Nadharia Tete: Bila Ujumbe NEC, Urais Haiwezekani

Nadharia Tete: Bila Ujumbe NEC, Urais Haiwezekani

Nd. Mchambuzi,

Unasema, " Mwaka huu ni muhimu sana kwangu kuhusu maamuzi magumu." Kwanza sisi vijana wa nchi hii ili tuendelee inabidi tuachane na "siasa za maji taka" kama utumiaji wa maneno vague na meaningless kama mfano "maamuzi magumu" , "Kujivua gamba" etc. Hii misemo inatugharimu sana kama Taifa. Tujiulize ni nguvu kazi kiasi gani imepotea kwa wananchi kudiscuss maana ya hii misemo?

Wewe kama young professional tunayekutegemea kwanza inabidi utuambie unategemea mabadiliko gani pindi ikifikia Dec2012? Kama mategemeo yako yasipotimizwa (yote au baadhi), utaamua kuachana/kujiondoa kwenye CCM? Maana sijaona mahali ulipoweka wazi kuwa a,b,c ... zisipotimia basi ni time ya kuondoka CCM. Otherwise kama unaendelea kuongea kwa kutumia lugha za viongozi wako nawe utakuwa huna tofauti nao. Yaani unakuwa unaitumia JF kama platform ya kujijenga ndani ya CCM as "a Young turk" wakukumbuke kwani unajua bigwigs wa CCM wanategemea JF for reliable political news. Mwanakijiji amekusaidia kuweka wazi kabisa jinsi gani hizo changes zilivyo shallow na sijaona CCM diehards hata mmoja aliyejitokeza kuja kumpinga kuwa hajui political reality ya TZ kwa kuwa yupo Nje. Naona tunajadili jinsi gani ya kuzuia inevitable yaani pending kifo cha CCM similar to KANU. Unasubiria kuachana nacho pale tu daktari atakapo declare kuwa kimekufa, huoni kuwa CCM imeshapoteza dira, moral authority? Binafsi thinking hiyo ya kusubiria naifananisha na watu wanaoitwa "Political Opportunists" ambao daima ni hatari sana kwani leadership skills zao kikomo chao huwa kipo chini, mfano hai ni Dr, Baba Mwanaasha, Vasco D-G, Msanii na mengineyo....hayo majina yote yametokana na mapungufu makubwa aliyonayo kiongozi wenu.
Ni hayo tu ndugu yangu, siasa njema.
Angalizo: Sijakushauri ujiunge na chama chochote kwani natambua unaouwezo wa kupima vilivyopo kama vinafaa au la, na pia unaweza kuanzisha cha kwako.

Gogomoka,

Asante sana kwa mchango wako mzuri. Naelewa msingi wa hoja yako. Lakini naomba nitoe ufafanuzi kidogo. Uamuzi mgumu mimi nadhani ni neno zuri tu, ili mradi unalitumia inavyotakiwa. Kwangu mimi, uamuzi mgumu ni 'opportunity cost', kwamba ukichagua kitu kimoja, basi uwe tayari kuachana na kingine by 100%. Katika mazingira ya hoja yako, huo mchakato sio mrahisi kwangu kwa maelezo yafuatayo:

Kama umekuwa unanifuatilia huko nyuma, mimi tatizo langu na vyama vilivyopo ni itikadi. Najaribu sana kuepuka kujiunga na chama fulani kwa sababu ya umaarufu wa muda mfupi kama vile ilivyotokea kwa NCCR miaka ya tisini, ambapo umaarufu wake ulitokana na personalities/majina makubwa - lamwai, kaborour, mrema, bagenda, marando... pamoja na kelele za ufisadi ambao ulikithiri chini ya serikali ya mwinyi. Haikuchukua muda umaarufu kwa NCCR ukafa kwa sababu kilijipanga zaidi kuingia ikulu, lakini mbaya zaidi kwa kutegemea vitu ambavyo vinakipa uhai chama kwa mufa mfupi tu, badala ya itikadi iliyo sheheni Alternative to IMF Development Agenda. Hakuna chama chenye maelezo yake kwenye katiba kuhusu foreign policy in the context of development zaidi ya kusema kitashirikiana na vyama vingine afrika, duniani....

Mambo yale yale ya NCCR 1990s yameanza kujitokeza tena katika siasa za sasa - umaarufu wa personalities na kelele dhidi ya ufisadi, huku wakiwekeza almost nothing kwenye itikadi ya maana. Itikadi zinazofuatwa na CCM, Chadema, CUF hivi sasa ni ya uliberali i.e. 'IMF development alternative' ambayo haitamwokoa mtanzania wa kijijini. Uliberali ndio sababu ya watanzania kuwa maskini, ndio uliozaa azimio la ovyo la zanzibar, ndio unaolea ufisadi, ambapo ubepari umepotezewa meaning na ufisadi. CCM na serikali yake wapo busy kusafisha mafisadi badala ya kusafisha ubepari uliochafuliwa na mafisadi.

Ni muhimu kwa vyama vya upinzani kupingana na ufisadi ulipo lakini ni muhimu wakatambua kwamba 'power corrupts', hivyo chama chochote kitachoingia madarakani baada ya CCM, lazima kiwe na mkakati wa muda mrefu juu ya hilo, vinginevyo hakitachukua miaka zaidi ya mitano kwenye madaraka. Na sioni chama chochote chenye mkakati wa muda mrefu juu ya hilo kwani IMF alternative to development imeachwa intact.

Navutiwa sana na CCK.
 
Mkuu, mchambuzi analysis yako nzuri na post zako kuhusu chama chako ziko deep na only active members ndio wataelewa. Hatuoni members wa vyama vingine wakifanya haya au kunena haya, wengi ni kama wanaburutwa tu, mbele wamezibwa, nyuma wamesahau kushoto na kulia kuna ushabiki

when it come to dream party for kids, CCM inaongoza...I mean kama mtoto anaona kuwa rais leo hii ni rahisi kusema na kufanya hivyo kupitia CCM na sio chama kingine chochote.

though I stand with my signature, lets me give u thump up to stand like this!

Waberoya,

Nashukuru sana kwa mawazo yako ya kutia moyo. Nakubaliana na wewe kimsingi. Ukipata muda, naomba usome pia jibu langu kwa gogomoka 'post number 42', halafu tutajadili zaidi.
 
