Mzee Yusufu kumtema mkewe baada ya kugoma kuacha kuimba taarabu kama alivyofanya

Yeye alipoamua kugeuza kibao hawakushauriana na familia yake? Au alukurupuka tu? Au walimkatalia akaamua kuingia peke yake?
 
Huyu naye wivu tu unamsumbua anajua wanayofanyaga kwenye shoo za usiku
 
Mbaazi ikikoswa matunda husingizia jua
 
Mnaomtetea huyo mwanamama em'jaribuni kama wanaume kuvivaa viatu vya mumewe...kwamba wangapi mpo tayari wake zenu warudi majumbani mwenu saa10 alfajiri kutoka kuimba huku ndani mna familia?watoto kuwaandaa shule asubuhi na mengineyo?!jamii inayokuzunguka itakuchukuliaje?sio kuwa mwanamuziki tu mkeo hata akiwa mnywa pombe ni mt'hani kweli kweli huyo mwanamama akikataa kufanya anachokitaka mumewe ampe tu talaka akafie mbali maisha ya mke na mume kuheshimiana sio tofauti na hivyo!
 
Nasikia wanaume wakifa wanapewa wanawake malaika 70, sasa wanawake je nao wanapewa malaika wangapi? Mi nafikiri hata wakipewa 5 tu shughuli yake si mchezo!
 
Huyu naye asituzingue. Lolote analolifanya sasa linamchango mkubwa toka kwenye hiyo kazi ya laana anayosema. Hata akifanya biashara halali atafanikiwa sababu ya umaarufu alioupata kwenye kazi ya dhambi,hana pakutokea
 
Kwahiyo ukiimba taarabu una kwenda Motoni??
 
We mungu wako ni yupi? Manake mvaa nepi unasema wa wazungu
 
Kwa hiyo mungu wako wewe anapenda muziki wa taarabu uliojaa masimango na matusi kumbee,,una mungu mlevi na muhuni wewe
 
We nadhani mungu lbilisi anayewafundisha wazungu kutengeneza vitu vya muda hapa duniani na wakifa wanaviacha hapa hapa duniani na havitawasaidia huko mbiguni
 
Nilishasemaga mimi..sitokuja kuolewa na mwanaume mwenye gubu kama hili milele[emoji46]!

Mawifi wanagubu sijawahi kuona[emoji35]...sasa huyo Khadija sijui anataka kuolewa na kaka yake?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…