Mzee Yusuph Makamba: Nampongeza Rais Samia kwa mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, asema isiwe mshangao wakirudishwa

Mzee Yusuph Makamba: Nampongeza Rais Samia kwa mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, asema isiwe mshangao wakirudishwa

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam Shalom!!

Mzee wetu ameibuka na Kutoa Pongezi kedekede Kwa Mh Rais Samia Suluhu Hassan Kwa uamuzi mzuri aliofanya kuwabadili baadhi ya mawaziri, mtoto wake akiwemo.

Amemfananisha Rais na Coach jinsi anavyobadili kikosi, Nia ni ushindi.

Ameenda mbali na kuwapongeza waliotumbuliwa akidai pia wanastahili Pongezi Kwa kuwa wamemsaidia Rais Kwa muda waliokuwa mamlakani.

Itoshe kusema kuwa, Mzee huyu naye ni MMOJA wa wazee muhimu waliobaki, tuwatumie.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Source: Mahojiano, Wasafi media.

Karibuni 🙏

======

Yusuf-Makamba.jpeg

Mwandishi: Mzee Makamba bwana, tumeona mabadiliko ya Baraza la mawaziri!

Makamba: Wewe unashangaa nini?

Mwandishi: Sishangai mzee Makamba, naangalia picha yako unavyoangalia na mheshimiwa Rais anavyoboresha

Makamba: Sawa labda nikwambie mambo mafupi tu! Halooo

Mwandishi: Nakusikia Mzee Makamba

Mzee Yusuph Makamba: Hivi kocha wa Simba akimtoa mchezaji unamlaumu? Mambo mawili yanayoweza kumfanya amtoe mchezaji, mwingine anaweza akawa hana makosa lakini amechoka, pumzi zimeisha lakini pumzi zikirudi anamrudisha tena maana hawa ambao leo wametolewa, walikuwemo wakatoka na wamerudi tena.

Kwahiyo usije ukashangaa tena mwingine akarudi baadae, jambo la kawaida tu. Nasema Rais ni kocha, kazi ya kocha ni kuhakikisha kwamba magoli yanafungwa.

Kwahiyo anatazama, je katika kipindi hiki nani mchezaji bora kuliko mwingine anamchukua na hawa anawapumzisha.

Kwahiyo tunampongeza Rais kwa uteuzi alioufanya, tunawapongeza walioteuliwa na tunawapongeza na hata hawa wameondolewa, wanapaswa kushukuru maana si walikuwemo?
 
Huyu mzee alikuwa na mganga wake alikuwa kiboko sana angekuwepo hai, mwanawe asingetumbuliwa. Huyo sangoma jina lake Mohamed Mbega enzi za uhai wake wakati wa Jk alikuwa anaingia Ikulu muda wowote, alikuwa mtu muhimu sana kwenye utawala wa JK na ndiye alifanya Makamba na JK wawe na uswahiba mkubwa.
 
Tenguzi Kwa makamba ni faida kwake.maana ameondika na bilioni mia sita kwenye wizara yake ya mambo ya nje.maana alijua muda wowote atatoka na kuanza kuchota pesa mapema kabisa .
 
Salaam Shalom!!

Mzee wetu ameibuka na Kutoa Pongezi kedekede Kwa Mh Rais Samia Suluhu Hassan Kwa uamuzi mzuri aliofanya kuwabadili baadhi ya mawaziri, mtoto wake akiwemo.

Amemfananisha Rais na Coach jinsi anavyobadili kikosi, Nia ni ushindi.

Ameenda mbali na kuwapongeza waliotumbuliwa akidai pia wanastahili Pongezi Kwa kuwa wamemsaidia Rais Kwa muda waliokuwa mamlakani.

Itoshe kusema kuwa, Mzee huyu naye ni MMOJA wa wazee muhimu waliobaki, tuwatumie.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Source: Mahojiano, Wasafi media.

Karibuni 🙏

======

Mwandishi: Mzee Makamba bwana, tumeona mabadiliko ya Baraza la mawaziri!

Makamba: Wewe unashangaa nini?

Mwandishi: Sishangai mzee Makamba, naangalia picha yako unavyoangalia na mheshimiwa Rais anavyoboresha

Makamba: Sawa labda nikwambie mambo mafupi tu! Halooo

Mwandishi: Nakusikia Mzee Makamba

Mzee Yusuph Makamba: Hivi kocha wa Simba akimtoa mchezaji unamlaumu? Mambo mawili yanoyoweza kumfanya amtoe mchezaji. Mwingine anaweza akawa hana makosa lakini amechoka, pumzi zimeisha lakini pumzi zikirudi anamrudisha tena maana hawa amabao leo wametolewa, walikuwemo wakatoka na wamerudi tena.

Kwahiyo usije ukashangaa tena mwingine akarudi baadae, jambo la kawaida tu. Nasema Rais ni kocha, kazi ya kocha ni kuhakikisha kwamba magoli yanafungwa.

Kwahiyo anatazama, je katika kipindi hiki nani mchezaji bora kuliko mwingine anamchukua na hawa anawapumzisha.

Kwahiyo tunampongeza Rais kwa uteuzi alioufanya, tunawapongeza walioteuliwa na tunawapongeza na hata hawa wameondolewa, wanapaswa kushukuru maana si walikuwemo?
Haya majitu ya ccm yakikwambia usiku mwema usiyaamini toka utakuta jua linawaka.

Majitu ya ccm yakikwambia nenda kulia wewe usiende nenda kushoto wote utawakuta huko.

Hakuna jitu linafiki kama huyu mzee, wakati wanamkata Samwel Sitta kugombea uspika wa bunge yeye ndio alikuwa katibu mkuu, alipohojiwa na DW likasema eti ni zamu ya wanawake, sasa kwa nini walitowa fomu kwa wanaume?
 
Haya majitu ya ccm yakikwambia usiku mwema usiyaamini toka utakuta jua linawaka.

Majitu ya ccm yakikwambia nenda kulia wewe usiende nenda kushoto wote utawakuta huko.

Hakuna jitu linafiki kama huyu mzee, wakati wanamkata Samwel Sitta kugombea uspika wa bunge yeye ndio alikuwa katibu mkuu, alipohojiwa na DW likasema eti ni zamu ya wanawake, sasa kwa nini walitowa fomu kwa wanaume?
Ametuhakikishia waliotumbuliwa watarudi🤔

Huyu ni Mzee wa BUSARA kama Juma Msanii alivyoimba.
 
Back
Top Bottom