Mzozo wa CHADEMA na TBC: Nitasema mimi kiazi, wewe muhogo una mzizi'!

Mzozo wa CHADEMA na TBC: Nitasema mimi kiazi, wewe muhogo una mzizi'!

Matusi ni ndo Sera ya ilani ya uchaguzi kwenye chama chenu, halafu mnataka waandishi wa habari wenye werediii maalumu kama TBC wawarushe hewaniii.
Ilipobumaa bwana yenu mkubwa kama kawaida yenu kaamua kuporomosha matusi na kuwafukuza waandishiii wetu.

Endeleakutukana maaana ndo ilani yenu ya uchaguzi kwa miaka 5.

Miminiko apa ubungo, njooo mamaaa
Weredi ndiyo nini??
 
Kauli ni sahihi maana wakiingia kule mjengoni ni kususa na kupinga kila kitu sasa tutapitishaje hoja zao waliopiga kura?. Safari hii wana saccos wa Ufipa, mtakula wa chuya.

Usiwe mtu wa kukubali kila jambo hata kama lina maslahi kwako binafsi achilia mbali jamii,
Uwe makini kijana kupinga jambo siyo kwa nia ovu bali kutaka kujua kwa undani maudhui ya jambo lile.
 
Waandishi wahabari wanautamaduni wao wakutoa taarifa inayoenda mojakwa moja kwenye jamiiiii. Hivyo sikila tamko au mijadala inayozungunzwa huwa inapelekwa mojakwa moja . hivyo lazima ichujwe kwanzaaa.

Hivyo kinachowagarimu nyie hadi jamaa yenu mkuuu akakasirika vile nikwa sababu mlitaka kila mnalopayuka liende moja kwamoja kwenye uma wawatu.

TBC ni waandishi wahabari mahili wanaozingatia miiko na taratibu za taaluma yao.
Walipayuka wakasemaje?
 
Mtaongea maneno mengi kwa kuyapanga mkidhani mnaelewa sana na kumbe ni bure tu

Kiufupi upinzani hasa hii chadema ni kundi la wahuni tu. Wapiga dili na sasa kiwango chao wanatamani kupiga dili kupitia Ikulu na mamlaka.

MUNGU hajawahi kua mjinga mpaka akawateua,uongozi wowote MUNGU huujua na ni yeye ndiyo hufanya uwepo wake

Watakwama vibaya sana..ninyi wengine ni vibaraka msiyo jua, dalili za wazi za mgombea zinaonyesha anataka mali na maisha yake yaende,amefanya makubaliano na white people kuja kufirisi nchi aliyo zaliwa,huyu ni muhaini.

Watu wa kiwango chako, kwenye mijadala kama hii unasoma na kujifunza kimya kimya. Kufugnua mdomo ni kuanika utupu hadharani. Huoni haibu?
 
Waandishi wa habari wana utamaduni wao wa kutoa taarifa inayoenda moja kwa moja kwenye jamii. Hivyo si kila tamko au mijadala inayozungumzwa huwa inapelekwa moja kwa moja . hivyo lazima ichujwe kwanzaaa.

Hivyo kinachowagarimu nyie hadi jamaa yenu mkuu akakasirika vile ni kwa sababu mlitaka kila mnalopayuka liende moja kwa moja kwenye umma wa watu.

TBC ni waandishi wa habari mahiri wanaozingatia miiko na taratibu za taaluma yao.
Ona haya japo kidgo zezeta wa ccm ww.
 
Watu wa Mungu wameacha kazi ya Mungu wamejikita kwenye siasa!
Fuasi jinga sijui umesoma ujumbe au unaendekeza uzombie wako....kwa upinzani wanafanya siasa ila ccm halali kwakua chama cha kidini....pumbafu sn wew
 
MZOZO WA CHADEMA NA TBC: 'NITASEMA MIMI KIAZI, WEWE MUHOGO UNA MZIZI'!

