Nafsi ni kitu gani?

Nafsi ni kitu gani?

Heshima kwenu wadau, nijuavyo mi ni kwamba binadamu ana mihimili mikuu mitatu. Kwanza ni roho, pili ni mwili na tatu ni nafsi.

ROHO nafahamu ni ile pumzi ya uzima kutoka kwa mungu mwenyezi, ambayo ipo connected na Mungu mwenyewe.

MWILI ni Physical appearance ya mtu ambayo inajumuisha milango yote ya fahamu. Kwa suala la NAFSI bado sijalipatia ufumbuzi.

Naomba mwenye elimu zaidi atujuze.

Nafsi wewe mwenyewe.
Ukisoma kitabu kiitwacho Biblia, sehemu ya mwanzo sura ya pili mstali w saba. Mwanzo 2.7 pameeleza kuwa Baada ya kuumbwa binadamu akapuliziwa pimzi. Ndipo binadam akawa nafsi hai.

Ieleweke wazi kwamba binadamu hana nafsi, hivyo usisumbuke kuitafuta nafsi mwilini mwa binadamu. Bali huyo mtu ndio nafsi.

Andiko linasema binadamu akawa nafsi. Yaani baada ya kupuliziwa tu pimzi akawa nafsi.

Hivyo mkuu usihangaike kutafuta nafsi ipo wapi? Hata wewe ni nafsi.

Ukiulizwa wewe ni nani.. Jibu kuwa wewe ni nafsi.
 
Heshima kwenu wadau, nijuavyo mi ni kwamba binadamu ana mihimili mikuu mitatu. Kwanza ni roho, pili ni mwili na tatu ni nafsi.

ROHO nafahamu ni ile pumzi ya uzima kutoka kwa mungu mwenyezi, ambayo ipo connected na Mungu mwenyewe.

MWILI ni Physical appearance ya mtu ambayo inajumuisha milango yote ya fahamu. Kwa suala la NAFSI bado sijalipatia ufumbuzi.

Naomba mwenye elimu zaidi atujuze.
Mwanadamu hana miili mitatu mkuu bali mwanadamu ana sehemu kuu tatu yaani mwili, nafsi na roho.

Nafsi ni sehemu ambayo mawazo, hisia na utashi unapatikana.

Mwili kazi yake ni kutoa viashiria kama mtu anatawaliwa zaidi na nafsi yake au roho yake.

Ni kwa ufupi tu.
 
Vyote nisisi ndio tumetengeneza kwa lugha katika uhalisia hamna hata kimoja
 
Heshima kwenu wadau, nijuavyo mi ni kwamba binadamu ana mihimili mikuu mitatu. Kwanza ni roho, pili ni mwili na tatu ni nafsi.

ROHO nafahamu ni ile pumzi ya uzima kutoka kwa mungu mwenyezi, ambayo ipo connected na Mungu mwenyewe.

MWILI ni Physical appearance ya mtu ambayo inajumuisha milango yote ya fahamu. Kwa suala la NAFSI bado sijalipatia ufumbuzi.

Naomba mwenye elimu zaidi atujuze.
ROHO: NI hali ya uhai "activeness" in things and animals
Nafsi : ni msingi wa utambulisho tuu, cha hali ndani yake"Identity" Mfano unaposema nafsi yangu mimi nafsi yake yeye.
 
kwa faida yako, kuna aina mbili za ufahamu. 'conscious mind' na 'sub conscious mind'. conscious mind ni aina ya ufaham ambao nimeuzungumzia hapo juu. ni ule unatumia milango ya fahamu. ufahamu unadili na mambo ya hiari tu, kama vile kusikiliza, kula na mambo yote unayojiongoza katika kuyafanya. conscious mind ipo kwa ajili ya kuchambua kila tendo ulifanyalo. tukija kwenye sub conscious huu ni aina ya ufahamu hujiongoza wenyewe. hu deal na matendo yasiyo hiari, mfano unapolala conscious mind inakua haifanyi kaz. lakin kinachofanya mapigo ya moyo yaendelee kupiga, msukumo wa damu na kupumua ni sub conscious. i hope nimechangia.......Aseee Upo sawa mkubwa.!
there is only consious no subconcious...kuna watu wanaweza kusimamisha hali tofauti ambazo unaweza kusema ni involuntary....utofauti ni kwamba hatupo makini na consious yetu.
 
