Nahisi mama mkwe wangu ni vampire

Nahisi mama mkwe wangu ni vampire

Nipe namba ya huyo mama mkwe wako.
Ana nyege tu ndio zinazompa hasira kali.
Mm ni mstaafu (over 60+) naamini tunaweza kuelewana Kiutu uzima nikamtuliza hasira na wenge lake.
 
Hilo tatizo liko rohoni na yeye hawezi kujicontrol,anahitaji msaada wa kiroho
Ila kwa sasa usiache watoto hapo kabisa mana asipowatoa damu atawafanyia mengine msiyoyatarajia kwasababu ametekwa na nguvu za giza
 
Huyo mama ni kichaa kabisa yaani ondoka fasta ndugu yangu!
 
Nimekuja ukweni kuwaleta watoto baada ya kufunga shule Ijumaa ya juzi, waje kwa Bibi yao, Babu yao alishatangulia mbele ya haki.

Hapa mama mkwe anaishi na watoto wake wawili wa kike ambao nao Wana watoto, hivyo basi mama mkwe anaishi na wajukuu zake pia.

Kuna kitu kiko very weird nimekiona. Mama mkwe ni mkali sana, ana hasira sana, akianza kupiga, hasira hazimuishi mpaka amuume na amtoe damu huyo anayempiga ndipo hutulia.

Jana nilipofika, mtoto wa nyumba jirani alikuja kuchota maji hapa, akaondoka akaacha maji yanatiririka bombani, mama mkwe akafoka sana kwa hasira na ukali wa juu.

Akaenda kwenye nyumba jirani akakavuta hako katoto, kakapiga sana kisha akakauma Sana mpaka damu zikamtoka, hakika kamjeruhi mtoto wa watu. Wenye mtoto wamepeka malalamiko serikali ya mtaa kesho kaitwa ofisini akajieleze.

Juzi jumapili mjukuu wake wa form 2 ambaye ni mtoto wa shemeji yangu kasahau biblia Kanisani kwa bahati mbaya, kapigwa Sana, Kisha akamuuma begani, kamuachia kidonda kikubwa Sana.

Nasikia ni kawaida yake kuonja damu kidogo, huwa anajikata kidogo apate damu. Hata akipika nyama anatenga ya kwake anataka iwe haijaiva, iwe nyekundu ndani.

Nilikuwa nimepanga tukae Hadi X mas, lakini kwa haya ninayoyaona, asije pandikiza hayo maroho kwa wanangu, kesho naanza maandalizi ya kurudi.

Je, hivi hili nyie wenzangu mnalionaje?
Hii kama nilishaisoma, hujawahi kuileta miaka ya nyuma?
 
Nasubiri muendelezo wa hii thd,Mama mkwe kamuua sikio mtu kama ilivyokua ile mechi ya boxing kati ya Tyson vs Evander Holyfield.
 
Nimekuja ukweni kuwaleta watoto baada ya kufunga shule Ijumaa ya juzi, waje kwa Bibi yao, Babu yao alishatangulia mbele ya haki.

Hapa mama mkwe anaishi na watoto wake wawili wa kike ambao nao Wana watoto, hivyo basi mama mkwe anaishi na wajukuu zake pia.

Kuna kitu kiko very weird nimekiona. Mama mkwe ni mkali sana, ana hasira sana, akianza kupiga, hasira hazimuishi mpaka amuume na amtoe damu huyo anayempiga ndipo hutulia.

Jana nilipofika, mtoto wa nyumba jirani alikuja kuchota maji hapa, akaondoka akaacha maji yanatiririka bombani, mama mkwe akafoka sana kwa hasira na ukali wa juu.

Akaenda kwenye nyumba jirani akakavuta hako katoto, kakapiga sana kisha akakauma Sana mpaka damu zikamtoka, hakika kamjeruhi mtoto wa watu. Wenye mtoto wamepeka malalamiko serikali ya mtaa kesho kaitwa ofisini akajieleze.

Juzi jumapili mjukuu wake wa form 2 ambaye ni mtoto wa shemeji yangu kasahau biblia Kanisani kwa bahati mbaya, kapigwa Sana, Kisha akamuuma begani, kamuachia kidonda kikubwa Sana.

Nasikia ni kawaida yake kuonja damu kidogo, huwa anajikata kidogo apate damu. Hata akipika nyama anatenga ya kwake anataka iwe haijaiva, iwe nyekundu ndani.

Nilikuwa nimepanga tukae Hadi X mas, lakini kwa haya ninayoyaona, asije pandikiza hayo maroho kwa wanangu, kesho naanza maandalizi ya kurudi.

Je, hivi hili nyie wenzangu mnalionaje?
Anataka mtoko na mkwe, atatulia.
 
Back
Top Bottom