Nahisi niliuziwa machungwa yaliyoivishwa kwa kekimikali zilizoanza kutumika Mbeya kuivisha matunda, Mungu atusaidie lakini Idara zetu zimelala mno

Nahisi niliuziwa machungwa yaliyoivishwa kwa kekimikali zilizoanza kutumika Mbeya kuivisha matunda, Mungu atusaidie lakini Idara zetu zimelala mno

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
N:B: Sina uhakika wa asilimia 100 kama niliuziwa chungwa lililoivishwa kikemikali ila kwa dokezo >> hili << nimepata wasiwasi

Nipo Mbeya kwa wiki kadhaa, Nilikuja na mashine yangu ya kusagia juisi ya machungwa, Napenda sana kunywa juisi hii.

Wiki iliyopita nilizinguka soko la soweto nilikuta machungwa mengi yameharibika nikaambiwa msimu ndio unaisha, Ilikuwa ni mida ya saa moja jioni nikaenda soko pale kabwe, machungwa yalikuwa bei sana shilingi 500, nikawa natafuta nafuu nikaona kuna binti anauza machungwa kwa bei rahisi shilingi 300.

Nikafurahi sana nikachukua matano, Nikafika kwenye makazi yangu nikasaga kuandaa juisi bila kutia maji yoyote yani iwe juisi asilimia 100.

Vile nimeshaandaa naanza kuinywa, juisi ilikuwa inanichoma kwenye lips lakini ikifika kwenye ulimi haina shida.

Ilibidi niongeze maji ikawa hainichomi lips.

Leo hii nimeona dokezo kuna mchunguzi huru kaweka ushahidi wa kutosha kwamba kuna kemikali za Calcium Carbide na Etefon 480 zinanunuliwa kwa njia zisizo halali kutoka Zambia zinaletwa Mbeya zinatumika na wafanyabiashara wasio waaminifu kuivisha ndizi na maparachichi, kwa kilichonikuta nimeona itakuwa inatumika mpaka kwenye machungwa.


1729941631940.png


 
Taasisi zimelala mnooo. Kuna watu waliripoti issue za ndizi za kemikali. Lkn sijaona wametoa taarifa kukanusha ama kusema hata wanafanya uchunguzi. Kweli fisiemu ni janga kwa watz
Tz sio nchi ya kula vyakula matunda ya kuivishwa na kemikali hatujafika huko
Magonjwa yamekuwa mengi figo kisukari presha inni janabi kila siku anatangaza number zinaongezeka za wagonjwa..........

Lkn ............kimya
 
Dunia imetawaliwa na pesa, ata anayetengeneza mabomu anategemea apate wateja wengi ili salio lisome.
Nyakati hizi ni jitihada za mtu binafsi kuamua ale nini asile nini ili asipate madhara.​
 
Zimelala mnooo. Kuna watu waliripoti issue za ndizi za kemikali. Lkn sijaona wametoa taarifa kukanusha ama kusema hata wanafanya uchunguzi. Kweli fisiemu ni janga kwa watz
Walitoa ripoti kuwa kemikali hizo, hazina madhara kea watumiaji,.., nadhani kwenye moja ya uzi hapa jamii forum walipost barua official kutoka kwenye mamlaka,....😞😞
 
Mimi kwenye begi langu siku hizi natembea na maziwa kila nikimaliza kula nashushia
Nimeanza kuona umuhimu wa kufuga ng'ombe nyumbani hata kama haingizi faida, ni asset kubwa sana kiafya kwa zama hizi, maziwa ya viwandani na mitaani nayo yameingiliwa
 
Mimi nashindwa kuelewa , kwani Tunda kama parachichi , likikaa lenyewe si Lina iva TU

Sasa kuna haja gani ya kuingia gharana kununua kemikali Kwa ajili ya kuivisha.

Naomba muongozo, sijaelewa kabisa
 
Mimi nashindwa kuelewa , kwani Tunda kama parachichi , likikaa lenyewe si Lina iva TU

Sasa kuna haja gani ya kuingia gharana kununua kemikali Kwa ajili ya kuivisha.

Naomba muongozo, sijaelewa kabisa
Yakiiva haraka wanapiga pesa nyingi zaidi
 
Nimeanza kuona umuhimu wa kufuga ng'ombe nyumbani hata kama haingizi faida, ni asset kubwa sana kiafya kwa zama hizi, maziwa ya viwandani na mitaani nayo yameingiliwa
Shida zote hili kutumia vitu natural wewe na mimi ambae sipati shida ya kufuga ng'ombe tutatofautiana nini
 
Kunyweni soda na juisi za viwandani angalau Zina uthibiti, acheni kujifanya wajuaji..... hakuna kitu kinachoitwa 'natural' kwa sasa.
 
Mimi nashindwa kuelewa , kwani Tunda kama parachichi , likikaa lenyewe si Lina iva TU

Sasa kuna haja gani ya kuingia gharana kununua kemikali Kwa ajili ya kuivisha.

Naomba muongozo, sijaelewa kabisa
Watu wanataka yaive haraka, wapige pesa haraka.
 
Back
Top Bottom