Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
NAFSI INAPOGHADHIBIKA
Kuna mtu alisema maneno yasiyopendeza miaka miwili iliyopita siku kama ya leo ikabidi nimjibu lakini nilikuwa nimeghadhibika:
"Jack kadri utakavyojua na kujua huwezi ukaifahamu historia ya African Association kama alivyoijua Kleist Sykes na wanae au walivyoijua wajukuu zake Daisy Abdul Sykes na mdogo wake Kleist Abdul Sykes...au nilivyoijua mimi kufikia kuisahihisha historia iloyoandikwa na Chuo cha Kivukoni mwaka wa 1981 au kufikia mimi kuwa mmoja wa waandishi 500 kutoka kila pembe ya dunia walioandika Dictionary of African Biography (DAB), mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York (2011).
Hizi ni volume sita.
Huwezi kuijua historia ya Tanganyika kwa kiasi cha kufanya mhadhara wa somo hilo kama nilivyofanya vyuo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania pamoja na Northwestern University, Evanston, Chicago chuo kinachoongoza duniani katika African History...bado hujafanyiwa review ya kazi yako yoyote katika Cambridge Journal of African History...kote huko nimepita "in flesh and blood."
Leo kwa taarifa yako limeundwa jopo likiongozwa na Prof. Shivji linaandika historia ya Mwalimu Nyerere na nimefanyanao mahojiano nyumbani kwangu mara mbili na nimewapa nyaraka na picha.
Wao wameamua kufanya hilo katika kuiweka sawa historia ya uhuru wa Tanganyika na kitabu cha Abdul Sykes ndicho chanzo.
Sidhani kama wewe una lolote la kumstaajabisha yeyote.
Lakini eleza unachojua tutakusikiliza.
Nimetaabika kusema haya lakini imebidi ili tufahamiane vizuri.
Baada ya haya nadhani umeelewa kuwa Mohamed Said si mtu chembelecho, wa ''kulisha watu matango pori.''
Picha ya kwanza kulia: Nakala tofauti za matoleo ya kitabu cha Abdul Sykes, Northwestern University, Chicago, kulia Prof. Shivji, Prof. Saida Othman, na Dr, Ngw'aza Kamata na picha ya mwisho siku watoto wa Abdul Sykes waliponialika kunionyesha Medali ya Mwenge wa Uhuru aliyotunikiwa baba yao mwaka 2011 kwa nchi kutambua mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Ally Sykes pia alitunukiwa medali hii kwenye sherehe ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.
Kuna mtu alisema maneno yasiyopendeza miaka miwili iliyopita siku kama ya leo ikabidi nimjibu lakini nilikuwa nimeghadhibika:
"Jack kadri utakavyojua na kujua huwezi ukaifahamu historia ya African Association kama alivyoijua Kleist Sykes na wanae au walivyoijua wajukuu zake Daisy Abdul Sykes na mdogo wake Kleist Abdul Sykes...au nilivyoijua mimi kufikia kuisahihisha historia iloyoandikwa na Chuo cha Kivukoni mwaka wa 1981 au kufikia mimi kuwa mmoja wa waandishi 500 kutoka kila pembe ya dunia walioandika Dictionary of African Biography (DAB), mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York (2011).
Hizi ni volume sita.
Huwezi kuijua historia ya Tanganyika kwa kiasi cha kufanya mhadhara wa somo hilo kama nilivyofanya vyuo mbalimbali ndani na nje ya Tanzania pamoja na Northwestern University, Evanston, Chicago chuo kinachoongoza duniani katika African History...bado hujafanyiwa review ya kazi yako yoyote katika Cambridge Journal of African History...kote huko nimepita "in flesh and blood."
Leo kwa taarifa yako limeundwa jopo likiongozwa na Prof. Shivji linaandika historia ya Mwalimu Nyerere na nimefanyanao mahojiano nyumbani kwangu mara mbili na nimewapa nyaraka na picha.
Wao wameamua kufanya hilo katika kuiweka sawa historia ya uhuru wa Tanganyika na kitabu cha Abdul Sykes ndicho chanzo.
Sidhani kama wewe una lolote la kumstaajabisha yeyote.
Lakini eleza unachojua tutakusikiliza.
Nimetaabika kusema haya lakini imebidi ili tufahamiane vizuri.
Baada ya haya nadhani umeelewa kuwa Mohamed Said si mtu chembelecho, wa ''kulisha watu matango pori.''
Picha ya kwanza kulia: Nakala tofauti za matoleo ya kitabu cha Abdul Sykes, Northwestern University, Chicago, kulia Prof. Shivji, Prof. Saida Othman, na Dr, Ngw'aza Kamata na picha ya mwisho siku watoto wa Abdul Sykes waliponialika kunionyesha Medali ya Mwenge wa Uhuru aliyotunikiwa baba yao mwaka 2011 kwa nchi kutambua mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Ally Sykes pia alitunukiwa medali hii kwenye sherehe ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.