Mind: the element of a person that enables them to be aware of the world and their experiences, to think, and to feel; the faculty of consciousness and thought.

Soul: the spiritual or immaterial part of a human being or animal, regarded as immortal

Immortal: living forever; never dying or decaying

Kwa ufupi kabisa mwili ni mwili huu tunaouona,nafsi ni kama akiri ya roho,sehemu ya ufahamu ya roho,inayofanya maamuzi na kureason.Kwa habari za hukumu itakayohukumiwa ni nafsi ya mtu,roho inaangamia kama nafsi ikiangamizwa kwa sababu roho inabeba nafsi,huwezi tenganisha au naweza sema kila nafsi kuna roho inaandamana nayo.
 
Mind: the element of a person that enables them to be aware of the world and their experiences, to think, and to feel; the faculty of consciousness and thought.

Soul: the spiritual or immaterial part of a human being or animal, regarded as immortal

Immortal: living forever; never dying or decaying

Kwa ufupi kabisa mwili ni mwili huu tunaouona,nafsi ni kama akiri ya roho,sehemu ya ufahamu ya roho,inayofanya maamuzi na kureason.Kwa habari za hukumu itakayohukumiwa ni nafsi ya mtu,roho inaangamia kama nafsi ikiangamizwa kwa sababu roho inabeba nafsi,huwezi tenganisha au naweza sema kila nafsi kuna roho inaandamana nayo.


Wadau naomba tafadhali na mimi nitoe mawazo yangu, Mtu nI Roho ana kaa katika Mwili na anayo Nafsi. Kama Mungu Baba na Mwana na Roho Mtakatifu.

SisI tumeumbwa tukawa Triune being (1Thesalonike 5:23).

Nafsi inajengwa na element tatu za Mind as a leading part of the Soul (Nafsi) Will (Nia) and Emotions (Hisia)

Kwenye Mind ndio tuna intellect, Kwenye will ndio tuna Choices na Kwenye Emotions ndio tuna feelings. Hizi zinamtofautisha Mwana damu na lower animals.
 
Heshima.

Unaweza kupata mwangaza zaidi juu ya mashauri ya hayo ambayo ungelipenda kuyabaini namna zake za kuzungumzia.

Ninashauri ukisome kitabu hichi: The Aquarian Age Gospel of Jesus, the Christ of the Piscean Age Author Levi H. Dowling

Humo kuna mengi ya msaada mno kwa kadri ya kiu yako ya kutamani kujua mielekeo ya hakika kutambua ukweli.

Ila hapa nitanukuu aya moja na kukutafsiria kama kitekenyo.

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

Aquarian Age Gospel of Jesus
Injili ya zama za Ndoo ya Yesu


Chapters 8 - 14
Sura 8 - 14


CHAPTER 8
Sura ya 8


Elihu's lessons. The unity of life. The two selfs. The devil. Love the saviour of men. The David of the light. Goliath of the dark.


Masomo ya Elihu. Umoja wa Uzima. Nafsi mbili. Ibilisi. Upendo mwokozi wa Watu. Daudi wa nuru. Goliati wa giza.

