Mzee Yusuph amkataa mtoto aliyedai ni mwanae wa nje ya ndoa

Mzee Yusuph amkataa mtoto aliyedai ni mwanae wa nje ya ndoa

aliyekwambia Sheria za dini hazifatwi ni nani? Waislamu linapokuja suala la Mirathi, Talaka, Ndoa sheria za dini zinafatwa mkuu labda usitake tu mwenyewe, kwahiyo huyo dogo hawezi kutoboa hata kama ni wake kweli.
Hakuna kitu kama hicho nimeshuhudia kesi za aina hiyo nyingi zinaishia kuamuliwa watoto wote kurithi bila kujali mtoto kazaliwa ndani ya ndoa au nje ndoa.
 
Ila Mungu fundi watoto wa nje huwa wanakuja copy & paste .. tukija kwenye sharia ya Dini sio mwanae huyo ... Hata huo ubini alitakiwa achukue kwa mama yake
Ila akipata pesa anakua wakwake
 
Kijana mmoja aliyejitambulisha kwa majina ya Ahmad Yusuph Mzee, amejitokeza hadharani katika studio za Wasafi Media akidai kwamba yeye ni mtoto wa mzee Yusuph wa damu kabisa ambapo anasema kwamba mama yake ambaye ni Marehemu kwa sasa alipewa ujauzito na Mzee Yusuph wakati alipokuwa akihudumu kama MC kwenye moja ya kumbi iliyokuwa hu
Hizi kesi pelekeni huko Zanzibar
 
Hakuna kitu kama hicho nimeshuhudia kesi za aina hiyo nyingi zinaishia kuamuliwa watoto wote kurithi bila kujali mtoto kazaliwa ndani ya ndoa au nje ndoa.

icho kitu kipo mkuu, labda wao wenyewe hawakufata taratibu zinazotakiwa.
 
Duuuuuuh basi hiyo dini ni hatari, eti mtoto ni mama kwamba alijipa mimba yeye mwenyewe bila ya kuwepo mwanaume 🤔🤔🤔🤔
 
Kijana mmoja aliyejitambulisha kwa majina ya Ahmad Yusuph Mzee, amejitokeza hadharani katika studio za Wasafi Media akidai kwamba yeye ni mtoto wa mzee Yusuph wa damu kabisa ambapo anasema kwamba mama yake ambaye ni Marehemu kwa sasa alipewa ujauzito na Mzee Yusuph wakati alipokuwa akihudumu kama MC kwenye moja ya kumbi iliyokuwa huko Mbagala miaka ya 2002.

Ahmad anasema awali alikuwa akiishi na mama yake pamoja na mume wa mama yake ambaye awali alikuwa anamtambua kama baba yake mzazi, lakini kabla mama yake hajafariki alimweleza ukweli kwamba hakua baba yake wa kumzaa bali baba yake ni Mzee Yusuph ambaye ndiye huyu muimba taarabu.

Ahmad amesema licha ya kwamba anatambua kama Mzee ana mali za kutosha na ni mtu maarufu, yeye kipaumbele chake anataka wakapime DNA ajiridhishe kama kweli Mzee Yusuph ni baba yake mzazi ili awe na faraja pamoja na amani ya kujihisi yupo salama duniani kwani kwa maisha anayoishi sasa ni kwamba hana baba wala mama, maisha ambayo ni hatari na siyo kwamba anamtafuta ili apate upenyo wa kurithi mali.

Kwa upande wa Mzee Yusuph licha ya kufanana na mtoto huyo kuanzia Mapua, Mdomo, Mashavu, kichwa mpaka rangi ya meno na ngozi. Bila aibu Mzee amesema hamtambui kijana huyo kama mtoto wake na hana kumbukumbu kama aliwahi kucheza michezo ya hasara huko Mbagala kiasi cha kumpatia mwanamke ujauzito.

Awali Mzee Yusuph alikataa kabisa kupima DNA lakini baadae baada ya kushinikizwa alikubali kwenda kupima DNA lakini kwa masharti mazito, ambapo amesema kijana huyo akitaka wakapime DNA pesa ya vipimo aitafute mwenyewe kijana na andapo atakuta siyo mtoto wake basi hatua kali za kisheria za uzalilishaji zitachukuliwa dhidi yake, aidha Yusuph ameongeza kuwa kama akikuta mtoto huyo ni damu yake atamfikilia kama aendelee kumlea au aachane naye kwani dini yake inasema mtoto wa nje ya ndoa siyo mtoto wake ni wa mwanamke.
View attachment 2660998

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa hatari yake nini mtu mzima huyo? Hovyo sana.
 
Mtoto ni wa Mzee Yusuph hakuna haja ya DNA....features zinajielezea waziwazi...nimemuangalia mara mbilimbili ...labda upande wa kuhitimisha kisayansi umalizie.....shida ni kwamba dogo Hana pesa Hana maisha..,.Hivi dogo angekuwa mtu mkubwa Kaliba ya kina Diamond je Mzee angemkana? Namalizia Kwa kusema fu..k you shida[emoji1745]
 
aidha Yusuph ameongeza kuwa kama akikuta mtoto huyo ni damu yake atamfikilia kama aendelee kumlea au aachane naye kwani dini yake inasema mtoto wa nje ya ndoa siyo mtoto wake ni wa mwanamke.

Sent using Jamii Forums mobile app
Atuambie hiyo dini yake inaruhusu kuimba taarabu tena kwenye show wanajaa machoko kibao
 
ila wazanzibari tunafanana sn yote sababu wazee wetu wana watoto rundo hd kufikia hatua unaona ndugu bila kujua na majina yetu hy Ahmed, Ally, said ni common unapuuzia unaona nduguyo.
Wazee wapunguze mwendo
 
Back
Top Bottom