Nahisi naanza kuchanganyikiwa, wapi nitapata tiba?

Nahisi naanza kuchanganyikiwa, wapi nitapata tiba?

I am so scared. I cry almost every night pamoja na uanaume wangu na sijui nafanyeje.
Umeshindwa kuvua hiyo kofia ya degree/diploma
unayopitia ni dhahiri chakukusaidia amua kubadilika amua kujishughulisha na Kazi za mikono Toka kwenye Hayo maisha ya gharama hama ulipo kaanze upya usilinganishe wakati yameshatokea yote usilalame weka Nia Fanya hata vibarua tambua tunaishi sasa sio Jana, hivyo ishi sasa
 
U wapi utakatifu wako?
I wapi imani yako kwa Mungu wako?
Mbona hukumbuki la kukuweka hai mpaka sasa? Huna kesi polisi, wala huko kwenye kitanda cha hospital
Una simu janja, una bando na una muda wa kuingia JF kuandika haya! Unapaswa kumshukuru Mungu pakubwa mno...
Kuna wengine hawana hata uwezo wa kumiliki smartphone
Kuna wengine hawana hata pa kulala.wako kwenye korido za watu wanapigwa baridi..
Kuna wengine muda huu wameshauza kila kitu hana cha kuuza tena
Kuna wengine wananuka madeni na hawakopesheki tena
Kuna wengine kesho vyombo vinatolewa nje kodi wameshindwa kulipa
Kuna wengine wanauguliwa na ndani hawana senti tano...Nknk
Shida inapokukamata wakumbuke na hawa kisha Mshukuru Mungu sana
Imagine umemaliza mwaka bila kazi na bado upo hai..mzima wa afya.. Hili pekee ni kubwa sana!

Usijione mnyonge
Usikate tamaa
Usipoteze tumaini
Mungu hatakupa jaribu kukuzidi, Mungu hatafunga milango yote, kuna mmoja utakuwa wazi ..Kumbuka hata usiku uwe mrefu kiasi gani kutapambazuka...!

Mungu katika Biblia Takatifu anatuasa tusiogope..na hili neno USIOGOPE limerudiwa mara 365 kwenye Bible! Tafsiri yake ninini? Hupswi kuogopa hata siku moja maana yeye yu pamoja nawe...!

Bado una nafasi ya pa kuweka mgongo upumzike
Bado una nafasi ya kuweza kuandika hata hii mada
Back una nafasi ya kuweza kupata chochote cha kutia kinywani bila shida
Bado una nafasi ya kuweza kuoga na kubadili nguo..Mshukuru sana Mungu

Kama huumwi
Kama huna kesi
Kama after iko vizuri
Kama akili iko sawa ... Tayari una mtaji mkubwa sana wa kuendelea na mapambano... Mshukuru Mungu kwa hilo...
Don't give up for in the darkest hours of time there is always a twinkle of light to lead you through...!



Umetoa ushauri wa busara sana mkuu.

Wengi tutajifunza kupitia hii comment.
 
tafuta sehemu hata uvolunteer for free kwa muda ndo kazi zinapatikana hivo sikuhiz, pia itakusaidia kutengeneza connections mpya.usiogope kuanza upya that's life
Nimeomba sehemu nyingi ngoja niendelee kufanya application. Asante kwa ushauri.
 
Mkuu pole sana, hiyo hali unayoipitia naamini ni Mungu anakuonesha namna vijana wenzako tunaipitia ambao hatujawahi hata kuipata ajira hata ya kujishikiza

Nakushauri tu usikate tamaa, na Mungu akikupa kazi tena ujitahidi kuwashika mkono na vijana wengine watakaokua wanahitaji msaada wako kwenye mambo ya kazi

Kila la heri mkuu..!!!!
Asante mkuu, shule niliyopitia kipindi hiki ni kubwa mno. Naomba Mungu akinipa neema nisije kusahau haya mafunzo.
 
Kuna watu toka wamalize elimu zao hawajapata ajila kwa ww ambae uliwai kupata ajila nafasi yako imekwisha pisha wasioajiliwa,

Acha kuwaza kuajiliwa embu jiajili mwenyewe tafuta jambo ufanye ukiwa na pesa kiasi fulani nenda kwa fundi piki piki mpe mwambie nimekwama naomba nikae hapa ofic kwako nijifundishe kazi ndogo ndogo na hii pesa ndio sehemu yangu ya malipo yangu, ukae pale ujifundishe ufundi mwisho wa cku utakuwa fundi kamili na utakuwa umejiajili mwenyewe.
 
Nimefikisha mwaka tangu nipoteze ajira baada ya kuingia covid 19.

