Nafuu tusiwe na utambulisho kuliko singeli kuwa utambulisho wa muziki wa Tanzania

Basi na hiyo singeli iachwe isambae, kama inapendeka. Wewe unaona ni fair ku-declare mziki unaochezwa sehemu ndogo tu za mkoa mmoja kuwa ni wa taifa? Mziki ambao wengi hawakubali na hawataki kabisa kuusikia. Kwa nini umma usipewa nafasi ya kuamua?
Mkuu tangu lini tumewahi kuwa na jambo la "umma" hapa kwetu?!
Kila jambo ni la kisiasa na linaamuliwa kisiasa. Zamani kulikuwa na mashindano ya muziki wa dansi na kwenye mashindano hayo nyimbo zilikuwa na vionjo vya midundo ya kikabila. Mashindano yale ilikuwa zaidi ya Yanga na Simba... Laiti yangeendelezwa yale mashindano sidhani kama kiongozi angejitokeza na kuamua jambo kivyake tu.

Uwezo wa kufikiri na kupambanua mambo viongozi wetu umefika mwisho,twende na "singeli" mkuu
 
Unaweza kutokwa povu bure kumbe na wao walilenga kulitambulisha Taifa na yaliyomo kupitia wimbo wa Taifa
 
Nafuu kama wameshindwa kabisa wangetumia nyimbo au midundo ya msondo ngoma
 
Aliona kwenye sherehe za kuzaliwa Chama 5/2
 
Hio miziki ya kipumbavu inayoua akili za vijana thus hawana ubunifu wowote zaidi ya kulalamika maisha magumu wakati wamezungukwa na fursa tele
Tuziweke baadhi ya majina ya nyimbo zao au mm naongea mnanda kina saidi dabani au safari ya sauzi dah hyo misauti na kulalalmika
 
Unashida na singeli au na wimbo wa dulla makabila?
 
Singeli inajulikana mikoa mingapi? Hili jambo sidhani ni la viongozi kupanga. Waachie wananchi waamue. Kinachofanya Tanzania iwe na ugumu wa kuwa na mziki au vazi la taifa ni kuwa makabila yapo mengi sana hivyo kuja na kitu common itakuwa ngumu.
Mikoa yote imagine Hadi wamasai wanacheza singeli
 
Tatizo mziki wa singers unausishwa na uchafu na kupenda uchafu ...labda wawekeze kwenye kuufanya uhusishwe na usafi ndiyo unaweza kuwa mzuri kidogo na wahadhi kwa jamii ....kama tumeshindwa kuboresha vifaa vya kitamaduni tulivyo navyo na kuvifanya vya mvuto kama ngoma ngao mikuki na kuboresha ngoza za 8takaduni ziwe katika usasa je tutaweza kuifanya sengeri kuwa ya kisasa
 
Rais amuonee huruma huyu mzee amrudishe kwenye wizara ya katiba na sheria huku a
Rais amuonee huruma huyu mzee amrudishe kwenye wizara ya katiba na.sheria ama ampumzishe huku alipomuweka anapuyanga tu
 
Huu mziki ni mchafu unachafua akili za vijana na kuwafanya wazidi kuwa masikini hakuna cha maana zaidi ya kupromote ngono na ujinga kwenye fikra za vijana maana akili inaharibika kwa kile ionacho au isikiacho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…