AGAIN Elihu met his pupils in the sacred grove and said, TENA Elihu alikutana na wanafunzi wake uani patakatifu na kusema , 2 No man lives unto himself; for every living thing is bound by cords to every other living thing. Hakuna mtu ajiishiye tu yeye mwenyewe; kwa kuwa kila kile chenye kuishi chafungamana kamba na kila kingine chenye kuishi 3 Blest are the pure in heart; for they will love and not demand love in return. Wamebarikiwa wenye moyo safi; kwa kuwa wao wapenda na si kutaka upendo kurejeshwa. 4 They will not do to other men what they would not have other men do unto them. Hawatawatendea watu wengine vile wengine wasingaliwatendea wao 5 There are two selfs; the higher and the lower self. Kuna nafsi mbili; nafsi ya juu na ya chini 6 The higher self is human spirit clothed with soul, made in the form of God. Nafsi ya juu ni roho ya mtu kuvikwa sonafi, iliyofanyika kwa namna ya Mungu 7 The lower self, the carnal self, the body of desires,is a reflection of the higher self, distorted by the murky ethers of the flesh. Nafsi ya chini, nafsi ya mwili wa nyama, mwili wa matamanio, ni mwakisiko wa nafsi ya juu, kuharibiwa uhalisia wa sura yake na aetha nzito za nyama. 8 The lower self is an illusion, and will pass away; the higher self is God in man, and will not pass away. Nafsi ya chini ni danganyiko la kimuonekano, nayo itapita zake; nafsi ya juu ni Mungu katika mtu, nayo haitapita zake 9 The higher self is the embodiment of truth reversed, and so is falsehood manifest. Nafsi ya juu ni ujazwa mwili wa kweli katika namna iliyopinduka, na hivyo ni isikweli kudhahirika 10 The higher self is justice, mercy, love and right; the lower self is what the higher self is not. Nafsi ya juu ni usawa wa haki, rehema, upendo na sahihi; nafsi ya chini ni kile isivyo nafsi ya juu 11 The lower self breeds hatred, slander, lewdness, murders, theft, and everthing that harms; the higher self is mother of the virtues and the harmonies of life. Nafsi ya chini huzaa chuki, usingiziaji, ukosaji heshima, mauaji, uwizi, na kilakitu chenye kuleta madhara; Nafsi ya juu ni mama wa kudra njema na matangamano ya uzima 12 The lower self is rich in promises, but poor in blessedness and peace; it offers pleasure, joy and satisfying gains; but gives unrest and misery and death. Nafsi ya chini ni tajiri ya ahadi, lakini i ni masikini ya ubarikika na amani; yaahidi kupatia starehe, furaha na mapatiko ya kuridhisha nafsi; lakini hutoa kutokutulia na dhiki na mauti 13 It gives men apples that are lovely to the eye and pleasant to the smell; their cores are full of bitterness and gall. Huwapa watu matunda ambayo yenye kuonekana ya kupendeka na mazuri kwa harufu; ndani mwake yamejaa uchungu na nyongo 14 If you would ask me what to study I would say, yourselves; and when you will have studied them, and then would ask me what to study next, I would reply, yourselves. Ikiwa mtaniuliza kipi mngalikusoma kujua ningalisema, ninyi mwenyewe; na mara mtakapokuwa mmezisoma, na halafu kuniuliza kipi tusome kufuatia, ningaliwajibu, ninyi wenyewe. 15 He who knows well his lower self, knows the illusions of the world, knows of the things that pass away; and he who knows his higher self, know God; knows well the things that cannot pass away. Yeye aijuaye vema nafsi yake ya chini, ayajua madanganyiko ya kimuonekano ya ulimwengu, avijua vitu vyenye kupita kwenda zake; na yeye mwenye kuijua nafasi yake ya juu, amjua Mungu; avijue vile visivyoweza kupita. 16 Thrice blessed is the man who has made purity and love his very own; he has been ransomed from the perils of the lower self and is himself his higher self. Amebarikiwa mara tatu mtu aliyeufanya usafi wa moyo na upendo kuwa ni wake; yeye ametolewa gharama za kugombolewa toka kwenye kingo za maanguko za nafsi yake ya chini na yeye mwenyewe ni nafsi yake ya juu 17 Men seek salvation from an evil that they deem a living monster of the nether world; and they have gods that are but demons in disguise; all powerful, yet full of jealousy and hate and lust; Watu wanatafuta kukombolewa kutoka kwenye uovu ambao wao wachukulia kusema ni dubwana la mahala pa chini kuzimu ; na wana miungu ambayo ni mapepo pagaishaji yaliyo na sura ya kujificha; yenye nguvu tele, na hapo hapo kujaa chuki na matamanio ya kimwili;18 Whose favours must be bought with costly sacrifice of fruits, and of the lives of birds, and animals, and human kind. Ambayo fadhila zake lazima kununuliwa na kafara za kigharama za matunda, na za uhai wa ndege, na wanyama, na mwanadamu 19 And yet these gods possess no ears to hear, no eyes to see, no heart to sympathise, no power to save. Na hapo hapo miungu hao hawana masikio kusikia, hawana macho kuona, hawana moyo kuonea huruma, hawana nguvu kuokoa. 20 This evil is myth; these gods are made of air, clothed with shadows of a thought. Uovu huu ni ngano; miungu hawa wamefanyika kwa hewa, kuvikwa na vimvuli vya fikra. 21 The only devil from which men must be redeemed is self, the lower self. If man would find his devil he must look within; his name is self. Ibilisi pekee ambaye toka kwa huyo watu hawana budi kukombolewa ni nafsi, nafsi ya chini. Ikiwa mtu angalikumpata ibilisi wake yeye yampasa kutazama ndani yake; jina lake ni nafsi. 22 If man would find his saviour he must look within; and when the demon self has been dethroned the saviour, Love, will be exulted to the throne of power. Ikiwa mtu angalikumtafuta mwokozi wake yeye hana budi kutazama ndani yake; na pale ambapo ibilisi ametolewa katika kiti chake cha enzi mwokozi, upendo, atainuliwa kwenye kiti cha nguvu. 23 The David of the light is Purity, who slays the strong Goliath of the dark, and seats the saviour, Love, upon the throne. Daudi wa nuru ni usafi wa moyo, mwenye kumchinjilia mbali Goliati wa kiza, na kumketisha enzini mwokozi, Upendo.


