Nahisi naanza kuchanganyikiwa, wapi nitapata tiba?

Nahisi naanza kuchanganyikiwa, wapi nitapata tiba?

mimi mtakatifu

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2019
Posts
248
Reaction score
539
Nimefikisha mwaka tangu nipoteze ajira baada ya kuingia COVID-19.

Kwa sasa nipo mtaani kwa muda mrefu sina shughuli yoyote ya kufanya sababu nilikuwa ni mtu naeishi maisha ya ku-dedicate muda wangu na nguvu zangu kwenye kazi za ofisi.

Sikuwai kuwaza kama kuna siku naweza kukaa bila kupata ajira kwa muda wote huu. Nimeishi miaka mingi ya kuajiriwa na kuna kazi nilikuwa natafutwa bila kuomba.

Leo hii nafanya application hata interview siitwi na nikiitwa sipati feedback. Imefika wakati nikiingia kwenye interview natetemeka nakuwa muoga nashindwa kujibu.

Kifupi maisha yangu yamebadilika yamekuwa magumu sana. Kula imekuwa ya shida na sasa hata kodi nimeshindwa kulipa naishi maisha ya kumkwepa mwenye nyumba.

Kuna kipindi nilikuwa nimeingia kwenye ulevi wa kupindukia nikijaribu kuitafuta relief ya maisha. Afya ilidhoofu majanga yakawa mengi nashukuru nilipata rafiki yangu mmoja alinitoa huko japo mara moja moja uwa narudi kwenye ulevi na kutoka.

Sasa hivi nahisi nimeanza kupata kitu kama kichaa nna hali sio ya kawaida. Naskia hasira kali sana muda wote, nasahau vitu kwa haraka mpaka watu nawasahu kibaya zaidi napata tatizo la ganzi kwenye mwili nikiwa kwenye mawazo. Siwezi kufikiria vizuri mimi ni mwandishi mzuri ila kwa sasa hata uwezo wangu wa drafting umeshuka sana.

Yani nimekuwa naishi kama kasha flani lisilo na kitu.Natafuta unafuu na amani lakini nimeshindwa kuipata kwenye pombe na strehe, kwenye wanawake hata ibadani siipati amani rohoni kwangu.

Kuna muda nataman kama nisiwepo kabisa duniani nisione mateso zaidi yanayokuja mbele yangu.

I am so scared. I cry almost every night pamoja na uanaume wangu na sijui nafanyeje.

Dah naomba Mungu anisaidie nafsi yangu ipone sipo sawa kabisa.
 
Wanaume tumeumbiwa mateso.

Hata mimi bro kipindi kovid inaingia kibarua kiliota. Hadi mke alinikimbia kwa msoto niliopitia.

Ila sasahivi MOMENTUM naanza kurudi kwenye rait traki.

Usikate tamaa pambana.

Oneday utarudi kusoma huu uzi wako kisha utajicheka.
 
Nikawaida ya mwanadamu kufika Hali Kama hiyo hasa anapo kuwa na sonona, nirahisi kupata majibu ya kujidhuru unapo jitenga na wenzio.

Sasa anza kutembelea wagongwa mahospilalini mara kwa mara ili uone BINADAMU anavyo hangaika kwa kuokoa uhai, Jambo lingine kubali kuwa kwa sasa maisha yamegeuka kiuchumi isitoshe jaribu kukaa na watu wa kiroho (dini) na eleza kinacho kusibu waweza pata sululisho japo kwa kiasi.

Pole ndungu jipe moyo ushindi upo. Pombe sio jibu, badili mfumo wako wa maisha.
 
U wapi utakatifu wako?

I wapi imani yako kwa Mungu wako?

Mbona hukumbuki la kukuweka hai mpaka sasa? Huna kesi polisi, wala huko kwenye kitanda cha hospital

Una simu janja, una bando na una muda wa kuingia JF kuandika haya! Unapaswa kumshukuru Mungu pakubwa mno.

Kuna wengine hawana hata uwezo wa kumiliki smartphone

Kuna wengine hawana hata pa kulala.wako kwenye korido za watu wanapigwa baridi.

Kuna wengine muda huu wameshauza kila kitu hana cha kuuza tena

Kuna wengine wananuka madeni na hawakopesheki tena

Kuna wengine kesho vyombo vinatolewa nje kodi wameshindwa kulipa

Kuna wengine wanauguliwa na ndani hawana senti tano...Nknk

Shida inapokukamata wakumbuke na hawa kisha Mshukuru Mungu sana

Imagine umemaliza mwaka bila kazi na bado upo hai..mzima wa afya.. Hili pekee ni kubwa sana!

Usijione mnyonge
Usikate tamaa
Usipoteze tumaini
Mungu hatakupa jaribu kukuzidi, Mungu hatafunga milango yote, kuna mmoja utakuwa wazi ..Kumbuka hata usiku uwe mrefu kiasi gani kutapambazuka!

Mungu katika Biblia Takatifu anatuasa tusiogope..na hili neno USIOGOPE limerudiwa mara 365 kwenye Bible! Tafsiri yake ninini? Hupswi kuogopa hata siku moja maana yeye yu pamoja nawe!

Bado una nafasi ya pa kuweka mgongo upumzike
Bado una nafasi ya kuweza kuandika hata hii mada
Back una nafasi ya kuweza kupata chochote cha kutia kinywani bila shida
Bado una nafasi ya kuweza kuoga na kubadili nguo..Mshukuru sana Mungu

Kama huumwi
Kama huna kesi
Kama after iko vizuri
Kama akili iko sawa ... Tayari una mtaji mkubwa sana wa kuendelea na mapambano... Mshukuru Mungu kwa hilo...
Don't give up for in the darkest hours of time there is always a twinkle of light to lead you through...!

