Nafanya mazoezi sana ila nazidi kuongeza uzito zaidi, nitakuwa nakosea wapi?

Nafanya mazoezi sana ila nazidi kuongeza uzito zaidi, nitakuwa nakosea wapi?

Chakula chakula chakula

Mazoezi yakuweka fit
Chakula kinajenga mwili.

Ushawahi kuona watoto wanakula zaidi ya watu wazima? Ni kwasababu wanajenga miili. Kila kitu kinakua, sasa wewe una miaka 35 na kuendelea, bado unakula kama kijana wa below (chini ya) 30 unategemea nini? Ni kwamba, mazoezi ndio yanaharakisha uchakataji wa misosi ulofakamia bila mpango.

Chakula chakula chakula.

Kwa vile tu una pesa, kila siku unaanza na supu na chapati, maziwa mayai, sukar kibao nk. Mchana nyama na mipilau jioni michemsho na ndizi. Je, mwili unahitaji yote hayo ukizingatia umeshaacha au umepungua kukua ulichobakisha ni kurudishia kinachopotea?

Chakula chakula chakula

Kuwa na nidhamu ya kula, fanya mazoezi kuweka fit viungo
Nimekuelewa vyema mkuu
 
Nyie wataalam ni waongo mlionishauri mazoezi ati nitapunguza kilo kumbe ni uongo tu, badala ya kupunguza naongeza KGS

Najituma sana mazoezini, namwaga jasho ili nikate weight ila naona KGS ziziongezeka kuliko kabla sijaanza

Bora hata nisingepiga tizi sioni faida yoyote ya mazoezi
Kufanya mazoezi kunaleta Appetite, na ukipata appetite usipokuwa makini utajikuta unakula sana na ndio kunenepa huko sasa
 
Kuna mazoezi extreme ambayo hayatajali mtu anakula nini ni yatampa anachotaka.

Unachoexperience ni kama weight loss trap. Ambapo mtu anayepungua au aliyepungua tayari anakua anagain weight zaidi ya mwanzo

Kwa beginner kama wewe ushauri wangu kwako ni huu "You get fit in the gym, you loose weight in the kitchen"
 
Nyie wataalam ni waongo mlionishauri mazoezi ati nitapunguza kilo kumbe ni uongo tu, badala ya kupunguza naongeza KGS

Najituma sana mazoezini, namwaga jasho ili nikate weight ila naona KGS ziziongezeka kuliko kabla sijaanza

Bora hata nisingepiga tizi sioni faida yoyote ya mazoezi
Kwa ninavyowajuwa Watanzania na kuto elewa vitu, usikute unafanya mazoezi kupunguza unene lakini bado baada ya mazoezi unakunywa beer, kula kitimoto, kula hovyo bila kuzingatia diet kama Shilole. Kwa hali hii huwezi punguza unene hata kidogo.
 
Kuna kufanya mazoezi ili kutafuta appetite na kufanya mazoezi kupunguza uzito. Je wewe unafanya yapi?
 
Back
Top Bottom