Napendekeza nadharia tete (Hypotheses) zifuatazo, lengo kuu ikiwa ni kutupa sote nafasi ya kuzipima nadharia hizi tete, kwa kutumia uzoefu wetu na uelewa wetu juu ya utamaduni wa CCM, hasa kwa kuzingatia matukio na mazingira ya nyakati hizi. Matokeo ya zoezi hili la kupima nadharia tete hizi yatatoa majibu ya aina mbili: Aidha majibu - KWELI, hivyo kufanya nadharia hizi tete kusimama, au majibu - SIO KWELI, hivyo kuziangusha hizi nadharia tete. Nadharia tete zipo nne kama ifuatavyo:

I. Ingawa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM halazimiki atoke miongoni mwa wajumbe wa NEC na pia suala hili halipo kikatiba, Chama Cha Mapinduzi hakina utamaduni wa kuteua wagombea wake wa Urais ambao sio miongoni mwa wajumbe wa NEC.

II. Ili mwana CCM awe na nafasi nzuri ya kuteuliwa kubeba bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, inamlazimu mwanachama huyu, agombee na ashinde uchaguzi wa wajumbe wa NEC kwenye uchaguzi wa ndani wa CCM mwaka huu wa 2012. Kwa kufanya hivyo, mwana CCM huyo atakuwa ni mjumbe wa NEC-CCM ifikapo mwaka wa uchaguzi mkuu, 2015, hivyo kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuteuliwa kubeba bendera ya CCM mwaka 2015.

III. Wanachama wa CCM wenye malengo ya kugombea Urais kupitia CCM mwaka 2015, ambao kwa sasa wanashikilia nafasi mbili kwa pamoja – yani ubunge na ujumbe wa NEC, chini ya mabadiliko ya katiba ya CCM ya hivi karibuni, itawalazimu aidha waachie nafasi zao za ubunge na kubakia wajumbe wa NEC, au waendelee na Ubunge na waachane na ujumbe wa NEC, huku wakisubiri Baraka za Mwenyekiti wa CCM Taifa za kuwateua kuwa wajumbe wa NEC, kupitia zile nafasi kumi, miezi michache kabla ya mchakato wa kutafuta mgombea Urais kupitia CCM, ili mwanachama huyo awe katika nafasi nzuri zaidi ya kushinda katika kinyang’anyiro hicho May, 2015.

IV. Kwa maana hii, Mchezo wote wa kinyang’anyiro cha Urais kupitia CCM mwaka 2015, umebadilika kutokana na mabadiliko ya katiba ya CCM, hivyo tutarajie majina mapya kutawala mbio hizi baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa CCM Novemba mwaka huu wa 2012, majina ambayo wengi hatukuyatarajia.

Nimezipenda hizi nadharia,lakini kama Chama Cha Mapinduzi hakina utamaduni wa kuteua wagombea wake wa Urais ambao sio miongoni mwa wajumbe wa NEC huoni kama kuna chama kipya tena kikubwa kina kuja,na kama sio chama je huoni kwamba hao wajumbe wa nec kwa sasa ambao watakuwa badae sio wajumbe kuto kuikubali hali hio,ni wazo tu
 
Uchambuzi wako ni kama umetumwa na Lowassa au ni mfuasi wake. Hii ndio kambi yenye hofu kupita kiasi lakini bila sababu za msingi.

Lowassa haninunulii mimi chai. Jamani, hawa viongozi baada ya miaka kumi, kumi na tano watakuwa hoi kama wastaafu. Mimi huwa sielewi kabisa kwa vijana wenye akili zao timamu kuwekeza kwa viongozi ambao sio future ya CCM kwa maana ya kwamba, watastaafu ndani ya miaka 15, huku vijana hao ikiwa ndio kwanza siasa zitakuwa zimeanza kuchanganya kwani hawatakuwa na zaidi ya umri wa miaka 50. Vijana hawa wanaotafuta kununuliwa chai na wanasiasa wa sasa badala ya kuwa na misimamo huru, wakija kuwafuata wanasiasa hawa miaka 10-15 baadae, watachoambiwa na wanasiasa hawa ni kwamba "mimi mstaafu bwana". Ni muhimu kwa vijana kuwa makini na kuepuka kuchagua the wrong side of history. Na ni muhimu waanze kuelewa kwamba 'history is not the past, history is the present'.

Mimi ni mwana CCM mwenye mawazo huru, vinginevyo kama ningekuwa nina mawazo tegemezi, ningeonekana nikizurura nao. Naomba ieleweke hivyo.
 
Nimezipenda hizi nadharia,lakini kama Chama Cha Mapinduzi hakina utamaduni wa kuteua wagombea wake wa Urais ambao sio miongoni mwa wajumbe wa NEC huoni kama kuna chama kipya tena kikubwa kina kuja,na kama sio chama je huoni kwamba hao wajumbe wa nec kwa sasa ambao watakuwa badae sio wajumbe kuto kuikubali hali hio,ni wazo tu

kwa uelewa wangu finyu, mabadiliko yoyote ya katiba ya CCM lazima yapitishwe na mkutano mkuu wa taifa. Sijaliona hilo likizungumziwa na kina Nape, sana sana wanazungumza kwamba mapendekezo yatapelekwa NEC. NEC kazi yake sio kufanya mabadiliko ya katiba bali kuandaa katiba. Kwa wale wanaoelewa tofauti hizi pengine wangetusaidia kutuondoa katika mchanganyo huu, kwani kama mkutano mkuu wa CCM taifa ndio wenye jukumu hilo, ina maana mkutano huu utakutana kabla ya uchaguzi wa chama November au agenda hii ya mabadiliko itafanyiwa kazi na mkutano mkuu kule Dodoma kabla ya mkutano huu kujikita katika kuchagua wajumbe wa NEC?

Kuhusu ujio wa Chama kingine kipya, sitashangaa hata vikija vingine mia moja kwani, tofauti na maoni ya wengi kwamba vyama vilivyopo vinatosha, viungane ili vipate nguvu, nguvu gani iliyokubwa zaidi ya nguvu ya soko inayomkandamiza mwanakijiji kila kukicha? Bado kuna gap kubwa ya ki-itikadi katika siasa za Tanzania, chama cha kweli kitakuwa kile ambacho kitaondokana na IMF alternative to development, suala ambalo CCM ndio inatekeleza hiyo alternative, huku Chadema wakijaribu kwenda ikulu kwenda kutekeleza kitu hiko hiko kwa kasi na nguvu zaidi. Ndio maana to donors, WorldBank, IMF, kwa hawa wakubwa, CCM, Chadema, NCCR, wote ni sawa tu, tofauti tunaona sisi tusioelewa nini kinaendelea.
 
