TANZIA Mzee William Mbunga mwandishi wa habari mkongwe afariki dunia

TANZIA Mzee William Mbunga mwandishi wa habari mkongwe afariki dunia

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
Habari zilizonifikia ni kuwa mzee William Mbunga mwandishi wa habari mkongwe, aliyepiga picha tukio maarufu uchanganyaji udongo kwenye Muungano wa Tanganiyika na Zanzibar amefariki Dunia tarehe 3/2/2021.

Pia ndiye muanzilishi wa shule ya uandishi wa habari SJMC.

Bwana ametoa, bwana ametwaa

mbuga.jpg

--
WILLIE MBUNGA: ALIYEPIGA PICHA YA MUUNGANO WA TANZANIA NA ZANZIBAR NA MWANZILISHI WA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI CHA SERIKALI NCHINI

Na Dereck Murusuri
O, so sad. Sad indeed. My mentor, Mzee wangu, rafiki na fellow lensman.

Mara ya mwisho tumewasiliana tarehe 19 November, 2020.

Alikuwa akitaka kuwepo na Degree ya upigaji picha na utengenezaji wa documentary za wanyama pori, ili kuboresha eneo hilo.

Alihoji, kwanini tuwe tunatumia zaidi picha za watu wa nje ya nchi kwenye Televisheni zetu, wanakuja wanatupigia na wanatuuzia wakati wanyama tunao hapa hapa kwetu?

Sisi ndio tulipaswa kuwauzia quality documentary.

Alinieleza kuwa SJMC (UDSM) tayari walikuwa wamekubali kuanzisha Programme hiyo na yeye alipewa jukumu la kusaidia kupata funding.

Sijui alifikia wapi, huenda Prof. Michael Andindilile atatueleza. Mzee mwanzilishi, kama alivyoanzisha Chuo cha Uandishi wa Habari, tayari ameshamaliza sehemu yake ya utumishi katika uso wa dunia.

Amekuwa anafanya kazi hadi dakika ya mwisho, kwake umri wake wa zaidi ya miaka themanini, haukuwa kikwazo. Lipo jambo kubwa la kujifunza katika utumishi endelevu.

Mtume Paulo katika maisha ya utumishi anasema, "Kuishi ni Kristo na Kufa ni faida (to gain)."

Ni Mzee Willie Mbunga aliyeipiga ile picha ya MUUNGANO ya kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar. Picha ambayo aliipiga siku moja na itabakia ishara ya Muungano milele na milele.

Amelitumiakia Taifa letu kwa ari, upendo mkubwa na bila kuchoka.

Ndiyo mwanzilishi wa Chuo cha Uandishi wa Habari cha Serikali nchini.

Nikiwa Afisa Habari Msaidizi pale Idara ya Habari, MAELEZO, chini ya Kaka yangu na Bosi wangu Raphael Hokororo, Mzee Mbunga hakuacha kuja na kututia moyo jinsi ya kuandika na kupiga picha za matukio ya Serikali.

Siku zote alikuwa Mwalimu kwetu na alituchukulia kama Baba kwa wanae.

Chuo alichokianzisha ndio SJMC ya leo, sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

SJMC imetoka mikononi mwa nyota hii iliyozima katika Hospitali ya Mloganzira.

Historia, kama Mkuu wa Chuo cha Uandishi wa Habari cha kwanza cha Serikali nchini, nayo imeandikwa kwa kalamu ya chuma.

Hata kama yeye amefariki dunia, historia aliyoitengeneza kwa muda wake duniani haitafutika kamwe.
 
Hapana , huyo ni marehemu Mangi wa wachaga marehemu Petro Itosi Marealle! Hawa warundi wakina Jiwe wanakula wasivyopanda, sisi wachaga tulimbeba sana Nyerere katika harakati za kupata uhuru wa nchi hii!!
Poleni kwa msiba.

Huyu Mangi ndiye aliyeuandika Ujamaa vizuri, Nyerere akasoma, akayachukua yale maandishi na kuyafanya dira ya nchi.

Kwa mujibu wa Paul Bjerk katika kitabu chake "Building A Peaceful Nation: Julius Nyerere And The Establishment of Sovereignty In Tanzania 1960-1964"
 
Habari zilizonifikia ni kuwa mzee william Mbunga mwandishi wa habari mkongwe, aliepiga picha tukio maarufu uchanganyaji udongo kwenye muungano wa Tanganiyika na Zanzibar amefariki Dunia tarehe 3/2/2020.
Pia ndiye muanzilishi wa shule ya uandishi wa habari SJMC.
Bwana ametoa, bwana ametwaaView attachment 1693796pumzika kwa amani
 
Hapana , huyo ni marehemu Mangi wa wachaga marehemu Petro Itosi Marealle! Hawa warundi wakina Jiwe wanakula wasivyopanda, sisi wachaga tulimbeba sana Nyerere katika harakati za kupata uhuru wa nchi hii!!
WE WERE A PROTECTORATE, AT ANY TIME WE WOULD HAVE GOTTEN OUR INDEPENDENCE
 
I'm sorry for asking this? why was he alone on that picture ? Where was the president of Zanzibar? Actually the event was very important but i would expect to see them together on that picture.
In all in all, a lot of thanks to the Cameraman for taking this picture, at least, i' m going to have something to show my grandkids . R . I . P
 
WILLIE MBUNGA: ALIYEPIGA PICHA YA MUUNGANO WA TANZANIA NA ZANZIBAR NA MWANZILISHI WA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI CHA SERIKALI NCHINI

Na Dereck Murusuri
O, so sad. Sad indeed. My mentor, Mzee wangu, rafiki na fellow lensman.

