nusuhela
JF-Expert Member
- Jan 26, 2014
- 5,915
- 7,210
Najua wengi tutasema ni "utapeli", wengine watasema ni upigaji.
Lakini naomba niwatoe hofu, hili ni wazo lenye kuleta manufaa endapo tutaweza kwenda sawa na makubaliano.
Hao watu 99 mimi nikiwa wa 100 tutafanya nini? Au ni wa kazi gani?
Ipo hivi, wazo langu ni kuwa na vikundi vitano ndani ya hao watu 100. Yaani kikundi kimoja kinakua na watu 20.
Je, laki moja ya nini kila mwezi ndani ya mwaka mmoja?
Hiyo laki moja kila mwezi kwa watu 100, tunapata mil 10. Hiyo milion 10, itakua inafungua mradi mmoja kwa kila mwezi ambao utakua ni mradi wa kikundi "A" ambao utasimamiwa na watu wote 100. Pia mwezi wa pili, unafunguliwa mradi wa kundi "B" ambao pia unakuwa chini ya watu wote kwanza.
Kwahiyo ndani ya miezi 5, tutakua tumeweza kuwa na miradi mitano inayosimamiwa na watu 100.
Plan yangu ni kuwa na miradi 10 ndani ya mwaka mmoja. Hivyo basi, tutatoa hizo laki laki kwa muda wa miezi 10. Baada ya hapo, kila kikundi kitakua na miradi miwili.
Nini fursa na hili wazo?
1. Tutaondokana na wimbi la kutegemea mshahara tu kutoka kwa waajiri wetu
2. Tutaweza kujifunza namna ya kusimamia na kuendesha miradi mbali mbali
3. Tutazalisha fursa za ajira kwa watu wengi maana miradi itakua endelevu na yenye kujizaa. Maana hatutaishia na miradi hiyo kumi tu
4. Kadri miradi itakavyokua inaongezeka, ndivyo ugawianaji wa faidi utakavyokua unazidi na kujikuta tunaachana na utumwa wa kutegemea ajira
5. Tutaweza kupata mikopo kutoka serikalini inayotolewa kwenye vikundi
Ikumbukwe, hii sio fursa ya kupata faida haraka haraka. Ila, kwa huko mbele, itakua na manufaa.
Kama itawezekana kupata watu wote hao, tutasajiri kikundi kwa kufuata sheria za nchi
Kama upo tayari na una uwezo wa kutoa laki kila mwezi ndani ya miezi 10, basi karibu pm au jiunge kwenye group la whatsap kupitia 100 special ili niweze kukusajiri kwa usajiri wa awali kabla hatujaanza vikao vya kukutana na kusajiri kikundi tayari kwa kuanza kuchangia.
Pia, hatutachangia hela yoyote kabla hatujasajiri wala kufahamiana kiundani na kuweka sawa masuala ya fedha. Na hatutachangia bila kujua tutaanzisha mradi gani na mchanganuo wake kwa mtaji huo wa mil 10. Maana yake ni nini hapa, maana yake ni kuwa, kila mwezi kutakua na kikao cha pamoja.
Karibuni sana
Lakini naomba niwatoe hofu, hili ni wazo lenye kuleta manufaa endapo tutaweza kwenda sawa na makubaliano.
Hao watu 99 mimi nikiwa wa 100 tutafanya nini? Au ni wa kazi gani?
Ipo hivi, wazo langu ni kuwa na vikundi vitano ndani ya hao watu 100. Yaani kikundi kimoja kinakua na watu 20.
Je, laki moja ya nini kila mwezi ndani ya mwaka mmoja?
Hiyo laki moja kila mwezi kwa watu 100, tunapata mil 10. Hiyo milion 10, itakua inafungua mradi mmoja kwa kila mwezi ambao utakua ni mradi wa kikundi "A" ambao utasimamiwa na watu wote 100. Pia mwezi wa pili, unafunguliwa mradi wa kundi "B" ambao pia unakuwa chini ya watu wote kwanza.
Kwahiyo ndani ya miezi 5, tutakua tumeweza kuwa na miradi mitano inayosimamiwa na watu 100.
Plan yangu ni kuwa na miradi 10 ndani ya mwaka mmoja. Hivyo basi, tutatoa hizo laki laki kwa muda wa miezi 10. Baada ya hapo, kila kikundi kitakua na miradi miwili.
Nini fursa na hili wazo?
1. Tutaondokana na wimbi la kutegemea mshahara tu kutoka kwa waajiri wetu
2. Tutaweza kujifunza namna ya kusimamia na kuendesha miradi mbali mbali
3. Tutazalisha fursa za ajira kwa watu wengi maana miradi itakua endelevu na yenye kujizaa. Maana hatutaishia na miradi hiyo kumi tu
4. Kadri miradi itakavyokua inaongezeka, ndivyo ugawianaji wa faidi utakavyokua unazidi na kujikuta tunaachana na utumwa wa kutegemea ajira
5. Tutaweza kupata mikopo kutoka serikalini inayotolewa kwenye vikundi
Ikumbukwe, hii sio fursa ya kupata faida haraka haraka. Ila, kwa huko mbele, itakua na manufaa.
Kama itawezekana kupata watu wote hao, tutasajiri kikundi kwa kufuata sheria za nchi
Kama upo tayari na una uwezo wa kutoa laki kila mwezi ndani ya miezi 10, basi karibu pm au jiunge kwenye group la whatsap kupitia 100 special ili niweze kukusajiri kwa usajiri wa awali kabla hatujaanza vikao vya kukutana na kusajiri kikundi tayari kwa kuanza kuchangia.
Pia, hatutachangia hela yoyote kabla hatujasajiri wala kufahamiana kiundani na kuweka sawa masuala ya fedha. Na hatutachangia bila kujua tutaanzisha mradi gani na mchanganuo wake kwa mtaji huo wa mil 10. Maana yake ni nini hapa, maana yake ni kuwa, kila mwezi kutakua na kikao cha pamoja.
Karibuni sana