Hapa JK anajisafishia njia kuhakikisha kuwa anaendelea kuwa mwenyekiti wa CCM mpaka 2015 na anajihakikishia kuwa na nguvu ya kumpitisha mgombea wake anayemtaka.
 
Comparative advantage ya CCM (over other ruling parties like ZANU-PF or former KANU, not over CDM or CUF) ni kuwa support base yake ni wanyonge (kielimu), na kuwa watu bado wafirikiri CCM 2010 au ile ya 2015 ni sawa na ile ya mwaka 1977, ndio maana bado wanendelea kuipigia kura. Wangekuwa na elimu ya kujua ukweli wa CCM ya sasa inavyofanya wawe na maisha magumu, wasingeipigia kura. CCM ya sasa ni chama tofauti kabisa na CCM ya mwaka 1977, na kamwe haitarudi kuwa CCM ile ya wakulima na wafanyakazi, no matter what is being done.

BongoLander,
Kimsingi, tupo pamoja kihoja. Lakini ningependa kuongezea kwamba:

CCM kumeguka katika vipande viwili ni kitu logical kabisa. Hivi tunavyozungumza, tayari CCM imemeguka ndani kwa ndani, LAKINI SIO KI-ITIKADI BALI KWA MTAZAMO WA: NYIE WACHAFU, SISI WASAFI. Swali linalofuata ni Je: iwapo CCM itakuja vunjika katika vipande viwili, ushindani baina yao utaendelea kuwa nini, USAFI na UCHAFU? Na haya pia ni makosa wanayofanya Chadema hivi sasa katika ushindani wao na CCM. Kwa kweli, ingawa watu wengi sana humu huwa wanajenga hoja kwamba itikadi sio muhimu katika vyama bali katiba mpya n.k, hakuna kitu muhimu kama itikadi katika Maendeleo na mafaniko ya Chama. Mwanakijiji leo katika gazeti la Tanzania Daima amelizungumzia vizuri sana suala hili. Vinginevyo, CCM ikibahatika kupata viongozi wa kulielewa suala hili kwa ufasaha, Chama kitameguka muda sio mrefu na mmeguko huo utakuwa na tija kubwa sana kwa taifa.

Leo hii, kisera, CCM inatekeleza IMF alternative to development – ubinaifisishaji, sokoo huria, sera za uwekezaji zenye lengo la kuvutia wawekezaji waje Tanzania badala ya mfano Kenya kwa kusamehe kodi, n.k. Haya yote yanahusiana na itikadi ya kiliberali, ambayo CUF na Chadema nao wanaifuata kwa intensity tofauti, huku mmoja akisema yupo mlango wa kati, mwingine akisema mlango wake una komeo, n.k. Kwahiyo, while CCM inatekeleza IMF alternative to development, ni dhahiri kwamba Chadema wakiingia Ikulu, watatekeleza sera zile zile za kiliberali za CCM, ila kwa ari, kasi, na nguvu zaidi, hasa ikizingatiwa kwamba muasisi wa Chadema Mzee wetu Edwin Mtei ni chanda na pete na IMF, tangia miaka ile alipotofautiana na Mwalimu na kuhamia Washington kama mwajiriwa wa IMF ambako alikuwa anajipanga kurudi nyumbani kuleta mageuzi ya kisiasa na kiuchumi, hasa hili la IMF Alternative to Development.

Madhara yake ni kwamba, chini ya CCM na Azimio lake la Zanzibar, na pia kwa mtazamo wa kiliberali wa Chadema, umaskini Tanzania utaendelea kuwa tatizo kubwa, kwani itikadi ya kiliberali ndio imezaa ufisadi, capital flight, n.k, kwani haya yote yanadekezwa na itikadi ya kiliberali ambayo tunaicha iwe juu ya sheria. Na pakitokea tatizo, CCM inasafisha mafisadi badala ya kusafisha Ubepari ambao umechafuliwa na Ufisadi. Ubepari ni jambo zuri kwa Maendeleo lakini sio ubepari holela.

Umezungumzia wananchi walio vijijini kwamba hawana uelewa mkubwa. Ni kweli lakini sio kama tunavyofikiri, kwani wengi vijijini wanaelewa kwamba ahadi za TANU hazijafanikiwa kwa sababu ya matatizo ya uongozi. Hilo wengi wanalijua. Lakini tatizo linakuja pale wanapokosa mbadala wa kweli kwa sababu wakiangalia siasa kwa mfano za Chadema, ni siasa za kupinga ufisadi na zenye kukipa chama umaarufu kutokana na majina makubwa – Slaa, Mnyika, Zitto, Lissu, kama ilivyokuwa kwa NCCR mwaka 1995 Mrema, kaborou, Bagenda, Masumbuko Lamwai, Mabere Marando), chama ambacho ambacho kumbe kilikuwa kinajikita zaidi kupata madaraka tu, sio kuendeleza mapambano dhidi ya umaskini, vinginevyo, kwanini kilipotea? Wanakijiji hawa wakiangalia CCM, nako kuna siasa za kupinga mafisadi kupitia kina Nape, Sitta, Kilango n.k, na pia CCM, kama ilivyokuwa Chadema, nayo ina majina mengi makubwa na yenye mvuto ambayo hayajachafuka. Chadema inahitaji kujenga imani kwa watanzania wanavutiwa na chama hiki kwamba hakita yarudia yale ya NCCR ya 1995. Bado hawajaonyesha mwelekeo huu.

Ni kutokana na mapungufu kama haya ndio maana unakuta kwenye jimbo la uchaguzi, wananachi hawamkubali mgombea Urais wa CCM, lakini wanamkubali mbunge wa CCM au hawamkubali mgombea ubunge CCM lakini wanamkubali mgombea Urais. Madhara mengine ni kwamba, kutokana na kukosekana kwa tofauti ya itikadi in the eyes ya wapiga kura, kuna wananchi ambao wanaona bora waendelee na shetani wanaemjua (CCM), kuliko kumjaribu mwingine (mfano Chadema) ambae wakati wa kampeni huko majukwaani, ilani yake ya uchaguzi na sera zake hazina tofauti aidha na zile ambazo CCM ilizijaribu miaka ya zamani na zikashindikana, au nyingi zinafana na zile ndani ya CCM nyakati hizi.