Mara ya mwisho tumewasiliana tarehe 19 November, 2020.

Alikuwa akitaka kuwepo na Degree ya upigaji picha na utengenezaji wa documentary za wanyama pori, ili kuboresha eneo hilo.

Alihoji, kwanini tuwe tunatumia zaidi picha za watu wa nje ya nchi kwenye Televisheni zetu, wanakuja wanatupigia na wanatuuzia wakati wanyama tunao hapa hapa kwetu?

Sisi ndio tulipaswa kuwauzia quality documentary.

Alinieleza kuwa SJMC (UDSM) tayari walikuwa wamekubali kuanzisha Programme hiyo na yeye alipewa jukumu la kusaidia kupata funding.

Sijui alifikia wapi, huenda Prof. Michael Andindilile atatueleza. Mzee mwanzilishi, kama alivyoanzisha Chuo cha Uandishi wa Habari, tayari ameshamaliza sehemu yake ya utumishi katika uso wa dunia.

Amekuwa anafanya kazi hadi dakika ya mwisho, kwake umri wake wa zaidi ya miaka themanini, haukuwa kikwazo. Lipo jambo kubwa la kujifunza katika utumishi endelevu.

Mtume Paulo katika maisha ya utumishi anasema, "Kuishi ni Kristo na Kufa ni faida (to gain)."

Ni Mzee Willie Mbunga aliyeipiga ile picha ya MUUNGANO ya kuchanganya udongo wa Tanganyika na Zanzibar. Picha ambayo aliipiga siku moja na itabakia ishara ya Muungano milele na milele.

Amelitumiakia Taifa letu kwa ari, upendo mkubwa na bila kuchoka.

Ndiyo mwanzilishi wa Chuo cha Uandishi wa Habari cha Serikali nchini.

Nikiwa Afisa Habari Msaidizi pale Idara ya Habari, MAELEZO, chini ya Kaka yangu na Bosi wangu Raphael Hokororo, Mzee Mbunga hakuacha kuja na kututia moyo jinsi ya kuandika na kupiga picha za matukio ya Serikali.

Siku zote alikuwa Mwalimu kwetu na alituchukulia kama Baba kwa wanae.

Chuo alichokianzisha ndio SJMC ya leo, sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

SJMC imetoka mikononi mwa nyota hii iliyozima katika Hospitali ya Mloganzira.

Historia, kama Mkuu wa Chuo cha Uandishi wa Habari cha kwanza cha Serikali nchini, nayo imeandikwa kwa kalamu ya chuma.

Hata kama yeye amefariki dunia, historia aliyoitengeneza kwa muda wake duniani haitafutika kamwe.
 
Habari zilizonifikia ni kuwa mzee William Mbunga mwandishi wa habari mkongwe, aliyepiga picha tukio maarufu uchanganyaji udongo kwenye Muungano wa Tanganiyika na Zanzibar amefariki Dunia tarehe 3/2/2020.

Pia ndiye muanzilishi wa shule ya uandishi wa habari SJMC.

Bwana ametoa, bwana ametwaa

View attachment 1693796
Kuweka rekodi vizuri. Ndie mwanzilishi wa Chuo cha Uandishi sa Habari TSJ kilikuwa pale jeshi la Wokovu kabla ya kuhamia Ilala. TSJ kilichukuliwa na UDSM na kuzaliwa IJMC kabla ya kubadilishwa na kuwa SJMC.
 
Habari zilizonifikia ni kuwa mzee William Mbunga mwandishi wa habari mkongwe, aliyepiga picha tukio maarufu uchanganyaji udongo kwenye Muungano wa Tanganiyika na Zanzibar amefariki Dunia tarehe 3/2/2020.

Pia ndiye muanzilishi wa shule ya uandishi wa habari SJMC.

Bwana ametoa, bwana ametwaa

View attachment 1693796
2021 na si 2020
R.I.P William Mbunga
 
Habari zilizonifikia ni kuwa mzee William Mbunga mwandishi wa habari mkongwe, aliyepiga picha tukio maarufu uchanganyaji udongo kwenye Muungano wa Tanganiyika na Zanzibar amefariki Dunia tarehe 3/2/2020.

Pia ndiye muanzilishi wa shule ya uandishi wa habari SJMC.

Bwana ametoa, bwana ametwaa

View attachment 1693796
03/02/2020 ndiyo unaleta leo? Au ni 2021?
 
Back
Top Bottom