Nahitaji ushauri wako kuhusu saratani ya damu

Nahitaji ushauri wako kuhusu saratani ya damu

hematological malignancy nyingi ni leukemia zinatibika na chemo, nenda ocean road watakupa ushauri mzuri zaidi
 
Mungu akuponye na uzima wa Mungu na pumzi ya Mungu iingie ndani yako. Hakuna kinacho shindikana kwake . amen
 
Ni upande wa kushoto unaweza hisi uvimbe kwa kujigusa au maumivu kwa mbali


HUWA NAHISI KAMA KUNACHOMA KWA MBALI KK,KUNA KIPINDI FULANI WALIVYONIAMBIA HIVYO NIMETUMIA SANA DAWA ZA KISWAHILI HALI ILITULIA KABISA LAKINI NAHISI IMEANZA TENA KWA MBALI....HUWA MIFUPA INAKUUMA PIA?
 
Wapendwa habari zenu.
Tatizo lenyewe ni kuwa ktk hali ya kupambana na Cancer ya Damu, ilikua 2014 mwanzoni nilipo anza kuhisi uvimbe tumboni ndipo nilipo amua kwenda Hosp na kufanya vipimo ambapo kwakweli majibu yalionyesha tu kuna uvimbe wa bandama na nilipewa tu vidonge vyakupunguza uvimbe.

Pia niliambiwa ukiendelea kuwepo basi watanipasua na kuitoa bandama jambo lililonipa wasiwasi sana,siku zikazidi kwenda uvimbe unaongezeka nilipo hosp nikaongezewa doze, baada ya kuanza kutumia vidonge na doze ikiwa imeongezwa afya ikaanza kudhoofika ndipo nilipo amua kuvuka mpaka na kwenda nchi ya jirani walipo gundua kuwa nina tatizo la Cancer ya Damu.

Nikaanzishwa dawa ya kuua makali na cells za cancer ambazo bado naendelea kuzitumia. Ombi langu kwenu wapendwa najua ktk wingi wetu humu JF wapo watu wenye kujua zaidi juu ya tiba mbadala ambazo nimeskia kuwa zipo Ila kwakweli sizifahamu, pili niliwahi ambiwa kuwa Serikali husaidia matibabu ya Cancer kupitia kuchangia gharama au kutoa dawa lakini kwangu binafsi sijui wapi pakuanzia. Nimekuja kwenu naitaji ushauri kutoka kwenu.
Kansa za damu zips za aina nyingi. Je wewe walikuambia uliyo nayo inaitwa je? Nikijua hilo nitakupa ushauri zaidi.
 
Pole sana ndugu. Nipo hospitali moja hapa India, kuna mama kutoka Kenya anatibiwa cancer ya damu kwa kufanya born marrow transplant,alivyonieleza ni kwamba wanaua cell za cancer halafu baada
ya muda ndio wanaweka born marrow toka kwa donor, mtu mnayematch. Gharama zao ni kubwa,kiasi. Kama utapenda nitakupa contacts uulizie zaidi.
 
ukweli naujua ila siwez kukushauri i felt sad naomba kilamtu a google source of cancer ili ajue jins ya kuepuka tatizo maana baadh ya kansa hazina dawa na tuepuke usasa tukidhan ni ufahal sijui soseji baga piza magarita spain wine na nk we kula dona bamia tembele togwa mbege na nk utakua salama
 
Pole mkuu i wish ningekuwa najua zaid kukusaidia. Ila nitakushauri ule sana vegetables,kitungu swaumu,binzari,tikiti maji ni baadhi ya vitu ambavyo ukila vinaweza kupbamana na kansa hio pia madawa makali. Mungu akujalie upone haraka.
 
Pole sana ndugu. Nipo hospitali moja hapa India, kuna mama kutoka Kenya anatibiwa cancer ya damu kwa kufanya born marrow transplant,alivyonieleza ni kwamba wanaua cell za cancer halafu baada
ya muda ndio wanaweka born marrow toka kwa donor, mtu mnayematch. Gharama zao ni kubwa,kiasi. Kama utapenda nitakupa contacts uulizie zaidi.
Asante sana ndugu,nami pia nilishauriwa kufanya hivyo,nitafurahi ukinipa details zaidi na ni hosp ipi
 
Pole mkuu i wish ningekuwa najua zaid kukusaidia. Ila nitakushauri ule sana vegetables,kitungu swaumu,binzari,tikiti maji ni baadhi ya vitu ambavyo ukila vinaweza kupbamana na kansa hio pia madawa makali. Mungu akujalie upone haraka.
Thanks
 
Ukiwa unaendelea na matibabu yako, kila mara ukipata muda, chukua kitunguu swaumu kitwange au kikuangue ( kama vile unataka kupikia labda mboga), kisha kiweke kwenye kikombe, kisha chukua asali kijiko kimoja weka ndani ya kikombe chenye kitunguu swaumu, harafu kata limao nusu kamulia ndani ya mchanganyiko wa hiyo asali na kitunguu swaumu. Baada ya hapo chemsha maji weka ndani ya kikombe hicho. Kunywa kama chai. Kila siku upatapo muda ( hakikisha kwa siku unakunywa si chini ya siku mbili). Utashangaaaa! ...... Jitahidi kutumia na usiache dawa zako endelea nazo
Asante
 
Nimesahau kitu.....unatakiwa kunywa huo mchanganyiko asubuhi kabla hujala kitu na vitunguu swaumu viwe vingi uwezavyo na uvimeze usiviache kwenye kikombe (kwa hiyo nivema unywe huku unakologa ile umeze vyote). Baada ya hapo mchana unaweza kunywa wakati wowote.... Ukitumia baada ya mwezi mmoja uje PM uniambie unaendeleje.......ni tiba usidharau tafadhari
Hakika siwezi dharau nitafanya hivyo maana nilikua natumia kitunguu swaumu chenyewe ktk maji ya uvuguvugu ss nitachanganya na asali
 
Back
Top Bottom