Chadema wanaungwa mkono na watanzania wengi hivi sasa, sio kwasababu wananchi wanaona kwamba Chadema ni mbadala bora wa Maendeleo, bali wanataka kufikisha ujumbe kwa CCM kwamba wamechoshwa na hali ngumu ya maisha ambayo inaa ambatana na mafanikio kwa wachache ndani ya CCM na serikali yake. Vinginevyo wananchi wengi wanatambua fika kwamba hata Chadema ikishinda uchaguzi, wapo viongozi ambao watatumia nafasi zao kujinufaisha wao na familia zao kama ilivyo chini ya CCM kwa sasa, na hii ni kwa sababu moja tu kuu kwamba- "POWER CORRUPTS"
 
1. Ingawa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM halazimiki atoke miongoni mwa wajumbe wa NEC na pia suala hili halipo kikatiba, Chama Cha Mapinduzi hakina utamaduni wa kuteua wagombea wake wa Urais ambao sio miongoni mwa wajumbe wa NEC.

...................CCM ilitoka kwenye mfumo wa chama kushika hatamu, wagombea wake kutoka NEC si jambo la ajabu. Katika hali ya kawaida mgombea wenye sifa na vigezo bora kuwa nje ya NEC kisiasa ni jambo ambalo sio rahisi sana. Mwanachama bora hawezi kuachwa na chama nje ya mfumo wa NEC ingawa kwa nadra inaweza kutokea.

II. Ili mwana CCM awe na nafasi nzuri ya kuteuliwa kubeba bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, inamlazimu mwanachama huyu, agombee na ashinde uchaguzi wa wajumbe wa NEC kwenye uchaguzi wa ndani wa CCM mwaka huu wa 2012. Kwa kufanya hivyo, mwana CCM huyo atakuwa ni mjumbe wa NEC-CCM ifikapo mwaka wa uchaguzi mkuu, 2015, hivyo kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuteuliwa kubeba bendera ya CCM mwaka 2015.

.........................Nadharia yako sio kweli, angalia hata chadema waliowahi kugombea wote hawakuwahi kuwa nje ya vikao vya juu vya chama. CCM wakati ukufika akaonekana mtu safi kabisa nje ya vikao vikuu vya chama nina hakika hawawezi kumtupa.

III. Wanachama wa CCM wenye malengo ya kugombea Urais kupitia CCM mwaka 2015, ambao kwa sasa wanashikilia nafasi mbili kwa pamoja – yani ubunge na ujumbe wa NEC, chini ya mabadiliko ya katiba ya CCM ya hivi karibuni, itawalazimu aidha waachie nafasi zao za ubunge na kubakia wajumbe wa NEC, au waendelee na Ubunge na waachane na ujumbe wa NEC, huku wakisubiri Baraka za Mwenyekiti wa CCM Taifa za kuwateua kuwa wajumbe wa NEC, kupitia zile nafasi kumi, miezi michache kabla ya mchakato wa kutafuta mgombea Urais kupitia CCM, ili mwanachama huyo awe katika nafasi nzuri zaidi ya kushinda katika kinyang'anyiro hicho.

.........................Nape amekanusha hili na hata Jk wabunge wataendelea kuwa wajumbe wa NEC wakati huo huo ni wabunge. Umepata wapi hii taarifa ya uongo?

IV. Kwa maana hii, Mchezo wote wa kinyang'anyiro cha Urais kupitia CCM mwaka 2015, umebadilika kutokana na mabadiliko ya katiba ya CCM, hivyo tutarajie majina mapya kutawala mbio hizi baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa CCM Novemba mwaka huu wa 2012, majina ambayo wengi hatukuyatarajia.

..................Rais aliyoko madarakani anamaliza kipindi chake hakuna ubishi majina mapya tutayaona wengi wakitaka kuchukua kiti cha Rais. Hii haitakuwa kwa CCM tu bali hata chadema na CUF vyama pinzani. Kimsingi, mabadiliko ya katiba ya CCM nimeona kwa ujumla wake ni mazuri. Kelele zinazopigwa ni hofu ya mabadiliko hayo. Binadamu hapendi mabadiliko kama yanagusa maslahi yake binafsi.

Iwapo unaelewa maana ya nadharia tete, utagundua kwamba umekwenda kinyume na malengo ya mjadala huu. Unaposema nimepata wapi taarifa hii na ile ya uongo, inaonyesha jinsi gani haukuwa makini kutumia muda zaidi kuelewa maana ya dhana ya nadharia tete. Na nilisema at the outset kwamba matokeo yake baada ya sote kuzipima nadharia hizi tete ni aidha matokeo kwamba ni KWELI au SIO KWELI, kutokana na hoja. Maneno unayotumia kama vile 'uongo' ni ishara kwamba uelewa wako juu ya nadharia tete ni kwamba zinatawaliwa na 'uzushi'. Hii sio kweli. Jitahidi kuelewa maana ya dhana hii, na uwe utanguliza hoja kuliko siasa katika mazingira ya nadharia tete. Vinginevyo nathamini mawazo yako, na naomba tuzidi kuelimishana kwa hoja. Kwa mfano, nini kinakufanya uamini kwamba CCM katika uchaguzi Mkuu wa 2015 itaweka mgombea asiyetokana na wana NEC? Na nini maana nzima ya kuhimiza umuhimu wa wagombea urais kuwa na uzoefu na chama, uzoefu wa namna gani?
 
Yetu macho, wengine tunasubiria Chama cha wahuni kife tushehereke
 
How long are we going to put up with the CCM politician parasites that run our country. They are draining our Natural resource, people are suffering while the fat cats line their pockets. They are all guilty make no mistake. Every one ,enriching him or herself with family, through corruption should be prosecuted point.The money they are stealing could be used to develop Tanzania and create jobs.Its a disgrace that they can even think of getting away with it. It has got nothing to do with party politics,its against the constitution and the law. Jail them all who are guilty and take there assets. Mchambuzi chama chako kimejaa wala rushwa na Watanzania wanazidi kukichukia kila siku hata mkibadilisha safu nzima ya uongozi lakini hakuna wa kuwawajibisha walioharibu hasa waliotuingiza kwenye mikataba ya kipumbavu na walioiba pesa za walipa kodi wanatakiwa kufungwa jela. Na sidhani kama kuna kiongozi yoyote kutoka CCM anawezakufanya hivyo zaidi ya Viongozi wa vyama vya upinzani ndio wataofanya hivyo.
 


