Nafurahi kuona kitu pekee ambacho CCM , CHADEMA, ACT Wazalendo wanakubaliana ni kuwa Magufuli hakufaa kuwa Rais wa hii nchi

Nafurahi kuona kitu pekee ambacho CCM , CHADEMA, ACT Wazalendo wanakubaliana ni kuwa Magufuli hakufaa kuwa Rais wa hii nchi

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Hili lipo wazi japo CCM wamekuwa hawalisemi sana hadharani, lakini unaona marekebisho yanayofanyika na ndipo hapa ninapojivunia kuwa mtanzania, wote hatujakubali uhayawani wa yule mtu na tulifurahi sana Mungu alivyoamua kesi na bahari imetulia

Pengine hata sio ndani ya Tanzania tu, nchi jirani nyingi hazikuweza kufanya kazi na Magufuli, hata Kagame ambaye Magufuli alikuwa akijipendekeza kwake kwa fujo alipoingia madarakani alikuja kumuona huyu mtu hafai na hata mazishi yake hakuhudhuria wala hakutuma mtu

Nashukuru watanzania tunakubaliana kwenye hili.
 
wote hatujakubali uhayawani wa yule mtu na tulifurahi sana Mungu alivyoamua kesi na bahari imetulia
Wote na nani?
Mimi usinisemee sijafurahi.
Huenda wapi wengine wengi hawapo pamoja nawe kwenye hiki kimawazo.

Unafurahia vipi kifo cha mwenzio?
Kisiasa pia sipo pamoja nawe.

Jisemee nafsi yako usiwasemee nafsibza wengine. Lililopo rohoni mwa mtu ni siri yake hadi aliweke hadharani mwenyewe kwa matendo au maneno.
 
Sass
Wote na nani?
Mimi usinisemee sijajafurahi.
Huenda wapi wengine wengi hawapo pamoja nawe kwenye hiki kimawazo.

Unafurahia vipi kifo cha mwenzio?
Kisiasa pia sipo pamoja nawe.

Jisemee nafsi yako usiwasemee nafsibza wengine. Lililopo rohoni mwa mtu ni siri yake hadi aliweke hadharani mwenyewe kwa matendo au maneno.
Sasa mapenzi ya Mungu tusiyafurahie? Tena hasa hayo mapenzi ya Mungu yakiwa yametuliza bahari?
 
Hili lipo wazi japo CCM wamekuwa hawalisemi sana hadharani, lakini unaona marekebisho yanayofanyika na ndipo hapa ninapojivunia kuwa mtanzania, wote hatujakubali uhayawani wa yule mtu na tulifurahi sana Mungu alivyoamua kesi na bahari imetulia

Pengine hata sio ndani ya Tanzania tu, nchi jirani nyingi hazikuweza kufanya kazi na Magufuli, hata Kagame ambaye Magufuli alikuwa akijipendekeza kwake kwa fujo alipoingia madarakani alikuja kumuona huyu mtu hafai na hata mazishi yake hakuhudhuria wala hakutuma mtu

Nashukuru watanzania tunakubaliana kwenye hili...
Jisemee wewe na wezi wenzako wa maliasili za nchi hii.

Jisemee wewe pamoja na watumbuliwa wote wa vyeti fake serikalini.

Jisemee wewe na wenzio mliozowea kuishi kwa kuwapunja wananchi wa kipato cha chini.

Jisemee wewe na Wapinzani Tumbopolitics waliobaki kwa sasa.

Magufuli hachafuki na ukitaka kumchafua utachafuka wewe.
View attachment 2251041View attachment 2251042
 
Hili halina ubishi kwamba jiwe alikuwa hafai.

Ndiyo maana mzee Diallo alisema "tuliongozwa na mtu aliyestahili kuwa Milembe.

Na askofu Mwingira akasema shetani alikuwa ikulu.

Mbowe akasema "never and never again.

