Mzee wangu yupo hoi, huenda Serikali ingeweka wazi, Mzee wangu asingeshiriki kuzika rafiki yao aliyefariki kwa changamoto

Mzee wangu yupo hoi, huenda Serikali ingeweka wazi, Mzee wangu asingeshiriki kuzika rafiki yao aliyefariki kwa changamoto

HII habari kama si'' kahawa ya asubuhi'' au'' hadithi za shigongo,'' inasikitisha sana!
 
Pole ndugu.

Jambo moja ni lazima kifo kiletwe na sababu ambayo kibinadamu tunasema ingeepukika hua tunasema Kwa nini*********?.*

Embu fikiria nchi zenye lockdown bado watu wapukutika tu je hawa wailaumu serikali? Suala jema ni wenyewe kuchukua tahadhar hasa misibani kwa mtu aliyesadikika kuondoshwa na covid, vaa barakoa, sanitizer mfukoni, kuachiana nafasi na sehemu zingine vivyo hivyo.
Tukiendelea kuilaumu serikali tukiendelea kuisubiri serikali tunaoumia ni sisi wenyewe.

Tuchukue tahadhari kulaumu ni kujiumiza ikiwa mlaumiwa hana limuingialo.

MLINZI WA AFYA YAKO NI WEWE MWENYEWE.
Watu hatuijaji lockdown lakini ile tamko na zile taarifa za hapa na pale za kujilinda zinatosha... Sasaivi hata vyombo vya habar wanaogop kusema kama kuna mdudu... Emu rudisha kumbukumbu zako mwaka jana mwezi wa tatu corona ilivyotangazwa, hadi vijijini ukienda unakutana nje kwenye magenge kuna ndoo ya maji ya kunawa...sasaivi ukimwambia mtu nawa mikono vaa barakoa anakwambia tuliambiwa hamna corona...hii hali unaionaje?
 
Kufa angekufa tu hata kwa kuchomwa na miiba kwa hiyo kama mpango wa Mungu ni kumuua baba yako na atakufa.
Kwahio wale watoto wanaokufa kwa kubakwa na kuuliwa hio ni plan ya Mungu (duh kweli master plan za huyo Mungu wako leaves a lot to be desired)

Kuhusu kufa kila mtu atakufa.., ila hii isiwe sababu watu kujirusha kutoka kwenye magorofa au kulala barabarani eti sababu mwisho wa siku watakufa...., (every minute kwenye hii dunia wewe kama nguvu kazi ni asset kwa jamii inayokuzunguka) unless otherwise wewe ni mchawi hence kuondoka kwako huenda kukawa ni neema...
 
Watu mnapenda propaganda za kijinga sana nchi hii.
Kwahiyo Rais asiposema kuna Corona nyie hamtachukua tahadhari?
Hii nchi imejaa pimbi wengi, kwahiyo unamlaumu Rais kwa uzembe wa baba yako?
Rais kashasema watu wachukue tahadhari na waendelee kumuomba Mungu, nyie mlitakaje ili mchukue tahadhari?
 
Naandika huku naumia sana.

Maisha ya mzee wangu yako hatarini sana anapumua kwa shida sana.

Chanzo cha kuumwa.
Kuna rafiki yao mzee mwenzao alifariki, wakaambiwa kuwa chanzo cha kifo cha huyo rafiki yao ni mapafu.
Kutoka hospital ya Bugando ndugu wa marehemu walipewa mwili kwenda kuzika kijijini geita bila tahadhari wakiamini kafa kwa ugonjwa wa kawaida.

Alipofikishwa huko kijijini, ndipo wazee wenzake wakawa wamejiandaa kumzika mwenzao kama ilivyo ada yao.
Jukumu la kubeba mwili kuzika, lilifanywa na wazee kama ishara ya heshima kwa mwenzao.
Miongoni mwa wazee hao! Na mzee wangu alishiriki.

Msiba ulikuwa na msongamano mkubwa kama ada na mila za vijijini.