 
Mwaka mmoja tu?watu wako tangu 2012 mpk leo hawajapata ajira na wako wanapambana na hali yao.
 
Wanaume tumeumbiwa mateso..
Hata mimi bro kipindi kovid inaingia kibarua kiliota..hadi mke alinikimbia kwa msoto niliopitia..

Ila sasahivi MOMENTUM naanza kurudi kwenye rait traki.

Usikate tamaa pambana.
Oneday utarudi kusoma huu uzi wako kisha utajicheka.
Asante mkuu.
 
Nikawaida ya mwanadamu kufika Hali Kama hiyo hasa anapo kuwa na sonona, nirahisi kupata majibu ya kujidhuru unapo jitenga na wenzio.

Sasa anza kutembelea wagongwa mahospilalini mara kwa mara ili uone BINADAMU anavyo hangaika kwa kuokoa uhai, Jambo lingine kubali kuwa kwa sasa maisha yamegeuka kiuchumi isitoshe jaribu kukaa na watu wa kiroho (dini) na eleza kinacho kusibu waweza pata sululisho japo kwa kiasi.

Pole ndungu jipe moyo ushindi upo. Pombe sio jibu, badili mfumo wako wa maisha.
Asante sana nimekuelewa.
 
U wapi utakatifu wako?
I wapi imani yako kwa Mungu wako?
Mbona hukumbuki la kukuweka hai mpaka sasa? Huna kesi polisi, wala huko kwenye kitanda cha hospital
Una simu janja, una bando na una muda wa kuingia JF kuandika haya! Unapaswa kumshukuru Mungu pakubwa mno...
Kuna wengine hawana hata uwezo wa kumiliki smartphone
Kuna wengine hawana hata pa kulala.wako kwenye korido za watu wanapigwa baridi..
Kuna wengine muda huu wameshauza kila kitu hana cha kuuza tena
Kuna wengine wananuka madeni na hawakopesheki tena
Kuna wengine kesho vyombo vinatolewa nje kodi wameshindwa kulipa
Kuna wengine wanauguliwa na ndani hawana senti tano...Nknk
Shida inapokukamata wakumbuke na hawa kisha Mshukuru Mungu sana
Imagine umemaliza mwaka bila kazi na bado upo hai..mzima wa afya.. Hili pekee ni kubwa sana!

Usijione mnyonge
Usikate tamaa
Usipoteze tumaini
Mungu hatakupa jaribu kukuzidi, Mungu hatafunga milango yote, kuna mmoja utakuwa wazi ..Kumbuka hata usiku uwe mrefu kiasi gani kutapambazuka...!

Mungu katika Biblia Takatifu anatuasa tusiogope..na hili neno USIOGOPE limerudiwa mara 365 kwenye Bible! Tafsiri yake ninini? Hupswi kuogopa hata siku moja maana yeye yu pamoja nawe...!

Bado una nafasi ya pa kuweka mgongo upumzike
Bado una nafasi ya kuweza kuandika hata hii mada
Back una nafasi ya kuweza kupata chochote cha kutia kinywani bila shida
Bado una nafasi ya kuweza kuoga na kubadili nguo..Mshukuru sana Mungu

Kama huumwi
Kama huna kesi
Kama after iko vizuri
Kama akili iko sawa ... Tayari una mtaji mkubwa sana wa kuendelea na mapambano... Mshukuru Mungu kwa hilo...
Don't give up for in the darkest hours of time there is always a twinkle of light to lead you through...!

Shukrani sana kwa neno lako la kutia matumaini. Be blessed!
 
tafuta sehemu hata uvolunteer for free kwa muda ndo kazi zinapatikana hivo sikuhiz, pia itakusaidia kutengeneza connections mpya.usiogope kuanza upya that's life
 
Mkuu pole sana, hiyo hali unayoipitia naamini ni Mungu anakuonesha namna vijana wenzako tunaipitia ambao hatujawahi hata kuipata ajira hata ya kujishikiza

Nakushauri tu usikate tamaa, na Mungu akikupa kazi tena ujitahidi kuwashika mkono na vijana wengine watakaokua wanahitaji msaada wako kwenye mambo ya kazi

Kila la heri mkuu!
 
Amani utaipata kwa Yesu tu! Kwingine ni ya muda tu!

Alisema amani tangu nawapa si kama ya dunia hii.

Cha kwanza kubali kuwa huna kazi, hujakubaliana na kilichotokea ndo maana unapata shida!

Ukishakubali mpe Mungu nafasi uone kama hajafanya

Sent from my TECNO P701 using JamiiForums mobile app
 
Wanaume tumeumbiwa mateso.

Hata mimi bro kipindi kovid inaingia kibarua kiliota. Hadi mke alinikimbia kwa msoto niliopitia.

Ila sasahivi MOMENTUM naanza kurudi kwenye rait traki.

Usikate tamaa pambana.

Oneday utarudi kusoma huu uzi wako kisha utajicheka.
Duh,serious[emoji119]yaani mke kabisa alikimbia?

Sent from my TECNO P701 using JamiiForums mobile app
 
Pole, Ila katika maisha usitegemee kitu kimoja kama chanzo cha kipato. Mf. Mwalimu anauza maandazi, genge nyumbani, na biashara ndogondogo huku anatekeleza wajibu wake kama mwalimu.

Kibarua kikiota majani anaegemea kwenye mambo yake na maisha yanasonga. Ila usikate tamaa,piga kazi yoyote ya halali Ili mradi mkono uende kinywani.
 
Back
Top Bottom