Wiki iliyopita nilihudhuria Uzinduzi wa Kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Tundu Lissu katika Viwanja vya Zakhiem, Mbagala jijini Dar es Salaam. Kama kawaida yangu, nilitoa nasaha au hotuba fupi kabla ya kuufungua Mkutano ule kwa Sala. Baada ya hapo viongozi kadhaa wa CHADEMA walihutubia akiwemo Mwenyekiti wake Mheshimiwa Freeman Mbowe.

Kulikuwepo na vyombo kadhaa vya Habari likiwemo Shirika la Utangazaji la Tanzania, TBC. Yapo matendo yaliyoonyeshwa au kufanywa na TBC yaliyopelekea Mheshimiwa Mbowe kuwafukuza mkutanoni siku ile. Kama Askofu nilishtuka na kushangaa kwa kuwa tukio lile halikuwa la kawaida ingawa kwa tulio wengi lilikuwa na tafsiri yake katika 'ulimwengu wa roho'. Mwitikio (reactions) kutoka kwa Mbowe ulikuwa wa ghafla (instant) ambao hata hivyo ulionekana kujengwa katika misingi ya kihistoria ya mahusiano kati ya CHADEMA au Viongozi wake na TBC.

Askofu ni mtetezi wa haki na haki haina upendeleo! Lakini katika tukio lile, Askofu alijikuta akikutana na mwitikio (reactions) kutoka kwa watu wanaodhani kuwa hawakutendewa haki na TBC. Kwa kuwa Askofu alikuwa ameukabidhi Mkutano ule mikononi mwa Mungu na kusafisha anga lote la Mbagala, akiendelea kuwa mtulivu kwa kuwa aliamini kuwa mbingu zilikuwa kazini.

TBC ni taasisi ya Umma inayoendeshwa kwa kodi za wananchi wa Tanzania wakiwemo wafuasi wa CHADEMA na vyama vyote vya Upinzani. Huko nyuma niliwahi kuisema TBC hadharani kupitia ukurasa wangu kuwataka waache upendeleo. Ni dhahiri kuwa baadhi ya matokeo ya hisia za upendeleo ni yale tuliyoyaona kule Mbagala wakati TBC ilipofukuzwa Mkutanoni. Watangazaji, Wapiga Picha, na Waandishi wa Habari wa TBC ni watoto wa nchi hii. Wao hawahusiki sana kwa kuwa wako chini ya watu wanaotoa maelekezo. Kama kuna shida ye yote kuhusiana na utendaji wa TBC wasilaumiwe hao, bali walaumiwe waliokabidhiwa kuongoza TBC akiwemo Mkurugenzi wake Mkuu na Mwenyekiti wa Bodi.

Mara kadhaa TBC imerusha hewani maudhui ya viongozi wa serikali inayotokana na CCM pasipo kukatisha matangazo hayo hata kama baadhi ya viongozi hao wametoa kauli ambazo kwa muono wetu kauli zile zinadharirisha watu wengine! TBC na Vyombo vingine vya Habari kwa pamoja vimevumilia maudhui kama hayo kurushwa mubashara pasipo kukatizwa. Hivi karibuni nimewasema Star TV kwa kuruhusu maudhui yaliyokuwa yanamfedhehesha Mgombea Urais wa CHADEMA, Mheshimiwa Tundu Lissu kupitia kipindi cha 'Agenda 2020' kinachoongozwa na Aloyce Nyanda 'Mtozi'! Star TV haikukatiza matangazo yale ingawa huko nyuma iliwahi kukatiza matangazo ghafla wakati mmoja wa viongozi wa CHADEMA akitoa hoja.

Vitendo vya kuchagua maudhui ya kurusha kwa upande wa Upinzani na kutokuchagua maudhui ya kurusha kwa upande wa CCM na Serikali yake ndivyo vinavyopelekea baadhi ya Vyombo vya Habari ikiwemo TBC walaumike na kuhisiwa kuwa wana upendeleo. Haijawa mara moja baadhi ya Vyombo vya Habari kusitisha matangazo kwa muda endapo yanayoongelewa na Wapinzani yanaonekana kuwa tishio kwa CCM na Serikali yake. Lakini vyombo vya Habari havitakiwi kufika huko. Vyama vya Siasa vyote vinavyoshiriki Uchaguzi Mkuu ni vyama halali na chama chochote kati ya hivyo kinaweza kushika dola. Hakuna Chama cha Kigaidi katika hivyo, la sivyo visingelisajiliwa na kuruhusiwa kushiriki Uchaguzi Mkuu.