Wazee hawa maskini ya Mungu pasipo kujua walibeba mwili bila tahadhari! Hadi atua ya mwisho ya kumzika mwenzao.

Baada ya hapo jioni mzee akanisimulia ilivyokuwa, akadai pia walibeba na jeneza liliwavujia majimaji.
Baada ya siku kadhaa wazee hawa wameanza kuumwa.
Watatu wana hali mbaya sana, na mzee wangu usiku wa kuamkia Leo kabanwa mbavu haswa! Ametumia dawa ya malimao, vitunguu, pilipili na tangawizi lakini hali si hali, kwanza kaanza kuchanganyiwa na haongei tena.
Yuko hospital kalazwa lakini hali ni mbaya sana.
Huenda serikali wangetangaza tahadhari hasa misibani haya yasingetokea.
Huenda serikali ingetangaza wazi misiba ya korona ingezikwa na vijana walivalia kinga.
Hapa najaribu kuwaza kama hali iko hivi, maambukizi yameathiri wangapi kwa uzembe wa serikali?

Hatuhitaji lockdown, lakini chamhimu tamko litoke lifike hata kijijini watu wapewe mbinu.

Imeniuma sana kwa uzembe huu mkubwa! Kama nitapoteza busara za mzee wangu, yamkini na mama yangu atakuwa kaambukizwa maana wanalala pamoja mda wote wa kuuguza.

Yamkini tungeweza kuwalinda wazee lakini watoto wa shule hawa wadogo bado ni Carrier wa kuleta homa hiyo nyumbani.
Serikali ingefunga shule hata kwa miezi miwili ingesaidia kupunguza kasi kama mwaka 2020 sambamba na kuchukua tahadhari.

Utafaa nini utajiri katikati ya misiba?

Serikali ingeweza hata kuja na mikakati, kama hawana pesa za chanjo, wangeipokea hata watu wakachomwa kwa hiari hata kwa malipo tungelipa.

Katiba imuondolee mamlaka mtu mmoja kutegemewa kutoa tamko ili kuliokoa taifa.

Inauma sana.

Kipimo ni katika msiba wa Maalim. Waombolezaji walikuwa wameonywa hatari ya kuambukizana wao kwa wao au hata tahadhari za kuchuku?

Hawa jamaa wameasababisha vifo vingi.

Pole sana mkuu.

Mwenyezi Mungu na akamfanyie wepesi mzee wako. Apone upesi na aje kusaidia katika vita vya kuokoa wengine.

Hawa wanaotuhami kwa maombi hali mikono yao imejaa damu hawana lolote!
 
Watu mnapenda propaganda za kijinga sana nchi hii.
Kwahiyo Rais asiposema kuna Corona nyie hamtachukua tahadhari?
Hii nchi imejaa pimbi wengi, kwahiyo unamlaumu Rais kwa uzembe wa baba yako?
Rais kashasema watu wachukue tahadhari na waendelee kumuomba Mungu, nyie mlitakaje ili mchukue tahadhari?
Huyo aliyefariki sababu ya corona ,kama serikali ingekuwa makini asingefikishwa hata huko kijijini kuzikwa.Alitakiwa azikwe na serikali.Rejea mazishi ya mtu aliyefariki kwa magonjwa ya milipuko kama kipindupindu,ebola n.k
 
Halafu goigoi fulani linacomment mahali huko kuwa serekali itoe miongozo ya nini kwani huwezi kujikinga!😬😬😬Imagine hata mtu akifa kwa Corona hospitalini, hakuna kuambiwa kuwa kafa kwa Corona ili mchukue tahadhari achilia mbali kutahadharishwa kuwa kazikeni kwa tahadhari.Tanzania kipindi hiki imepatikana walahi!🚶🚶🚶
Ni kujiongeza tu rafiki, mtu akifa kwa tatizo la upumuaji basi nyie ndugu chukueni tahadhari. Pole sana mtoa mada
 
Kufa angekufa tu hata kwa kuchomwa na miiba kwa hiyo kama mpango wa Mungu ni kumuua baba yako na atakufa.
Unaona je tufanye ni mpango wa Mungu ukanunue kamba ujinyonge?