Kwa sasa nipo mtaani kwa muda mrefu sina shughuli yoyote ya kufanya sababu nilikuwa ni mtu naeishi maisha ya ku-dedicate muda wangu na nguvu zangu kwenye kazi za ofisi.

Sikuwai kuwaza kama kuna siku naweza kukaa bila kupata ajira kwa muda wote huu. Nimeishi miaka mingi ya kuajiriwa na kuna kazi nilikuwa natafutwa bila kuomba.
Leo hii nafanya application hata interview siitwi na nikiitwa sipati feedback. Imefika wakati nikiingia kwenye interview natetemeka nakuwa muoga nashindwa kujibu.

Kifupi maisha yangu yamebadilika yamekuwa magumu sana. Kula imekuwa ya shida na sasa hata kodi nimeshindwa kulipa naishi maisha ya kumkwepa mwenye nyumba.

Kuna kipindi nilikuwa nimeingia kwenye ulevi wa kupindukia nikijaribu kuitafuta relief ya maisha. Afya ilidhoofu majanga yakawa mengi nashukuru nilipata rafiki yangu mmoja alinitoa huko japo mara moja moja uwa narudi kwenye ulevi na kutoka.

Sasa hivi nahisi nimeanza kupata kitu kama kichaa nna hali sio ya kawaida. Naskia hasira kali sana muda wote, nasahau vitu kwa haraka mpaka watu nawasahu kibaya zaidi napata tatizo la ganzi kwenye mwili nikiwa kwenye mawazo. Siwezi kufikiria vizuri mimi ni mwandishi mzuri ila kwa sasa hata uwezo wangu wa drafting umeshuka sana.

Yani nimekuwa naishi kama kasha flani lisilo na kitu.Natafuta unafuu na amani lakini nimeshindwa kuipata kwenye pombe na strehe, kwenye wanawake hata ibadani siipati amani rohoni kwangu.

Kuna muda nataman kama nisiwepo kabisa duniani nisione mateso zaidi yanayokuja mbele yangu.

I am so scared. I cry almost every night pamoja na uanaume wangu na sijui nafanyeje.

Dah naomba Mungu anisaidie nafsi yangu ipone sipo sawa kabisa.
Pole sana. Usikate tamaa.

Kama huna wategemezi hakikisha unajizuia na kutokuwa na matamanio mengi na makubwa hasa kipindi hiki usichokuwa na ajira. Hiyo itakupunguzia hasira taratibu na pressure. Matamanio yako ya siku yawe ni kupata chakula na sehemu ya kulala. Baada ya muda uta stabilize afya yako then utaanza kuwaza kwa usahihi.
 
Asante madam..nitakutafuta private.
U wapi utakatifu wako?
I wapi imani yako kwa Mungu wako?
Mbona hukumbuki la kukuweka hai mpaka sasa? Huna kesi polisi, wala huko kwenye kitanda cha hospital
Una simu janja, una bando na una muda wa kuingia JF kuandika haya! Unapaswa kumshukuru Mungu pakubwa mno...
Kuna wengine hawana hata uwezo wa kumiliki smartphone
Kuna wengine hawana hata pa kulala.wako kwenye korido za watu wanapigwa baridi..
Kuna wengine muda huu wameshauza kila kitu hana cha kuuza tena
Kuna wengine wananuka madeni na hawakopesheki tena
Kuna wengine kesho vyombo vinatolewa nje kodi wameshindwa kulipa
Kuna wengine wanauguliwa na ndani hawana senti tano...Nknk
Shida inapokukamata wakumbuke na hawa kisha Mshukuru Mungu sana
Imagine umemaliza mwaka bila kazi na bado upo hai..mzima wa afya.. Hili pekee ni kubwa sana!

Usijione mnyonge
Usikate tamaa
Usipoteze tumaini
Mungu hatakupa jaribu kukuzidi, Mungu hatafunga milango yote, kuna mmoja utakuwa wazi ..Kumbuka hata usiku uwe mrefu kiasi gani kutapambazuka...!

Mungu katika Biblia Takatifu anatuasa tusiogope..na hili neno USIOGOPE limerudiwa mara 365 kwenye Bible! Tafsiri yake ninini? Hupswi kuogopa hata siku moja maana yeye yu pamoja nawe...!

Bado una nafasi ya pa kuweka mgongo upumzike
Bado una nafasi ya kuweza kuandika hata hii mada
Back una nafasi ya kuweza kupata chochote cha kutia kinywani bila shida
Bado una nafasi ya kuweza kuoga na kubadili nguo..Mshukuru sana Mungu

Kama huumwi
Kama huna kesi
Kama after iko vizuri
Kama akili iko sawa ... Tayari una mtaji mkubwa sana wa kuendelea na mapambano... Mshukuru Mungu kwa hilo...
Don't give up for in the darkest hours of time there is always a twinkle of light to lead you through...!

