Ilboru ni moja ya shule zenye utulivu! kwan ulisoma mwaka gani? Vurugu na migomo ndo vimetawala sikuhiz
Ushauri wngu mpeleke Mzumbe maana kule atajenga kitu kichwani kutokana spirit iliyojengeka pale shuleni. Kwa sisi watoto wa mjini tuliosomaga Azania tulikuwa tunasoma kwa spirit iliyojengeka zamani Azania vichwa kwnye hesabu.
Angalizo ukimpeleka huko private muandalie hela ya kumsomeshea as private Chuo kikuu maana sisi wengne tulichukuliwa na shule moja private baada ya kufanya vizuri o -level cha moto tulikiona chuo kwnye mikopo,ukiangalia familia uliyotoka ya kuungaunga ilikuwa balaa tupu.
Shule za serikali hata kama ni special ili mwanafunzi afaulu lazima awe mpiganaji la sivyo atafeli.Nakumbuka nikiwa form 2 Tanga tech mwalimu wa chemistry aliingia darasani mara 2 tu mwaka mzima lakini matokeo yalipotoka A zilikua 82 na B za kutosha halafu wanafunzi 7 walipata 100, headmaster alimpa huyo mwalimu zawadi ambayo kwa kweli hakustahili kabisa .Mi nakushauri mpe ukweli kuhusu mazingira yalivyo kama atakubali kwamba anaweza kupigana basi mpeleke mzumbe