Naelekea Wizarani kumkabidhi Waziri bodaboda na vyeti ili asote navyo mwezi mzima

Walivyo wapigaji hao viongozi wenyewe, bodaboda yako watauza, vyeti wataghushi na kutumia majina yako na kesi watakubambikia ya kuwa muahini.

Roma katuliza akili hasa kwenye huu wimbo.
 
Suluhisho la yote haya ni uchaguzi ujao kama tu wananchi wataacha kisikiliza maneno ya uraghai na vijizawadi vya vitenge na vijisenti vya mkopo kwa akina mama

Inahitaji akili kubwa kufungua akili za watanzania. Viongozi wanayachukulia maisha simple tu ilihali wanawaumiza wananchi wa kipato cha chini

Subiri ifike 2024, utaona vijimaendeleo watakavyovifanya ili kuteka akili za wananchi. Hapo ndipo utawaona wabunge majimboni wakishika chepe ili kutindua mifereji, wengine watapanda vibajaji wakidai wanazungukia kero za wananchi wao

Hii nchi ni ngumu sana. Wakihashiba makande, hurejea bungeni kuishawishi serikali ipandishe kodi huku wakibeua na kujamba ovyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…