina hii tena zikiendeshwa na watu wakubwa kama mzee wangu Mkapa
 
tangu juzi mkapa ametoa maneno ya kuwaita viongozi wa chadema na wanaojiunga nao kuwa niwapumbavu na malofa kusema wao ni chama cha ukombozi wakati ukombozi ulishafanyika chini ya vyama vya tanu na asp,wamejitokeza watu wengi kwenye mitandao na kuonyesha kukerwa na kauri hizo nawangine kuongeza chumvi na kusema amewatukana watanzania kitu ambacho sio kweli pengine wengi hawakumsikiliza maelezo aliyoyatoa juu ya kauri yake,

kwangu pengine ni sawa anatakiwa kujitokeza kuomba msamaha au kutoa ufafanuzi tena juu ya kauri yake

lakini kwangu nilichojiuliza na kuona kama ni unafiki na ushabiki kwa wengi kwenye mitandao na baadhi ya watu muhimu kama baregu na mwandosya ambao wameeleza hisia zao zidi ya kauri ya mkapa,mimi nawauliza swali mbona hamkujitokeza zidi ya matusi na kejeri zilizotolewa juu ya magufuli mbeya na arusha?

Nawakumbusha hayo matusi na kejeri za kipuuzi zilizotolewa na viongozi wa chadema mbele ya viongozi wa kuu nakushangilia,
1.magufuli ni bamed
2,magufuli mwisho milagoni mwa gest
3,magufuli analopoka ovyoovyo tu
4,magufuli hana akili
5,john pombe magufuli ni pombe tu hana lolote

nawauliza mbona hamkujitokeza kukemea kauri hizo na kusema ni za kumzalilisho kiongozi hiyo badara yake leo hii mnaona kauri ya mkapa ndo ya kujadiri kuriko kitu chochote ,
narudia kusema huu ni unafiki tu wa baadhi ya watu kweli pengine mkapa kakosea lakini mjie hata na wengine nao ni binadamu kama mlivyokose nyie na mkapa kakose
tuache ushabili maana naona kuna watu wameifanya kama ndo mtaji wao wa kisiasa kila mtandao kila blog ,hii sio sawa ,
 
wadau salaam,
ni wazi sasa mgombea urais kupitia ukawa mhe. Edward lowassa amekuja kuwaonyesha aina mpya ya siasa ambayo wapinzani hawakuizoea, siasa ya kukaa karibu na wananchi kwa kuwatembelea katika mazingira yao na kujua shida zao. Kwangu mimi hii ni mbinu kali sana kisiasa, utakumbuka mbinu hii imetumiwa sana na katibu mkuu wa ccm ndugu kinana hivi karibuni na imefanikiwa kuirejesha ccm angalau kwenye mstari maana ilikuwa icu.

Hakika mhe. Lowassa anafanikiwa kwenye hili kwa maana tulizoea upinzani wa kuporomosha maneno makali ya kejeli lakini cha kushangaza mtindo huo wa kejeli tena usio na hoja umehamia kwa jirani zao wa ccm tena ma senior wa chama kama mzee mkapa ndio vinara wa hili. Mkapa aliamua kuwatukana watanzania wenzake kwa kuwaita wapumbavu na malofa kwa sababu tu wanadai ukombozi wa mtanzania. Mzee wangu mkapa amesahau kuwa neno ukombozi ni dhana na sio lazima limaanishe ukombozi kutoka kwenye ukoloni tu bali mtu unaweza kuhitaji ukombozi katika mazingira mbalimbali ya kisiasa,ki jamii, na hata kiuchumi.

Kwa fikra zangu za kipumbavu na ki lofa nakiona kifo cha ccm kama itaendeleza siasa za aina hii tena zikiendeshwa na watu wakubwa kama mzee wangu mkapa

wewe ili ndo unaliona la kujitwisha mbona matusi ya mbeya na arusha zidi ya magufuli haukujitwisha kama unavyojitwisha kauri ya mkapa,
kama wewe ni muungwanai ungeanza na matusi na kejeri zidi ya magufuli yaliyotolewambele ya viongozi wa cdm arusha na mbeya na kumuita bamed,hana akili,analopoka ovyoovyo,mwisho wake gest,hapo ndo nigeona kweli wewe unatenda haki zidi ya viongozi na pengine unaweza kuwaeleza viongozi manbo ya msingi kuriko wao kujisahau,
 
Mbona hueleweki.... Mifano yako haiendani na aina ya watu unaowazungumzia na maneno unayoyamaanisha hayafananiii...

so umeandika c.r.a.p
 
wadau salaam,
ni wazi sasa mgombea urais kupitia ukawa mhe. Edward lowassa amekuja kuwaonyesha aina mpya ya siasa ambayo wapinzani hawakuizoea, siasa ya kukaa karibu na wananchi kwa kuwatembelea katika mazingira yao na kujua shida zao. Kwangu mimi hii ni mbinu kali sana kisiasa, utakumbuka mbinu hii imetumiwa sana na katibu mkuu wa ccm ndugu kinana hivi karibuni na imefanikiwa kuirejesha ccm angalau kwenye mstari maana ilikuwa icu.

Hakika mhe. Lowassa anafanikiwa kwenye hili kwa maana tulizoea upinzani wa kuporomosha maneno makali ya kejeli lakini cha kushangaza mtindo huo wa kejeli tena usio na hoja umehamia kwa jirani zao wa ccm tena ma senior wa chama kama mzee mkapa ndio vinara wa hili. Mkapa aliamua kuwatukana watanzania wenzake kwa kuwaita wapumbavu na malofa kwa sababu tu wanadai ukombozi wa mtanzania. Mzee wangu mkapa amesahau kuwa neno ukombozi ni dhana na sio lazima limaanishe ukombozi kutoka kwenye ukoloni tu bali mtu unaweza kuhitaji ukombozi katika mazingira mbalimbali ya kisiasa,ki jamii, na hata kiuchumi.

Kwa fikra zangu za kipumbavu na ki lofa nakiona kifo cha ccm kama itaendeleza siasa za aina hii tena zikiendeshwa na watu wakubwa kama mzee wangu mkapa

matusi ya mbeya na arusha haukuyaona wala kuyasikia hila ya mkapa ndo umeyaona tenda haki na haki itakufanya uwe uhuru kifra,
 
attachment.php
 
Back
Top Bottom