III. Wanachama wa CCM wenye malengo ya kugombea Urais kupitia CCM mwaka 2015, ambao kwa sasa wanashikilia nafasi mbili kwa pamoja – yani ubunge na ujumbe wa NEC, chini ya mabadiliko ya katiba ya CCM ya hivi karibuni, itawalazimu aidha waachie nafasi zao za ubunge na kubakia wajumbe wa NEC, au waendelee na Ubunge na waachane na ujumbe wa NEC, huku wakisubiri Baraka za Mwenyekiti wa CCM Taifa za kuwateua kuwa wajumbe wa NEC, kupitia zile nafasi kumi, miezi michache kabla ya mchakato wa kutafuta mgombea Urais kupitia CCM, ili mwanachama huyo awe katika nafasi nzuri zaidi ya kushinda katika kinyang'anyiro hicho.

.........................Nape amekanusha hili na hata Jk wabunge wataendelea kuwa wajumbe wa NEC wakati huo huo ni wabunge. Umepata wapi hii taarifa ya uongo?

Kama Nape anasema hayo basi na yeye anajichanganya tu kwani kwa upande mwingine anasema kwamba kuanzia sasa, ujumbe wa NEC itakuwa ni kazi ya kudumu, huku ikijulikana wazi kwa mujibu wa katiba kwamba ubunge pia ni kazi ya muda wote. Kwa mujibu wa kanuni mpya za uchaguzi:

"Mwanachama ambaye anaomba nafasi za uongozi ambayo ni kazi ya muda wote, hataruhusiwa kushika nafasi ya aina hiyo zaidi ya moja katika chama isipokuwa kamati kuu imeamua vinginevyo."

Viongozi wa CCM wasiwe waoga, waseme tu wazi kwamba ubunge ni nafasi ya kudumu kama ilivyokuwa ujumbe wa NEC chini ya utaratibu mpya, hivyo wahusika wachague kusuka au kunyoa. Vinginevyo CCM isiwapotezee watanzania muda kwa kuwachanganya na maamuzi yake yenyewe huku viongozi hao hao wakikwepa kuwa wa kweli kuhusu athari za maamuzi ya vikao vyao, kwani tafsiri juu ya maamuzi haya, hata kwa mwanafunzi wa darasa la saba anayefuatilia siasa za CCM kwa ukaribu, ni wazi kwamba, kwa mujibu wa mabadiliko haya, kuanzia sasa vyeo vya ubunge na ujumbe wa NEC kuanzia sasa vimetengwa, vinginevyo Mwenyekiti wa CCM taifa aamue kwa kushauriana na wenzake katika chama kumteua mbunge kuwa pia mjumbe wa NEC, kukidhi malengo watakayokusudia kwa wakati huo.
 
c. Mabadiliko haya hayaweki uhuru wa wagombea kuwa na ilani zao ambazo zitashindanishwa mbele ya wanachama ili aliye na ilani bora na anayekubalika ndiye anaweza kushinda. Na badala yake bado Ilani ya chama itachorwa kwa ujumla wake na wagombea watatakiwa kuitekeleza.

Kuna point kubwa hapo.
 
Mchambuzi kwa mara nyingine tena you got it right.

Kwa hakika wewe ni shahidi kwamba ktk CCM nadharia yoyote inaweza kuanguka na kuwa sio kweli. Hili unalijua maana upo ndani.
Hebu niambie kwa nadharia zote nne ulizotaja hapo juu na kwa CCM ya sasa ipi inaweza kumkwaza the mighty and all powerful EL??

Lakini kilichofanyika Dodoma kina maana yoyote basi nadharia namba 4 ingesimama.

Ni dhahiri lengo sio wajumbe wa NEC kuwa karibu na wananchi, CCM inamtandao hadi chumba kwa chumba. Ni kipi kipya wajumbe wa NEC watafanya katibu, mwenyekiti, kamati ya siasa wilaya hawafanyi???
Kuna lengo wanataka kutimiza na sio kisingizio cha kuwa karibu na wananchi kwani kama hili lingekuwa kweli basi aliyetakiwa kupunguziwa madaraka ni mwenyekiti cum Rais.

Kama siasa sio shughuli yako ya kila siku, nakushauri kaa huko huko (CCM) ila mapambano ya ukombozi yaendelee kutoka kila kona.
 
BongoLander,
Kimsingi, tupo pamoja kihoja. Lakini ningependa kuongezea kwamba:

CCM kumeguka katika vipande viwili ni kitu logical kabisa. Hivi tunavyozungumza, tayari CCM imemeguka ndani kwa ndani, LAKINI SIO KI-ITIKADI BALI KWA MTAZAMO WA: NYIE WACHAFU, SISI WASAFI. Swali linalofuata ni Je: iwapo CCM itakuja vunjika katika vipande viwili, ushindani baina yao utaendelea kuwa nini, USAFI na UCHAFU? Na haya pia ni makosa wanayofanya Chadema hivi sasa katika ushindani wao na CCM. Kwa kweli, ingawa watu wengi sana humu huwa wanajenga hoja kwamba itikadi sio muhimu katika vyama bali katiba mpya n.k, hakuna kitu muhimu kama itikadi katika Maendeleo na mafaniko ya Chama. Mwanakijiji leo katika gazeti la Tanzania Daima amelizungumzia vizuri sana suala hili. Vinginevyo, CCM ikibahatika kupata viongozi wa kulielewa suala hili kwa ufasaha, Chama kitameguka muda sio mrefu na mmeguko huo utakuwa na tija kubwa sana kwa taifa.

Leo hii, kisera, CCM inatekeleza IMF alternative to development – ubinaifisishaji, sokoo huria, sera za uwekezaji zenye lengo la kuvutia wawekezaji waje Tanzania badala ya mfano Kenya kwa kusamehe kodi, n.k. Haya yote yanahusiana na itikadi ya kiliberali, ambayo CUF na Chadema nao wanaifuata kwa intensity tofauti, huku mmoja akisema yupo mlango wa kati, mwingine akisema mlango wake una komeo, n.k. Kwahiyo, while CCM inatekeleza IMF alternative to development, ni dhahiri kwamba Chadema wakiingia Ikulu, watatekeleza sera zile zile za kiliberali za CCM, ila kwa ari, kasi, na nguvu zaidi, hasa ikizingatiwa kwamba muasisi wa Chadema Mzee wetu Edwin Mtei ni chanda na pete na IMF, tangia miaka ile alipotofautiana na Mwalimu na kuhamia Washington kama mwajiriwa wa IMF ambako alikuwa anajipanga kurudi nyumbani kuleta mageuzi ya kisiasa na kiuchumi, hasa hili la IMF Alternative to Development.

