Tetesi: Mzungu/Muitaliano wa January Makamba kuongea na waandishi wa Habari kesho Saa Nane, Hyatt Hotel

Status
Not open for further replies.

Lakini...ukishaanza kuli play kwenye social media mwishowe litakosa mwelekeo wa maana na kuishia kuonekana ni majungu hususan ukizingatia wahusika na historia zao.
 
Huyu mzungu mwenyewe tumemzuia kuondoka hapa hotel sababu ya madeni tunayomdai ashachanganyikiwa tayari huyu ni wa kupuuzwa tu.
 

MWL NYERERE ALITUJUZA KETENDO CHA WAZIRI AU KIONGOZI WA UMMA KUSHUTUMIWA TU, ANAKAA PEMBENI KWA UCHUNGUZI. HAPASWI KUSHUTUMIWA, JANUARI KAA PEMBENI TAFADHALI.
 
Ushaipigania chama wewe?..... Hapo ulipo yawezekana una hali mbaya sana kiuchumi ETI tunapigania chama....

Endelea kupigania chama, sisi twala kivulini
Ushaipigania chama wewe?..... Hapo ulipo yawezekana una hali mbaya sana kiuchumi ETI tunapigania chama....

Endelea kupigania chama, sisi twala kivulini
wewe kula kivulini lakini muda mfupi ujao utakula juani.. Kutumika katika aina yako ni kujidharau mwenyewe. Unajisikiaje kuandika uongo ambao haukufaidishi na Chochote?
 
Nyani Ngabu mkuu salama? Naona new names tu humu.

Vijana sakeni hela acheni kutoka mapovu. Kama kala rushwa au hajala kuna vyombo vyakufanyia kazi hilo suala. Sisi wengine tunawalipa hivyo vyombo kupitia kodi zetu.
 
Pesa itoke wapi wakati huu ni uzushi jameni eboooo
mkuu tusilibeze sana jambo hili, wazee husema dume mkubwa hupigwa na dume mdogo kimzaha...hii inamaanisha kuwa ck zote dume mkubwa amezoea kumtisha mdogo naye hukimbia lkn mwisho ataamua kujiandaa kumkabili dume mkubwa, hivyo mkubwa atakapo thubutu kumrushia pembe dume mdogo kama alivyozoea, ndipo mdogo atakomaa naye hadi amwangushe mkubwa...naona tuweke akiba ya maneno tuone mwisho wa jambo hili
 
Hapa kidogo kuna utata. Hivi mtoa rushwa na mpoke rushwa wote si wanamakosa wa sheria ni kwamba ni kifungo? Au kuna kitu na miss hapa?
 
Nchi hii inautitiri wa kodi, na rais wetu mpendwa alilizungumzia sana kipindi cha kampeni. na ndio mifumo hii mibovu inayochangia wazawa kuwa masikini na kushindwa kufanya innovation au kufungua viwanda vidogovidogo vyenye kuzalisha bidhaa nafuu na kutoa ajira.. kuendelea na mifumo hii ni kuruhusu umasikini usio na kikomo kwa walala hoi wengi ambao ndio wanashabikia ccm na kuliwa kodi na kuchekelea.

mfano tazama hii

Ada ya ukaguzi wa vifaa vya zimamoto inaumuhimu gani hapo? je TRA wanagawa fire extinguisher?Je trafik anaekagua halipwi mshahara na hiyo pesa humlipa ruzuki ya kukagua trafik? ILi mradi tu ni visheria vinavyo waongezea mzigo wa kodi wananchi na hivi vilitungwa na ccm ktk mfumo ccm. Tunaomba rais wetu mpendwa JPM atimize wajibu kwa kutusaidia wananchi kupunguziwa kodi ili wazawa wajipambanue ktk kutumia raslimali tulizonazo kujikwamua kiuchumi na kuzipiku nchi zinazotuzunguka...lkn tukiendelea hivi tutabakia kushangilia majipu na hapa kaz# mwisho umaskini na hali ilele na mambo yaleyale.

Pia nimuombe rais wetu asimame imara kukemea ukandamizaji wa demokrasia unaofanywa na ccm ktk chaguzi za umeya na kule zanzbar. ni matumaini yangu rais wetu mpendwa wa JMT ataliona hili na kulifanyia kazi na mwisho automatic atasifika kuwa rais wa karne bila kujisifia mwenyewe.

