Nafikiria kukopa kisha kuweka dhamana vyeti vyangu!

Nafikiria kukopa kisha kuweka dhamana vyeti vyangu!

Mkuu ulivyojielezea nimekumbuka maisha yangu enzi za saidia fundi kule Iringa na Njombe daah hadi nimetamani nikupe tu hiyo hela ukipata utarudisha, ukikosa kurudisha basi utakuwa umesogeza gurudumu la maisha mbele na huenda ukaja kusaidia kizazi changu mbeleni au ukaja kuifanya dunia iwe mahali salama pa kuishi, tuwasiliane!
Mkuu nimekucheck pm ila naona kimya
 
Usichezee riba Mkuu, hela ya riba inaenda haraka kama uyoga, kwa biashara changa sikushauri uchukue mkopo wenye riba, Nenda kwa watu binafsi wakukopeshe bidhaa/pesa ukifanya huduma uzirudishe.

Unaweza kupata hiyo hela na riba ikawa asilimia arobaini, kumbuka biashara hiyo ni changa.
 
Usichezee riba Mkuu, hela ya riba inaenda haraka kama uyoga, kwa biashara changa sikushauri uchukue mkopo wenye riba, Nenda kwa watu binafsi wakukopeshe bidhaa/pesa ukifanya huduma uzirudishe.

Unaweza kupata hiyo hela na riba ikawa asilimia arobaini, kumbuka biashara hiyo ni changa.
Sawa mkuu
 
Endelea kupambana utafanikiwa kwa Sasa unahitaji kuinvest kwenye nguvu zako kupata huo mtajii usichague kazii na pigana mwenyewe uweze kupata hiyo pesaa biashara bro haitabiriki usiweke 100% kwenye biashara sometimes Mambo yanabadilika unaweza poteza hata mtaji wote
Ushaurii pambana upate chako mtaji wakoo utafanya biashara kwa amaniii [emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Habari wana JF,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu, mimi ni mhitimu wa chuo kikuu ngazi ya shahada (degree) kati ya chuo kimoja hapa nchini. Kuna mradi/biashara moja nataka kuanzisha ila nakwama kwenye mtaji (Ambao kwa makadirio sio chini ya Milioni Moja).

Nimewaza sana na kuwazua, suluhisho nilopata ni kukopa,tatizo linakuja kwenye kuweka dhamana. Sina cha maana chochote kinachofikia thamani ya huo mkopo naotaka kuchukua. Nimepata wazo la kuweka dhamana vyeti vyangu vya taaluma (o level,advance mpaka chuo) ili niweze kujikwamua na hili janga la ukosefu wa ajira na kuweza kujiajiri mwenyewe. Nina uhakika wa hii biashara kutiki asilimia 90 hivyo sibahatishi katika ilo.

Nina maswali kadhaa yana rindima kichwani mwangu, nayo kama yafuatavyo;

1. Ni nani mtu sahihi wa kunikopesha na kuvitunza vyeti vyangu mpaka pale nitapomaliza mkopo (bila kutapeliwa vyeti vyangu)?
2. Ni nani wa kumface na kunikubalia kunipa huo mkopo kwa dhamana ya vyeti vyangu?
3. Kuna taasisi au benki yenye kukopesha kwa dhamana ya vyeti vya mhusika?

NB: Nipo tayari kuandikishiana mbele ya mashahidi na mwanasheria. Pia nipo tayari kukopeshwa kwa riba hisiyozid 40%.

Nakaribisha ushauri na maoni yenu au msaada wa nini cha kufanya kutimiza lengo hili husika.

Bora wewe unataka kuviweka dhamana uchukue mkopo,mi natamani hata kuviuza maana hakuna kitu vimenisaidia
 
Ila mleta mada hiyo username yako inaweza kukufanya usiaminike humu ndani ukashindwa kukopesheka 😀
 
Sidhan kama ni rahis kuvitelekeza vyeti kwa mkopo wa Milioni moja. Nashukuru kwa mchango wako mkuu
😅😅😅😅😅😅😅😅 Umenichekesha sana mdogo wangu.
 
Hili tatizo lipo kwa Jamii yetu ya JamiiForums

Ndio maana nilileta hili wazo la kuwasaidia wahitaji kama wewe na wengine wenye pesa zao kuweza kupata faida..

Naomba suggestions za wadau kuchangia mada; hata usipo-vote tuone ni vipi tunaweza kufanya hili jambo

 
Hii hali ilinikuta mwaka 2017 nilipo acha chuo NIT , nika ja mtaani. Maisha ya mtaa bado kidogo yanichanganye akili. Nashukuru MUNGU , akanitoa kwenye stress hizi. Mi ushauri wangu nimpe bro , Asisahau kusali
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] Umenichekesha sana mdogo wangu.
Anadhan ni kazi rahis kuvitelekeza vyeti uyu[emoji28][emoji28]
 
Ila mleta mada hiyo username yako inaweza kukufanya usiaminike humu ndani ukashindwa kukopesheka [emoji3]
Kua na fujo haimaanishi sikopesheki, nina fujo zisizoumiza kama bongo zozo [emoji2]
 
Bora wewe unataka kuviweka dhamana uchukue mkopo,mi natamani hata kuviuza maana hakuna kitu vimenisaidia
Tuendelee kupambana mkuu ipo siku Mungu atatufungulia milango
 
Hii hali ilinikuta mwaka 2017 nilipo acha chuo NIT , nika ja mtaani. Maisha ya mtaa bado kidogo yanichanganye akili. Nashukuru MUNGU , akanitoa kwenye stress hizi. Mi ushauri wangu nimpe bro , Asisahau kusali
Shukran sana mkuu kwa kuntia moyo,huwa nazidi kumuomba sana Mungu
 
Anadhan ni kazi rahis kuvitelekeza vyeti uyu[emoji28][emoji28]
Nino vyeti, mimi wamenitelekezea kadi za magari na hati za nyumba.

Hapa siku nitageuka kuwa trafic na kukamata magari.
 
Nino vyeti, mimi wamenitelekezea kadi za magari na hati za nyumba.

Hapa siku nitageuka kuwa trafic na kukamata magari.
Vp ulishajaribu kuwacheck?
 
Nino vyeti, mimi wamenitelekezea kadi za magari na hati za nyumba.

Hapa siku nitageuka kuwa trafic na kukamata magari.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Biashara hii nzuri ila changamoto ndio kama hizi sasa
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Biashara hii nzuri ila changamoto ndio kama hizi sasa
Mimi kuna Jamaa kanichia hati ya nyumba mwaka unaenda wa tatu sasa, kila nikimtafuta anabadili namba na nikimpata ni sound tu.

Sasa nimesikia amazenguana na Mke wametengana, natafuta mawasiliano na Mke nikimpata nawachonganisha, nawaambia atakayenipa changu nampa hati.
 
Back
Top Bottom