Madhara yake ni kwamba, chini ya CCM na Azimio lake la Zanzibar, na pia kwa mtazamo wa kiliberali wa Chadema, umaskini Tanzania utaendelea kuwa tatizo kubwa, kwani itikadi ya kiliberali ndio imezaa ufisadi, capital flight, n.k, kwani haya yote yanadekezwa na itikadi ya kiliberali ambayo tunaicha iwe juu ya sheria. Na pakitokea tatizo, CCM inasafisha mafisadi badala ya kusafisha Ubepari ambao umechafuliwa na Ufisadi. Ubepari ni jambo zuri kwa Maendeleo lakini sio ubepari holela.

Umezungumzia wananchi walio vijijini kwamba hawana uelewa mkubwa. Ni kweli lakini sio kama tunavyofikiri, kwani wengi vijijini wanaelewa kwamba ahadi za TANU hazijafanikiwa kwa sababu ya matatizo ya uongozi. Hilo wengi wanalijua. Lakini tatizo linakuja pale wanapokosa mbadala wa kweli kwa sababu wakiangalia siasa kwa mfano za Chadema, ni siasa za kupinga ufisadi na zenye kukipa chama umaarufu kutokana na majina makubwa – Slaa, Mnyika, Zitto, Lissu, kama ilivyokuwa kwa NCCR mwaka 1995 Mrema, kaborou, Bagenda, Masumbuko Lamwai, Mabere Marando), chama ambacho ambacho kumbe kilikuwa kinajikita zaidi kupata madaraka tu, sio kuendeleza mapambano dhidi ya umaskini, vinginevyo, kwanini kilipotea? Wanakijiji hawa wakiangalia CCM, nako kuna siasa za kupinga mafisadi kupitia kina Nape, Sitta, Kilango n.k, na pia CCM, kama ilivyokuwa Chadema, nayo ina majina mengi makubwa na yenye mvuto ambayo hayajachafuka. Chadema inahitaji kujenga imani kwa watanzania wanavutiwa na chama hiki kwamba hakita yarudia yale ya NCCR ya 1995. Bado hawajaonyesha mwelekeo huu.

Ni kutokana na mapungufu kama haya ndio maana unakuta kwenye jimbo la uchaguzi, wananachi hawamkubali mgombea Urais wa CCM, lakini wanamkubali mbunge wa CCM au hawamkubali mgombea ubunge CCM lakini wanamkubali mgombea Urais. Madhara mengine ni kwamba, kutokana na kukosekana kwa tofauti ya itikadi in the eyes ya wapiga kura, kuna wananchi ambao wanaona bora waendelee na shetani wanaemjua (CCM), kuliko kumjaribu mwingine (mfano Chadema) ambae wakati wa kampeni huko majukwaani, ilani yake ya uchaguzi na sera zake hazina tofauti aidha na zile ambazo CCM ilizijaribu miaka ya zamani na zikashindikana, au nyingi zinafana na zile ndani ya CCM nyakati hizi.

Chadema wanaungwa mkono na watanzania wengi hivi sasa, sio kwasababu wananchi wanaona kwamba Chadema ni mbadala bora wa Maendeleo, bali wanataka kufikisha ujumbe kwa CCM kwamba wamechoshwa na hali ngumu ya maisha ambayo inaa ambatana na mafanikio kwa wachache ndani ya CCM na serikali yake. Vinginevyo wananchi wengi wanatambua fika kwamba hata Chadema ikishinda uchaguzi, wapo viongozi ambao watatumia nafasi zao kujinufaisha wao na familia zao kama ilivyo chini ya CCM kwa sasa, na hii ni kwa sababu moja tu kuu kwamba- “POWER CORRUPTS”


Mchambuzi nakupata vizuri sana. Lakini tunakwenda mbali sana na kuwa too philosophical. Jaribu siku moja utembee kwa mguu kutoka kariakoo hadi buguruni au jaribu kutembea kutoka Posta hadi Aga Khan uwaulize watu itikadi ya CCM ni ipi na ya Chadema ni ipi. Huko pia kunaweza kuwa mbali sana,m au tafuta watu wenye kadi za CCM uwaulize itikadi ya CCM ni nini unawza kushangaa.

Kwa sasa ukweli ni kwamba ni vigumu sana kuwa na tofauti kubwa kati ya sera za vyama na itikadi zake, tunachochagua ni personalities. Nakupa mfano mdogo tu. Kuna mbunge anaitwa Sugu, angalia kama kweli watu wa mbeya mjini walimchagua kwa sera au nini. Au angalia CUF na CCM visiwani Zanzibar na uangalie vyama hivyo hivyo bara, uone ni kwanini wafanane Zanzibar na wasifanane bara.

Kuna hali fulani inayofanya watu wa mrengo wa kulia wasiwe na maana na wa mrengo wa kushoto wasiwe na maana, kuwa liberali kuna maana kiasi fulani. Lakini ningeoenda nitofautiane na wewe kidogo, ufisadi ni ufisadi tu, upo kwenye itikadi zote. Tulikuwa nao kwenye awamu ya kwanza, ukapaliliwa wamau ya pili, ukakusanya nguvu awamu ya tatu na sasa umestawi. Naamini pia hata Chadema wakiwa madarakani bado utakuwepo.

Kenya watu walikuwa wanasema kuwa bila KANU mambo hayatawezekana, walisema hakuna alternative others even believed that without Moi Kenya would not be Kenya, look at them now still going strong.

CCM ikipasuka ndio tutajua kuwa kuna mbadala, kuna watu wengi ndani ya CCM wako ndani kwa sababu ya necessity na wengine kwa sababu ya opporrtunity, na wengi wanaogopa kuwa real kwa kuwa wakiwa real wataambiwa tokeni kwenye chama. Kikipasuka utaona akili na u-free wa wanaobanwa ndani ya CCM kwa sasa.
 
Mchambuzi kwa mara nyingine tena you got it right.

Kwa hakika wewe ni shahidi kwamba ktk CCM nadharia yoyote inaweza kuanguka na kuwa sio kweli. Hili unalijua maana upo ndani.
Hebu niambie kwa nadharia zote nne ulizotaja hapo juu na kwa CCM ya sasa ipi inaweza kumkwaza the mighty and all powerful EL??

Lakini kilichofanyika Dodoma kina maana yoyote basi nadharia namba 4 ingesimama.