Vyombo vya Habari na hasa TBC watende haki na watimize wajibu wao pasipo upendeleo hasa ikizingatiwa kuwa wao wanaendeshwa kwa kodi za Watanzania wote.

Tunatoa wito kwa TBC na CHADEMA kuketi na kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza. Tunahimiza uvumilivu kwa pande zote mbili wakati wa kushughulikia jambo hilo. Taasisi zote mbili yaani TBC na CHADEMA wajizuie kuendelea kutoa kauli endelezi hadharani kuhusiana na suala hilo zaidi ya kutafuta suluhu.

Wazaramo wana msemo usemao: "Sema wewe kiazi, nikisema mie muhogo nina mzizi'! Na mimi kama Askofu nimeamua kusema yale ambayo wengine wanaogopa kuyasema!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
Vitendo vya kuchagua maudhui ya kurusha kwa upande wa Upinzani na kutokuchagua maudhui ya kurusha kwa upande wa CCM na Serikali yake ndivyo vinavyopelekea baadhi ya Vyombo vya Habari ikiwemo TBC kuhisiwa kuwa wana upendeleo. Swali fikirishi, je CCM na Serikali yake ndiyo wenye akili sana kuliko watanzania wote 'marakadhaa tumeshudia viongozi tuliowapa dhamana wakijitoa ufahamu hadi tunashanga'
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
MZOZO WA CHADEMA NA TBC: 'NITASEMA MIMI KIAZI, WEWE MUHOGO UNA MZIZI'!

Wiki iliyopita nilihudhuria Uzinduzi wa Kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Tundu Lissu katika Viwanja vya Zakhiem, Mbagala jijini Dar es Salaam. Kama kawaida yangu, nilitoa nasaha au hotuba fupi kabla ya kuufungua Mkutano ule kwa Sala. Baada ya hapo viongozi kadhaa wa CHADEMA walihutubia akiwemo Mwenyekiti wake Mheshimiwa Freeman Mbowe.

Kulikuwepo na vyombo kadhaa vya Habari likiwemo Shirika la Utangazaji la Tanzania, TBC. Yapo matendo yaliyoonyeshwa au kufanywa na TBC yaliyopelekea Mheshimiwa Mbowe kuwafukuza mkutanoni siku ile. Kama Askofu nilishtuka na kushangaa kwa kuwa tukio lile halikuwa la kawaida ingawa kwa tulio wengi lilikuwa na tafsiri yake katika 'ulimwengu wa roho'. Mwitikio (reactions) kutoka kwa Mbowe ulikuwa wa ghafla (instant) ambao hata hivyo ulionekana kujengwa katika misingi ya kihistoria ya mahusiano kati ya CHADEMA au Viongozi wake na TBC.

Askofu ni mtetezi wa haki na haki haina upendeleo! Lakini katika tukio lile, Askofu alijikuta akikutana na mwitikio (reactions) kutoka kwa watu wanaodhani kuwa hawakutendewa haki na TBC. Kwa kuwa Askofu alikuwa ameukabidhi Mkutano ule mikononi mwa Mungu na kusafisha anga lote la Mbagala, akiendelea kuwa mtulivu kwa kuwa aliamini kuwa mbingu zilikuwa kazini.

TBC ni taasisi ya Umma inayoendeshwa kwa kodi za wananchi wa Tanzania wakiwemo wafuasi wa CHADEMA na vyama vyote vya Upinzani. Huko nyuma niliwahi kuisema TBC hadharani kupitia ukurasa wangu kuwataka waache upendeleo. Ni dhahiri kuwa baadhi ya matokeo ya hisia za upendeleo ni yale tuliyoyaona kule Mbagala wakati TBC ilipofukuzwa Mkutanoni. Watangazaji, Wapiga Picha, na Waandishi wa Habari wa TBC ni watoto wa nchi hii. Wao hawahusiki sana kwa kuwa wako chini ya watu wanaotoa maelekezo. Kama kuna shida ye yote kuhusiana na utendaji wa TBC wasilaumiwe hao, bali walaumiwe waliokabidhiwa kuongoza TBC akiwemo Mkurugenzi wake Mkuu na Mwenyekiti wa Bodi.

