Smart codetz
JF-Expert Member
- Jan 25, 2023
- 218
- 875
Aliyekuwa kocha wa Yanga SC Nasreddine Nabi ameeleza maamuzi yake ya kutoendelea kuwa na timu hiyo aliyawasilisha mara baada ya mechi dhidi ya TP Mazembe, na tangu hapo hajawahi kukaa mezani na timu hiyo kujadiliana kuhusu mkataba mpya kwani tayari alishawasilisha maamuzi yake Na kwa kipindi hicho alichowasilisha maamuzi hayo,hakuwa na ofa kutoka timu yoyote.
Nabi kupitia ukurasa wake wa Instagram amefafanua kuwa ripoti za mwanae wa kiume ni wakala wake na alikuja Tanzania kwa ajili ya mazungumzo ya mkataba ni uongo na za kijinga, kwa sababu mwanae bado ni mwanafunzi pia mwanae ni shabiki wa timu,Alikuja Tanzania kuisapoti timu na baba yake
Ameandika Nabi kupitia Insta Story.
Kocha huyo amemaliza kwa kuwaomba watu wasimuhusishe mwanae kwani hahusiki kabisa kwenye maamuzi ya kazi yake.