Ni dhahiri lengo sio wajumbe wa NEC kuwa karibu na wananchi, CCM inamtandao hadi chumba kwa chumba. Ni kipi kipya wajumbe wa NEC watafanya katibu, mwenyekiti, kamati ya siasa wilaya hawafanyi???
Kuna lengo wanataka kutimiza na sio kisingizio cha kuwa karibu na wananchi kwani kama hili lingekuwa kweli basi aliyetakiwa kupunguziwa madaraka ni mwenyekiti cum Rais.

Kama siasa sio shughuli yako ya kila siku, nakushauri kaa huko huko (CCM) ila mapambano ya ukombozi yaendelee kutoka kila kona.

Una hoja nzuri sana, kwani job description ya mjumbe wa NEC hadi hivi sasa haionyeshi jinsi gani mjumbe wa NEC ana shughulika moja kwa moja na wananchi/wanachama wa ngazi za huko chini. Bila ya uangalifu, mabadiliko haya yanaweza kuleta mvutano mkubwa sana huko wilayani - baina ya viongozi watatu ambao wote wana nafasi za muda wote - Katibu wa CCM wilaya, Mbunge na Mjumbe wa NEC, hasa nyakati za chaguzi za ndani ya chama na chaguzi za nchi.

Kuhusu nadharia ipi inaweza kumkwaza EL iwapo atakuwa na nia ya 2015, lakini pia kiongozi mwingine yoyote ambaye kwa sasa ni Mbunge, ni nadharia ya pili, na njia pekee ya kuwaokoa watu wa namna hii ni nadharia ya tatu, hasa iwapo mwenyekiti atateua mwanachama aliye mbunge kuwa mjumbe wa NEC miezi kadhaa kabla ya kuanza kwa mchakato wa kutafuta mgombea urais kupitia CCM, ili mtu huyo awe na sifa za uzoefu na uongozi ndani ya Chama, ambapo ni kawaida kwa mtu huyo kuchaguliwa kutoka miongoni mwa wajumbe wa NEC. Lakini bado hatujajua iwapo mchakato wa kumpata mgombea urais CCM utabadilishwa au utabaki kama ulivyo sasa. Kwa mtazamo wangu, utaratibu huu ni muhimu ubadilike iwapo CCM inajitakia mema. Iruhusu wanaogombea wajieleze kwa hoja, wauze sera zao, wazungushwe nchi nzima ili wajumbe wa mikutano ya CCM wilaya wapate nafasi ya kuwa scrutinize, na kura zipigwe huko huko wilayani - kwa mtindo wa primaries kama ilivyokuwa marekani.

Kuhusu siasa kama shughuli zangu - mimi sina nafasi yoyote ndani ya CCM zaidi ya kuwa mwanachama hai na wala sina mpango wa kugombea nafasi yoyote ndani ya chama katika uchaguzi wa chama mwaka huu wa 2012.
 
Mchambuzi nakupata vizuri sana. Lakini tunakwenda mbali sana na kuwa too philosophical. Jaribu siku moja utembee kwa mguu kutoka kariakoo hadi buguruni au jaribu kutembea kutoka Posta hadi Aga Khan uwaulize watu itikadi ya CCM ni ipi na ya Chadema ni ipi. Huko pia kunaweza kuwa mbali sana,m au tafuta watu wenye kadi za CCM uwaulize itikadi ya CCM ni nini unawza kushangaa.

Kwa sasa ukweli ni kwamba ni vigumu sana kuwa na tofauti kubwa kati ya sera za vyama na itikadi zake, tunachochagua ni personalities. Nakupa mfano mdogo tu. Kuna mbunge anaitwa Sugu, angalia kama kweli watu wa mbeya mjini walimchagua kwa sera au nini. Au angalia CUF na CCM visiwani Zanzibar na uangalie vyama hivyo hivyo bara, uone ni kwanini wafanane Zanzibar na wasifanane bara.

Kuna hali fulani inayofanya watu wa mrengo wa kulia wasiwe na maana na wa mrengo wa kushoto wasiwe na maana, kuwa liberali kuna maana kiasi fulani. Lakini ningeoenda nitofautiane na wewe kidogo, ufisadi ni ufisadi tu, upo kwenye itikadi zote. Tulikuwa nao kwenye awamu ya kwanza, ukapaliliwa wamau ya pili, ukakusanya nguvu awamu ya tatu na sasa umestawi. Naamini pia hata Chadema wakiwa madarakani bado utakuwepo.

Kenya watu walikuwa wanasema kuwa bila KANU mambo hayatawezekana, walisema hakuna alternative others even believed that without Moi Kenya would not be Kenya, look at them now still going strong.

CCM ikipasuka ndio tutajua kuwa kuna mbadala, kuna watu wengi ndani ya CCM wako ndani kwa sababu ya necessity na wengine kwa sababu ya opporrtunity, na wengi wanaogopa kuwa real kwa kuwa wakiwa real wataambiwa tokeni kwenye chama. Kikipasuka utaona akili na u-free wa wanaobanwa ndani ya CCM kwa sasa.

Nakubaliana na wewe kwamba wanachama wengi wa vyama vyote hawajui itikadi za vyao vyao ni nini. Lakini tutakuwa tunafanya makosa kwa kutumia hicho kama kigezo kwamba muda wa itikadi bado, hivyo tuangaikie mengine. Tatizo hili ni tatizo kubwa sana, na ndio maana siasa zetu ahzina ushindani wa maana. Ni muhimu vyama vikaanza ku address suala hili. Ukipata muda, jaribu kusoma makala ya mwanakijiji ya leo kwenye Tanzania Daima. Ameelezea vizuri sana suala la itikadi na umuhimu wake kwenye vyama vya siasa.

Kuhusu Sugu na Mbeya, hapo awali nilisema kwamba wananchi wengi hawachagui chadema kwa sababu wana amini kwamba sera za Chadema au itikadi yake ni superior kwa CCM. Wananchi wengi wanachagua Chadema kwa sababu/umaarufu wa muda mfupi, kitu ambacho hata wewe in a way umekielezea. Sugu kushindwa Mbeya 2015 sio kazi kwani wananchi wengi wa Mbeya mjini wana hasira na CCM na huwa wana express hasira zao katika chaguzi kuu. Hakuna lingine.

Pia kuhusu CCM kupasuka, nilihoji, je, kila upande utakuwa na nini cha kujitofautisha na upande mwingine, kwani hakuna anaye jali kuwekeza kwenye suala la itikadi. CCM ya namna hii, ikivunjika nini itakuwa msingi wa ushindani kati ya makundi hayo mawili: SISI WASAFI NA NYIE WACHAFU?
 