Hii mijamaa:


IMG_20210218_174254_207.jpg


na chizi nijo ni mzigo sana kwa taifa hili.
 
Ni kujiongeza tu rafiki, mtu akifa kwa tatizo la upumuaji basi nyie ndugu chukueni tahadhari. Pole sana mtoa mada
Mimi nawashauri wazee kijijini kwetu msiba wowote unaotokea mjini, kama ajali haijahusika, wasihudhurie hata kama waliofariki ni watoto wao.Full Stop!
 
Watu mnapenda propaganda za kijinga sana nchi hii.
Kwahiyo Rais asiposema kuna Corona nyie hamtachukua tahadhari?
Hii nchi imejaa pimbi wengi, kwahiyo unamlaumu Rais kwa uzembe wa baba yako?
Rais kashasema watu wachukue tahadhari na waendelee kumuomba Mungu, nyie mlitakaje ili mchukue tahadhari?
Kwahyo hata ile combine iliyokuleta duniani nayo ni mapimbi sio? Je wajomba zako walioko kiparanga ambapo hakuna hata network zaid ya kusikiliza Radio watajuje kuwa korona ipo ili wachukue tahadhari? Sawa Rais kasema tuchukue tahadhari vipi kuhusu kusambaza vipeperushi huko vijijin kuhusiana na tahadhari za mdudu endelea kula ugali kwa shemeji yako ambae ni kada wa mtukuf
 
nchi za wenzetukatiba zao zinaruhusu kuwa shughulikia viongozi wanao toa maagizo ambayo baadae huleta athari kwa jamii mfano ni govana wa new york

 
Yaani nafsi yangu naipenda sana siwezi kusubiri mtu aniambie nichukue tahadhari. Nyumbani kwangu nina sauti inayosikilizwa na watu wanatii . Tunachukua tahadhari kwa kadri ya uwezo wetu . Inabidi kila mtu ailinde nafsi yake. Usiikabidhi nafsi iendeshwe na serikali shauri lako 🤓🤓🤓
 
Pole ndugu.

Jambo moja ni lazima kifo kiletwe na sababu ambayo kibinadamu tunasema ingeepukika hua tunasema Kwa nini*********?.*

Embu fikiria nchi zenye lockdown bado watu wapukutika tu je hawa wailaumu serikali? Suala jema ni wenyewe kuchukua tahadhar hasa misibani kwa mtu aliyesadikika kuondoshwa na covid, vaa barakoa, sanitizer mfukoni, kuachiana nafasi na sehemu zingine vivyo hivyo.
Tukiendelea kuilaumu serikali tukiendelea kuisubiri serikali tunaoumia ni sisi wenyewe.

Tuchukue tahadhari kulaumu ni kujiumiza ikiwa mlaumiwa hana limuingialo.

MLINZI WA AFYA YAKO NI WEWE MWENYEWE.

Hivi huyu serikali asiyelaumiwa wala kuwajibika kwa anaowasimamia ni nani hasa?

Hivi huyu serikali aliapa kuilinda katiba ambayo inamtaka pia kuhakikisha anawahami vilivyo walio nchini yake kwa kuhakikisha ikiwamo na kuwapa taarifa sahihi na kwa wakati kuhusiana na hatari na namna ya kujikinga na majanga yakiwamo magonjwa? Au amesahau?

Enyi:

IMG_20210218_174254_207.jpg


Huyu serikali kazi yake nini basi? Kuchukua kodi tu?

Tafadhalini angalieni kauli zenu au japo hata mmweleze kungali asubuhi, karibuni anapoteza uhalali wake.

Huu ndiyo ulio ukweri mchungu kweri kweri.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Pole sana. Mungu ni mweza wa yote pamoja na matibabu endeleeni kumuombea.
 
Back
Top Bottom