Bima nayo unalipia laki moja (ya chini) lakini imeongezewa na kodi inakuwa 118000.. najiuliza sana badala ya bima kulipa kodi. kodi hiyo imewekwa kwa mkata bima huu ni wizi wa mchana. tunaomba kodi zipunguue sio kutudanganya na usanii wa majipu
@@@@ni wajibu wa trafik kukagua gari sababu analipwa mshahara kutokana na kodi zetu****
 
Nini kinaendelea hapo Hyatt Hotel wakuu?maana saa nne imepita kitambo
 
Akimaliza maongezi yake, ajiandae safari ya Segerea, maana alikuwa anatoa rushwa na analalamika tu kwa kuwa kakosa deal!
Amesahau kutoa na kupokea rushwa yote ni makosa!
 
Nyani Ngabu mkuu salama? Naona new names tu humu.

Vijana sakeni hela acheni kutoka mapovu. Kama kala rushwa au hajala kuna vyombo vyakufanyia kazi hilo suala. Sisi wengine tunawalipa hivyo vyombo kupitia kodi zetu.

Mazee Fikiraduni....natania tu bana....

Kuna uzi wa kumbukumbu ya miaka 10 ya JF humu.

Hebu nenda nawe ukatie neno basi....
 
Yaani akajikaange right in front of the media?? The ITALIAN NATIONAL???Haiingii akilini. Kama ataongea kweli, expect a lot of REFUTATION.

Wala sio lazima aseme kwamba alitoa rushwa, anaweza kusema kwamba alitoa $1M kwa Makamba kama malipo ya udalali wa kupigania tenda. In this case mzungu hajatoa rushwa na Makamba atakuwa matatizoni kwa kuwa dalali wa tenda ambayo mzungu analalamika kutopata.

Ila tu niseme kwamba sio kweli kwamba mtoa rushwa na mpokeaji wote wana makosa. Mtoa rushwa anapotoa rushwa na kusema tunamwadhibu kwa kosa gani? Rushwa ni bei ya haki inayotozwa na mtu mwenye mamlaka au dhamana. Kwa maana hiyo kuna mnunuzi na muuzaji. Mnunuzi ananunua kwasababu anahitaji haki ambayo anashindwa kuipata katika muda na njia husika kwasababu muuzaji amefanya muda na njia husika kutopitika na mnunuzi. Hivyo basi kumwadhibu mtoaji rushwa sio sahihi na kufanya hivyo kunaendeleza rushwa! Nikitoa rushwa kumbe sitakiwi kusema maana nikisema kumbe sina utofauti na yule aliyepokea: if that is the case nitatoa na kutunza siri. Lazima tubadiri hii sheria au desturi inayosema kutoa rushwa ni kosa na badala yake tuseme mtoa rushwa ambaye atagundulika alitoa bila kutoa taarifa ataadhibiwa. Hii itamfanya mpokeaji kukataa maana hana uhakika kama mtoaji atakaa kimya!
 
Hahaha sawa mkuu ,unajua najaribu kum link huyu muitaliano na kina Michael Corleone wa Godfather ,unataka kuniambia hajui kabisa ni kosa kutoa rushwa ?? Na kama anajua ni kosa ni kipi kinampa kiburi cha kuja public?? Labda kuna mengi anayoyajua ndio maana akaamua hivyo ,anaweza akawa kabisa labda ni secret service wa Italy na pengine alikua anatumika na ubalozi wa Italy na tayari wana contingency plan
Kwa serikali zetu zilivyo mtu wa namna hiyo angekua ameshakamatwa na kutoroshwa na baadae tunaambiwa mtuhumiwa ametoroka kesi hamna
Hushagai kwanini huyo Muitaliano yuko hapo Hyatt comfortable kabisa pamoja na kwamba inasemekana ameshindwa kulipia hotel room service na kazuiwa na hotel ,ngoja tumsikie atasema nini hiyo kesho

Na hasa ukizingatia awamu iliyopita serikali ilikua inaendeshwa na genge la wafanyabiashara ,yote yanawezekana
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…