Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Uhuru kwa Wateule uliisha Enzi za nyerere, yeye alikuwa akiwadhibiti Wateule na ili kumuenzi ndio ukaona hadi sasa Wateule mfano Majaji na Mahakimu Achana na hao wa majukwaani wanasiasa, bali uhuru wamekosa, ajabu na cha kushangaza ni kuwa wakati watanganyika wanapambana na ukoloni na kuhitaji uhuru Tulikuwa wa moja sasa hawa wabaguzi ndio wanapelekea utwana kwa ndugu zetu (wateule)Nikiwa nafuatilia jinsi hawa wateule wanafanya kazi nahisi wako kama watumwa. Kuna mda naona kabisa sisi ambao tuko kitaa tuna furaha na amani kuliko wao.
Kuna haja ya wateuzi kuwaambia wawe huru kwenye kazi zao. Mfano Rais anakuja kuzindua mradi uliobuniwa na kujengwa na mtangulizi wake, wateule wake wanajitutumua na kumwambia tunashukuru kwà juhudi zako
Hii huwa hainiingii akilini.
Mfano Mwingine ni pale mteuliea anaamua kudanganya umma ili amfurahishe mteuzi wake. Mfano mteule anashindwa kuwaambia mteuzi kwamba Tanzania Kuna uhaba wa madarasa, Madawati, na kwamba Maji Dar hayatoshi. Mnaishia kumsifia sifia tu hadi sisi Wana nchi tunashangaa jinsi mteule alivyopoteza uhuru wake.
Poleni wateule. Ila kwà nini huwa munakuwa hivyo?
Hao waungwana wanajawa na chuki mpaka wanapoteza uwezo wa kawaida kabisa wa kufikiria.Serikali ndo inatekeleza, kwa hiyo anayesifiwa ni rais aliyepo madarakani kama mkuu wa serikali kwa wakati husika.