Nahitaji kusoma MUHAS au UDSM

hauzeeee45

Member
Joined
Jul 3, 2024
Posts
23
Reaction score
71
Kama uzi unavyosema hapo nimemaliza Diploma ya NURSING AND MIDWIFERY Ufaulu GPA 4.8

Nina malengo ya kusoma MUHAS AU UDSM, nimejaribu kupitia guidebook nimeona kuna course naweza kuapply kupitia course yangu ndugu zangu hvi naweza kupata nafasi pale kwa huo ufaulu

Pia naona admision capacity 5, nauliza pia ina maana wanachukua watu wa 5 kwa mwaka waliomaliza Diploma au zile mbwembwe tu pale?
 
Ya katavi au ostabey
 
Umesoma chuo gani hicho hadi uwe na overall gpa ya 4.8?
 
Wataangalia matokeo yako ya kidato cha 4 na 6 ulifanyaje. Kisha watarudi kuangalia chuo ulichopata hiyo Gpa ya 4.8 .
Kumbuka muhas na udsm huwa wanachukua wanafunzi kutoka diploma wachache sana yaani sana.
Mfano upande wa afya MD hawafiki hata 10
 
Hata ungekua wewe ndio mkuu wa chuo, assume una nafasi na una watu wawili wanaomba.

Wa kwanza ana div 1 ya 4 ya fom 6 pcb.

Wa pili ana gpa ya 4.8 diploma.

Je ungempa nani nafasi? Jijibu mwenyewe.

Form ni ngumu ila ina value kuliko diploma linapokuja swala la kuomba chuo kikuu/degree.
 
Kwa muhas unaweza ku apply kusoma bachelor of science in nursing, bachelor of science in midwifery, bachelor of science in nursing anaesthesia, physiotherapy, audiology, occupational therapy nahisi usipopenda mojawapo hapo bas hutak kusoma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…