Napendekeza nadharia tete (Hypotheses) zifuatazo, lengo kuu ikiwa ni kutupa sote nafasi ya kuzipima nadharia hizi tete, kwa kutumia uzoefu wetu na uelewa wetu juu ya utamaduni wa CCM, hasa kwa kuzingatia matukio na mazingira ya nyakati hizi. Matokeo ya zoezi hili la kupima nadharia tete hizi yatatoa majibu ya aina mbili: Aidha majibu - KWELI, hivyo kufanya nadharia hizi tete kusimama, au majibu - SIO KWELI, hivyo kuziangusha hizi nadharia tete. Nadharia tete zipo nne kama ifuatavyo:

I. Ingawa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM halazimiki atoke miongoni mwa wajumbe wa NEC na pia suala hili halipo kikatiba, Chama Cha Mapinduzi hakina utamaduni wa kuteua wagombea wake wa Urais ambao sio miongoni mwa wajumbe wa NEC.

II. Ili mwana CCM awe na nafasi nzuri ya kuteuliwa kubeba bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, inamlazimu mwanachama huyu, agombee na ashinde uchaguzi wa wajumbe wa NEC kwenye uchaguzi wa ndani wa CCM mwaka huu wa 2012. Kwa kufanya hivyo, mwana CCM huyo atakuwa ni mjumbe wa NEC-CCM ifikapo mwaka wa uchaguzi mkuu, 2015, hivyo kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuteuliwa kubeba bendera ya CCM mwaka 2015.

III. Wanachama wa CCM wenye malengo ya kugombea Urais kupitia CCM mwaka 2015, ambao kwa sasa wanashikilia nafasi mbili kwa pamoja – yani ubunge na ujumbe wa NEC, chini ya mabadiliko ya katiba ya CCM ya hivi karibuni, itawalazimu aidha waachie nafasi zao za ubunge na kubakia wajumbe wa NEC, au waendelee na Ubunge na waachane na ujumbe wa NEC, huku wakisubiri Baraka za Mwenyekiti wa CCM Taifa za kuwateua kuwa wajumbe wa NEC, kupitia zile nafasi kumi, miezi michache kabla ya mchakato wa kutafuta mgombea Urais kupitia CCM, ili mwanachama huyo awe katika nafasi nzuri zaidi ya kushinda katika kinyang’anyiro hicho May, 2015.

IV. Kwa maana hii, Mchezo wote wa kinyang’anyiro cha Urais kupitia CCM mwaka 2015, umebadilika kutokana na mabadiliko ya katiba ya CCM, hivyo tutarajie majina mapya kutawala mbio hizi baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa CCM Novemba mwaka huu wa 2012, majina ambayo wengi hatukuyatarajia.


Nimesoma mabadiliko yaliyofanywa na NEC ya ccm hasa kuhusu wajumbe wa Nec kuchaguliwa toka wilayani na kwamba kazi yao itakuwa ni full time hivyo they cannot be wabunge as well hivyo kuwatoa katika nafasi ya kuweza kuchaguliwa kupeperusha bendera ya CCM kwenye kinyang'anyiro cha urais 2015!! Sina hakika kama katika mabadiliko haya zile nafasi za wabunge wa ccm kuwakilishwa kwenye NEC pia zimefutwa? Kama zile nafasi hazijafutwa basi huko ndiko kutakakokuwa kichochoro cha kuingilia Nec kwa wabunge wanaouwania urais 2015!!
 
Mchambuzi chama chako kimejaa wala rushwa na Watanzania wanazidi kukichukia kila siku hata mkibadilisha safu nzima ya uongozi lakini hakuna wa kuwawajibisha walioharibu hasa waliotuingiza kwenye mikataba ya kipumbavu na walioiba pesa za walipa kodi wanatakiwa kufungwa jela. Na sidhani kama kuna kiongozi yoyote kutoka CCM anawezakufanya hivyo zaidi ya Viongozi wa vyama vya upinzani ndio wataofanya hivyo.
Kimsingi upo sahihi lakini ufahamu tu kwamba suala la ufisadi/rushwa lipo katika vyama vyote, ni kwamba tu CCM imekuwa too extreme, sana sana kutokana na wao kuwa jikoni ambapo kuna mengi ya kula.

Tujiulize - kwanini CAG hapewi ushirikiano na vyama vya upinzani kwenda kukagua jinsi gani wanatumia ruzuku wanazopewa na serikali ambazo ni fedha za walipa kodi?

Kitendo cha CCK kutamka kwamba hakitaki ruzuku ya serikali kwani hiyo ni sehemu ya ufisadi, ni kitendo cha kizalendo sana, na ni mwanzo mzuri sana kwa chama hiki.

Vinginevyo hakuna chama cha upinzani chenye mkakati jinsi gani kitashughulikia ufisadi/rushwa, kama una details hizo, naomba unielimishe kidogo. Hata Nyerere alishindwa katika hili, tena chini ya mfumo wa chama kimoja. Ni muhimu ukafahamu kwamba 'power corrupts'.

Muhimu ni kujaribu to kuwa na mechanism za ku minimize tatizo hili, vinginevyo chama kikifanya ufisadi ndio agenda ya kuingia ikulu, chama hicho kikifanikiwa kukaa Ikulu kwa miaka zaidi ya mitano kitakuwa na bahati sana.
 
Kwani haya mabadiliko tayari yamekuwa rasmi kabla ya Katiba yenyewe kufanyiwa mabadiliko na Mkutano Mkuu?
 
Sina hakika kama katika mabadiliko haya zile nafasi za wabunge wa ccm kuwakilishwa kwenye NEC pia zimefutwa? Kama zile nafasi hazijafutwa basi huko ndiko kutakakokuwa kichochoro cha kuingilia Nec kwa wabunge wanaouwania urais 2015!!

Upo sahihi. Na tukumbuke kwamba wabunge walioingia NEC kupitia Bunge ni watu kama Sitta, Mwakyembe na wengine wachache. Hawa walichagua kugombea kupitia bunge tofauti na wenzao ambao walitumia njia nyingine kama zile za kugombea mikoani na pia vile vile kupitia kura za mkutano mkuu wa CCM taifa. Kwa mtazamo wangu, mtu kama Sitta ataendelea kuwa mbunge na Mjumbe wa NEC kwani sioni akipigiwa kura za hapana na wabunge iwapo atawania nafasi hiyo mwaka huu.
 
Back
Top Bottom