Mara kadhaa TBC imerusha hewani maudhui ya viongozi wa serikali inayotokana na CCM pasipo kukatisha matangazo hayo hata kama baadhi ya viongozi hao wametoa kauli ambazo kwa muono wetu kauli zile zinadharirisha watu wengine! TBC na Vyombo vingine vya Habari kwa pamoja vimevumilia maudhui kama hayo kurushwa mubashara pasipo kukatizwa. Hivi karibuni nimewasema Star TV kwa kuruhusu maudhui yaliyokuwa yanamfedhehesha Mgombea Urais wa CHADEMA, Mheshimiwa Tundu Lissu kupitia kipindi cha 'Agenda 2020' kinachoongozwa na Aloyce Nyanda 'Mtozi'! Star TV haikukatiza matangazo yale ingawa huko nyuma iliwahi kukatiza matangazo ghafla wakati mmoja wa viongozi wa CHADEMA akitoa hoja.

Vitendo vya kuchagua maudhui ya kurusha kwa upande wa Upinzani na kutokuchagua maudhui ya kurusha kwa upande wa CCM na Serikali yake ndivyo vinavyopelekea baadhi ya Vyombo vya Habari ikiwemo TBC walaumike na kuhisiwa kuwa wana upendeleo. Haijawa mara moja baadhi ya Vyombo vya Habari kusitisha matangazo kwa muda endapo yanayoongelewa na Wapinzani yanaonekana kuwa tishio kwa CCM na Serikali yake. Lakini vyombo vya Habari havitakiwi kufika huko. Vyama vya Siasa vyote vinavyoshiriki Uchaguzi Mkuu ni vyama halali na chama chochote kati ya hivyo kinaweza kushika dola. Hakuna Chama cha Kigaidi katika hivyo, la sivyo visingelisajiliwa na kuruhusiwa kushiriki Uchaguzi Mkuu.

Vyombo vya Habari na hasa TBC watende haki na watimize wajibu wao pasipo upendeleo hasa ikizingatiwa kuwa wao wanaendeshwa kwa kodi za Watanzania wote.

Tunatoa wito kwa TBC na CHADEMA kuketi na kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza. Tunahimiza uvumilivu kwa pande zote mbili wakati wa kushughulikia jambo hilo. Taasisi zote mbili yaani TBC na CHADEMA wajizuie kuendelea kutoa kauli endelezi hadharani kuhusiana na suala hilo zaidi ya kutafuta suluhu.

Wazaramo wana msemo usemao: "Sema wewe kiazi, nikisema mie muhogo nina mzizi'! Na mimi kama Askofu nimeamua kusema yale ambayo wengine wanaogopa kuyasema!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
Tiibiisii ni sikio la kufa ambalo lilishakufa zamani
 
Watu wa Mungu wameacha kazi ya Mungu wamejikita kwenye siasa!
Siasa ni maisha unayoishi binaadamu yeyoye siasa inaweza amua ukaishi kama digi digi siasa inaweza amua ukaishi kama upo peponi unataiacha siasa siku utakapo ingia kaburini mtu unaposema wewe sio mwanasiasa wakati siasa hizo hizo ndio zinakuendeshea mfumo wako wa maisha kila siku huwa nakushangaa sana nikuweke kwenye kundi gani kilazaaa au mbulula
 
Kinachofanyika TBC ni mfano wa yale yanayofanywa na vyombo vingi sana vya serikali, wala sio siri wala kufichana. Kama huamini leo hii chukua wimbo wako hata wa dini, peleka TBC uwaombe waurushe hewani kwa mfano kwenye vipoindi vya dini, hautapokelewa....unless uwe unasifia
 
Back
Top Bottom