Mshana Jr you are a blessing. Hakika nimefarijika sana.
 
U wapi utakatifu wako?
I wapi imani yako kwa Mungu wako?
Mbona hukumbuki la kukuweka hai mpaka sasa? Huna kesi polisi, wala huko kwenye kitanda cha hospital
Una simu janja, una bando na una muda wa kuingia JF kuandika haya! Unapaswa kumshukuru Mungu pakubwa mno...
Kuna wengine hawana hata uwezo wa kumiliki smartphone
Kuna wengine hawana hata pa kulala.wako kwenye korido za watu wanapigwa baridi..
Kuna wengine muda huu wameshauza kila kitu hana cha kuuza tena
Kuna wengine wananuka madeni na hawakopesheki tena
Kuna wengine kesho vyombo vinatolewa nje kodi wameshindwa kulipa
Kuna wengine wanauguliwa na ndani hawana senti tano...Nknk
Shida inapokukamata wakumbuke na hawa kisha Mshukuru Mungu sana
Imagine umemaliza mwaka bila kazi na bado upo hai..mzima wa afya.. Hili pekee ni kubwa sana!

Usijione mnyonge
Usikate tamaa
Usipoteze tumaini
Mungu hatakupa jaribu kukuzidi, Mungu hatafunga milango yote, kuna mmoja utakuwa wazi ..Kumbuka hata usiku uwe mrefu kiasi gani kutapambazuka...!

Mungu katika Biblia Takatifu anatuasa tusiogope..na hili neno USIOGOPE limerudiwa mara 365 kwenye Bible! Tafsiri yake ninini? Hupswi kuogopa hata siku moja maana yeye yu pamoja nawe...!

Bado una nafasi ya pa kuweka mgongo upumzike
Bado una nafasi ya kuweza kuandika hata hii mada
Back una nafasi ya kuweza kupata chochote cha kutia kinywani bila shida
Bado una nafasi ya kuweza kuoga na kubadili nguo..Mshukuru sana Mungu

Kama huumwi
Kama huna kesi
Kama after iko vizuri
Kama akili iko sawa ... Tayari una mtaji mkubwa sana wa kuendelea na mapambano... Mshukuru Mungu kwa hilo...
Don't give up for in the darkest hours of time there is always a twinkle of light to lead you through...!

Upo sahihi kabisa. Ukitaka kumshukuru Mungu tizama walio chini yako either kwa kipato, afya matatizo nk lazima utajikuta unamshukuru Mungu na kupata nguvu mpya
 
Tatizo lililopo unashindwa kukubaliana na hali iliyolukuta unataka kufosi maisha.
Kuna watu wamesoma na hawajawahi kuajiriwa, mtu hajawahi kumiliki hata sofa na maisha yanaendelea tu.. maisha yakibadilila na wewe unapita nayo japo ni ngumu kama ulishazoea mambo mazuri.
Nna bro wangu saivi kawa kama omba omba tangu aachishwe kazi nmemwambia hayo maisha unayoona unayaishi saivi sisi ndo maisha yetu ya kila siku kaza msuli Bro.
Depression zipo sana kikubwa usikae pekeyako, nenda mtafute Mungu hudhuria kanisani ,jipe moyo utashinda...

MUHUBIRI:3
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa
Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka;
Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza
Wakati wa vita, na wakati wa amani.
Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza
 
Kuwa na moyo wa uvumilivu na ujasiri kijana miujiza inatendeka kila siku.
 
Upo sahihi kabisa. Ukitaka kumshukuru Mungu tizama walio chini yako either kwa kipato, afya matatizo nk lazima utajikuta unamshukuru Mungu na kupata nguvu mpya
Kuna mtu anaumwa muda huu, hana kitu na familia inamtegemea yeye.. Hii changamoto ni kubwa sana
 
Wanaume tumeumbiwa mateso.

Hata mimi bro kipindi kovid inaingia kibarua kiliota. Hadi mke alinikimbia kwa msoto niliopitia.

Ila sasahivi MOMENTUM naanza kurudi kwenye rait traki.

Usikate tamaa pambana.

Oneday utarudi kusoma huu uzi wako kisha utajicheka.
Jifunze boda boda ingia road
 
Haupo mwenyewe tupo wengi... Nimetafuta connection hadi na ibilisi sijapata
 
Jamani natafuta kazi ya kupika ,mie najua kupika saana,mtu yeyote anataka mpishi anicheki,mshahara uanzie laki na 80 asanteni
 
Huo utakatifu wako ulipewa au umejipachika tu, usije ukawa umejitaftia gundu mwenyewe.
Labda upo kwenye stage ya ku prove imani yako.
 
Back
Top Bottom