Nahitaji kupungua uzito


kama ulefu ulio taja ni feet na si inches, kwa kutumia BMI kwa uzito wako wa 92kg wewe una uzito ulio pitiliza na bado kidogo uingie kwenye obesity!. (BMI yako ni 29.4) kwakweli unahitaji kupunguza uzito.
 
Kuacha/kupunguza vyakula vyenye mafuta kama chipsi, vyenye sukari kama soda na bia. Mazoezi jogging, kuruka kamba at least 30min kwa siku 4 hadi 5 za wiki.
 

Nadhani nakuelewa sasa, mm pia ni group O+, na niligundua maji yananisaidia,naomba nieleweshe zaidi
 
Karbu nikupe product za mimea na matunda hazina madhara yoyote .zisipo kusaidia hela yako inaludi 0683109166
 
Aisee we bonge sana. Anyway punguza au acha kunywa chai na vitu vya sukari sukari sana. Acha vyakula vyenye wanga na mafuta (chips, mayai, nyama, wali, dona). Ukila kula kidogo sana. Kula vyakula vya asili mf ugali ulokobolewa n.k

ale nini sasa mbona naona ndiyo unapotosha eti ale ugali uliokobolewa...
 
ale nini sasa mbona naona ndiyo unapotosha eti ale ugali uliokobolewa...

Ugali ulokobolewa ni makapi tu mkuu hauna chochote interms of nutrients na kama ipo ni kidogo sana. Kwahiyo hauwez kumuathiri kwenye dhamira yake ya kupunguza uzito.

Dona au wali ni janga kwake akipenda kula kila siku. Uzito hautapungua hata siku moja.
 

This is very wrong my dear friend... Kinyume chake ndio sahihi... Anapaswa kula whole grain meals.. Vyakula ambavyo havijakobolewa... Ila portion sizes control ni muhimu ili energy input iwe ndogo kuliko energy output ili apungue
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…