mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,309
- 4,798
Watanzania wametakiwa kuepuka mashinikizo yoyote yanayoweza kuhatarisha usalama wa nchi, yakiwemo maandamano, hasa wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Rai hiyo imetolewa na Nabii wa Kanisa la Heavenly Image Manifest (HIM), Nabii Edmund Mystic, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuhusu mkesha mkubwa wa kuliombea Taifa, Rais Samia Suluhu Hassan, na uchaguzi mkuu ujao.
Mkesha huo unatarajiwa kufanyika Februari 28, mwaka huu, katika Ukumbi wa Ubungo Plaza, ukihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa.
"Tumeona mwaka jana jinsi hali ilivyokuwa nchini Kenya baada ya machafuko kutokea. Watumishi wa Mungu walihubiri kuhusu hatari hizo, lakini wengi hawakuzingatia. Sisi kama Watanzania, tunapaswa kutambua kuwa usalama wa Taifa letu ni jukumu la kila mmoja wetu. Ni muhimu kuepuka shinikizo lolote linaloweza kuleta machafuko na sisi viongozi wa dini tunapaswa kusimama imara kuliombea Taifa," alisisitiza Nabii Edmund.
Rai hiyo imetolewa na Nabii wa Kanisa la Heavenly Image Manifest (HIM), Nabii Edmund Mystic, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuhusu mkesha mkubwa wa kuliombea Taifa, Rais Samia Suluhu Hassan, na uchaguzi mkuu ujao.
Mkesha huo unatarajiwa kufanyika Februari 28, mwaka huu, katika Ukumbi wa Ubungo Plaza, ukihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa.
"Tumeona mwaka jana jinsi hali ilivyokuwa nchini Kenya baada ya machafuko kutokea. Watumishi wa Mungu walihubiri kuhusu hatari hizo, lakini wengi hawakuzingatia. Sisi kama Watanzania, tunapaswa kutambua kuwa usalama wa Taifa letu ni jukumu la kila mmoja wetu. Ni muhimu kuepuka shinikizo lolote linaloweza kuleta machafuko na sisi viongozi wa dini tunapaswa kusimama imara kuliombea Taifa," alisisitiza Nabii Edmund.