Zitto akasema " nchi iliongozwa na washamba na malimbukeni"
 
Sass

Sasa mapenzi ya Mungu tusiyafurahie? Tena hasa hayo mapenzi ya Mungu yakiwa yametuliza bahari?
Siyo kila mapenzi ya Mungu yanafurahisha binadamu hasa wahusika wa tukio.

Yesu mwenyewe hakufurahia kifo chake kiasi kwamba akaomba ikiwezekana Mungu amuepushe na kikombe kile cha mateso na uchungu.
Ingawa mwishoni alimwambia Mungu mapenzi yake yatimie.
 
Siyo kila mapenzi ya Mungu yanafurahisha binadamu hasa wahusika wa tukio.

Yesu mwenyewe hakufurahia kifo chake kiasi kwamba akaomba ikiwezekana Mungu amuepushe na kikombe kile cha mateso na uchungu.
Ingawa mwishoni alimwambia Mungu mapenzi yake yatimie.
Sasa amani imepatikana, CCM wamepatana wao kwa wao, waliobambikiziwa kesi wameachiwa, walionyimwa haki zao wamepewa, Wapinzani wanaridhiana na CCM, taifa limeeudi kwenye umoja.
Kwa nini tusifurahie haya mapenzi mazuri ya Mungu?
 
Jisemee wewe na wezi wenzako wa maliasili za nchi hii.

Jisemee wewe pamoja na watumbuliwa wote wa vyeti fake serikalini.

Jisemee wewe na wenzio mliozowea kuishi kwa kuwapunja wananchi wa kipato cha chini.

Jisemee wewe na Wapinzani Tumbopolitics waliobaki kwa sasa.

Magufuli hachafuki na ukitaka kumchafua utachafuka wewe.
View attachment 2251041View attachment 2251042
Wafuasi wa Magufuli tatizo lenu ni kudhani kila aliyekuwa hakubaliani na yule mtu kuwa ni mhalifu
Na ndio maana alikuwa akiwaua na kuwafilisi?
 
Hili lipo wazi japo CCM wamekuwa hawalisemi sana hadharani, lakini unaona marekebisho yanayofanyika na ndipo hapa ninapojivunia kuwa mtanzania, wote hatujakubali uhayawani wa yule mtu na tulifurahi sana Mungu alivyoamua kesi na bahari imetulia

Pengine hata sio ndani ya Tanzania tu, nchi jirani nyingi hazikuweza kufanya kazi na Magufuli, hata Kagame ambaye Magufuli alikuwa akijipendekeza kwake kwa fujo alipoingia madarakani alikuja kumuona huyu mtu hafai na hata mazishi yake hakuhudhuria wala hakutuma mtu

Nashukuru watanzania tunakubaliana kwenye hili...
Hii joint agreement inatisha sana😅😅
 
Mungu anafurahia vifo? Atakuwa mungu siyo Mungu.
 
Wote na nani?
Mimi usinisemee sijafurahi.
Huenda wapi wengine wengi hawapo pamoja nawe kwenye hiki kimawazo.

Unafurahia vipi kifo cha mwenzio?
Kisiasa pia sipo pamoja nawe.

Jisemee nafsi yako usiwasemee nafsibza wengine. Lililopo rohoni mwa mtu ni siri yake hadi aliweke hadharani mwenyewe kwa matendo au maneno.
Kifo cha mtu mwovu ni faraja sana
 
Magufuli alikuwa mzalendo wa kweli na aliwashughulikia nyote mliohujumu nchi. Ninafikiri tumuache apumzike, endeleeni kulamba asali.
 
Jisemee wewe na wezi wenzako wa maliasili za nchi hii.

Jisemee wewe pamoja na watumbuliwa wote wa vyeti fake serikalini.

Jisemee wewe na wenzio mliozowea kuishi kwa kuwapunja wananchi wa kipato cha chini.

Jisemee wewe na Wapinzani Tumbopolitics waliobaki kwa sasa.

Magufuli hachafuki na ukitaka kumchafua utachafuka wewe.
View attachment 2251041View attachment 2251042
Magufuli alijichafua mwenyewe kwa matendo yake ya kishetani
 
Back
Top Bottom