Chanzo cha nukuu: The Aquarian Age Gospel of Jesus, the Christ of the Piscean Age
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

Baraka
nimekuelewa....
 
wanasayansi walifanya jaribio la kuchunguza roho wakati mtu anapofariki walimchukua mtu wakamweka katika box la kioo liliojaa maji mara baada ya yule mtu kukaribia kukata roho waliona maji yanatoa kitu kama povu walipochunguza kwa kina hakuna walichoona NB quran inasema wanakuuliza kuhusu habari za roho wambie roho ni katika mambo ya allah sw isopukuwa binadam tumepewa kwa kiasi kidogo sana ktk ilimu yake kwa watu aliowachagua hvyo basi hakuna mtu mwenye majibu sahihi ya mwili roho nafsi akili kwa sabab mwili huliwa na wadudu baada ya kufa lkn roho hurudi kwa allah sw nafsi ni matamanio yani yanweza kuwa mazuri au mabaya ila akili ni maamuzi yanaweza kuwa sahihi ama la.nafsi ikishatamani akili hupewa jukuma kuamua
 
Huwa nina jiuliza maswali mengi sana juu ya hivi vitu sijui ndio vitu, au ndio nini "roho, akili, nafsi".

Hivi vitu tunaambiwa kinadharia kwamba kila mtu anavyo lakini ukimuuliza anaekwambia kwamba una hivyo vitu viko wapi kama kweli ninavyo, Atakuletea misamiati mingi kweli na inayochanganya lakini kukuthibitishia kiko wapi hawezi.

Ninaamini kila mmoja wetu anaamini kwamba makao ya Akili ni kichwani lakini ukimfanyia mtu upasuaji wa kichwa huwezi kuzi kuta akili bali utakuta ubongo!

Sasa ninaomba kwa mwenye jibu nini huwa kinatokea mpaka akili ziwe kichwani lakini zisiwe zinaonekana atusaidie jibu.

Msamiati waki nadharia kama huo tuna ukuta kwenye ... hiki kitu kiitwacho ,Roho, nachenyewe hiki kitu kiitwacho .Roho,tuna ambiwa kina ishi ndani , ya moyo, wa mtu lakini ajabu. Na chenyewe hakithibitishiki , hakuna mtu anae weza kuni letea ,roho yamtu kama amba vyo hakuna mtu , mwenye uwezo wa kuniletea Akili , zamtu. Kama , pia kuna mtu mwenye uwezo wakuni saidia jibu nita shukuru sana , nini huwa kina fanya hivyo vitu visi onekane ?? Nani nani alie vigundua .. kwamaana havionekani........nani kwanini kama hatu wezi ku ziona Akili ni kwanini tusi amini , huwa tuna tumia ubongo kufikiri na wala sio akili zisizo onekana.

Misamiati kama hiyo hapo juu tuna kutana nayo tena kwenye kitu kiitwacho , nafsi hiki ndicho sijui hata kinadhaniwa kuishi wapi.

Ninawakaribisha wote ili tujiulize kwa pamoja kama vipo au havipo , tusije tukawa tunaamini vitu ambavyo ni nadharia tu na wala havipo.
wewe unachanganya madesa.
Nafsi ni kitu kingine Roho haikai kwenye Moyo...Roho na Nafsi vyote vipo kwenye ulimwengu wa Roho (Vitu visivyoonekana...na akili na Moyo vipo kwenye ulimwengu wa Mwili (Vitu vinavyoonekana)
Nafsi ni Identity yako wewe, ndio inayokutofautisha na binadamu mwengine yeyote yule kwenye huo ulimwengu wa nafsi. yenyewe hubeba riziki zako zote, uelewa na Vipaji vyote ulivyonavyo. Na nafsi haifi, itadumu milele na milele...ila muda ukifika, itauacha mwili wako. Unapoona watu wanapandwa na majini..ni kuwa wanaruhusu nafsi zao zikae pembeni, ili mwili wao utumike na hao majini. kwa wale wa kufanya Meditation, huwa wanazisafirisha nafsi zao na kwenda mahala pengine, huku wakiuacha mwili wao pale ulipo. ila wakibugi stepu, wanaweza wasirudi tena kwenye miili yao. na ndo amaana watu hufa.
hatujui mengi zaidi ya ulimwengu wa roho, na ndio maana wachawi na wengineo wanao uelewa mwingi zaidi wa dunia hiyo ya vitu visivyoonekana kwa macho ya mwili.
 
Roho ni ile pumzi tunayopuliziwa na mungu mwenyewe. na hii roho ndo kiunganish pekee kati yetu na mungu. siku hizo pumzi zitakapokata na ndo mwisho wa uhai wako hapa duniani.
Yah, Roho ni kama Activator/Verification/Password ya Wewe. Ni Daraja kuu kati yako na Mungu. Bila roho, hauwezi kuwa kiumbe chochote kile. Ni Mungu mwenyewe anajua, na ndio aliyokupulizia kukuumba, inaishi kizazi na kizazi kwa kuzaliana...e.t.c; na kwa kupitia hiyo, unapopiga goti na kusali, unatumia mawasiliano yako uliyonayo na Mungu, kuwasiliana naye mojakwamoja. na ndio maana anakusikia, na anaweza kukujibu au laa. nadhani ukijiuliza kwanini unafumba macho ukisali, utapata jibu sahihi, sio?
 
Vyote nisisi ndio tumetengeneza kwa lugha katika uhalisia hamna hata kimoja
Uhalisia upo, ukifanya utafiti yakinifu na kusoma kwa bidii, ndugu.
penye elimu ifuate, ili uijue, na sio kuishia nje....na kusema unayoyajua wewe
 
Nafsi: ni ufahamu unaomtambulisha mtu, ni utambuzi unaoidhinisha na kudhihirisha uwepo wa mhusika.
Kitabu cha mwanzo kinaeleza jinsi Adam alivyoumbwa toka mavumbini, Mungu alimpulizia pumzi ya uhai na Adam akawa nafsi hai.

Nafsi(soul) is self identity that presents a person.
 
Uhalisia upo, ukifanya utafiti yakinifu na kusoma kwa bidii, ndugu.
penye elimu ifuate, ili uijue, na sio kuishia nje....na kusema unayoyajua wewe
Labda huo utafiti ulioufanya ni upi?na umesoma wapi? Kabla hujafika hata mbali Nafsi ni nini? Na ipo wapi? Na kwanamna gani tunaweza kuifahama kama sio human invention
 
Labda huo utafiti ulioufanya ni upi?na umesoma wapi? Kabla hujafika hata mbali Nafsi ni nini? Na ipo wapi? Na kwanamna gani tunaweza kuifahama kama sio human invention
Soma vitabu vya Falsafa, na kisha pitia Maandiko ya Dini..utapata baadhi ya Majibu.
kama unataka niwe Tutor wako...pole sana. watafute wanaojua zaidi wakuelekeze
 
Soma vitabu vya Falsafa, na kisha pitia Maandiko ya Dini..utapata baadhi ya Majibu.
kama unataka niwe Tutor wako...pole sana. watafute wanaojua zaidi wakuelekeze
Nafsi inavyomaanisha kwa Falsafa ni tofauti naunayo maanisha? Kwa falsafa nafsi ni sawasawa na Mind!!
Dini ndio ipo njee kabisa hata wanaloelezea hawawezi kudhibitisha.
Wala sijasema wewe uwe Tutor wangu ninacho omba ujibu hayo maswali kusema nikasome vitabu nisawa nakuniambia nikasome mawazo ya mtu mwingine na wakati wewe unauwezo wakutoa uwelewa wako juu ya kitu unachoamin.
 
Back
Top Bottom