Nahitaji wazo la biashara isiyohitaji usimamizi mkubwa

Nahitaji wazo la biashara isiyohitaji usimamizi mkubwa

Fazilijr

Member
Joined
May 12, 2022
Posts
21
Reaction score
19
Habari zenu ndugu zangu wana JF

Nilikuwa naomba msaada wa wazo la biashara ambayo haitohitaji management kubwa sana. Mimi niko nje ya nchi na nimeajiriwa sitaki kuacha kazi yangu right away. Nataka nianze na uwekezaji wa 50M kwa kuanza.

Ni biashara ipi ambayo unaweza fanya kwa kiasi hicho? Serious people unaweza piga what'sup number +225718765236 kwa maongezi zaidi. Piga what'sup tu kwa sababu niko nje ya nchi.

Nb: Kwa atakayekuwa na business plan or ideas nzuri. I will be more than happy kushirikiana naye kufanya kazi.
 
Habari zenu ndugu zangu wana JF nilikuwa naomba msaada wa wazo la biashara ambayo haito hitaji management kubwa sana...
Unataka kufanya biashara au unatafuta mbia wakifanya nae biashara au unataka kumfanya biashara sio kwa haraka hiyo ya kutoa number za simu
 
Unataka kufanya biashara au unatafuta mbia wakifanya nae biashara au unataka kumfanya biashara sio kwa haraka hiyo ya kutoa number za simu
Business phone number haikuwagi private ndugu yangu, natafuta ideas za biashara tu ndugu kuna watu wengine hawapendagi ku share ideas zao in public na nikiona business idea yako ina make sense why tusifanye kazi
remember kuna mtu anaweza kuwa na idea but anakosa capital why tusishirikiane?
 
Biashara isiyo hitaji usimamizi mkubwa sana ni kilimo cha miti ya mbao, njoo bongo land likizo nenda mufundi au njombe kodi hekari za kutosha tafuta kijana/vijana kwaajili ya usimamizi wa shamba lako.

Kodi shamba kwa miaka 10, panda miti ya mbao vijana ni kwaajili ya usimamizi. Pia wanunulie smart phone kwaajili ya mawasiliano na wewe. Taarifa za shamba lako picha n.k zita tumwa kupitia hizo simu

Malipo ya hao vijana yata kua yanaongezeka kadri kazi inavyo zidi kua kubwa miti ikiwa michanga kazi ina kua ndogo miti ikikua kuna kazi ya ku pruni na kufyeka nyasi ili miti isi zidiwe na nyasi itakosa afya.

Kwa ufupi ni hivyo baada ya miaka 10 una weza kuja kuvuna sii chini ya 700M kama faida, Kazi kwako.
 
Habari zenu ndugu zangu wana JF

Nilikuwa naomba msaada wa wazo la biashara ambayo haitohitaji management kubwa sana. Mimi niko nje ya nchi na nimeajiriwa sitaki kuacha kazi yangu right away. Nataka nianze na uwekezaji wa 50M kwa kuanza...
50M makadilio at least ya faida kwa mwezi unataka kuingiza tsh ngapi?
 
Biashara isiyo hitaji usimamizi mkubwa sana ni kilimo cha miti ya mbao, njoo bongo land likizo nenda mufundi au njombe kodi hekari za kutosha tafuta kijana/vijana kwaajili ya usimamizi wa shamba lako.

Kodi shamba kwa miaka 10, panda miti ya mbao vijana ni kwaajili ya usimamizi. Pia wanunulie smart phone kwaajili ya mawasiliano na wewe. Taarifa za shamba lako picha n.k zita tumwa kupitia hizo simu

Malipo ya hao vijana yata kua yanaongezeka kadri kazi inavyo zidi kua kubwa miti ikiwa michanga kazi ina kua ndogo miti ikikua kuna kazi ya ku pruni na kufyeka nyasi ili miti isi zidiwe na nyasi itakosa afya.

Kwa ufupi ni hivyo baada ya miaka 10 una weza kuja kuvuna sii chini ya 700M kama faida, Kazi kwako.
Motivation [emoji344]

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Yaani 50M ununue kiwanja pia, ujenge nyumba iliyo kamilika labda mikoani ila sio Dar.
50m unatoa nyumba ya vyumba vitatu vya kulala tena hapa hapa DSM.

Mie nina nyumba za kupangisha nyingi mjini na ninazijenga chini ya hiyo hela.

Kuna sehemu watu mnakosea ktk ujenzi. Nyumba ya kupanga haina mbwembwe nyingi kama hizi tunazoishi wenyewe. Mfano geti la nyumba yangu ya kuishi pamoja na kipaa cha kulifunika ilinicost mil 6 lakini nyumba za kupanga geti linagharimu laki 5 tu.

Milioni 50 unaweza jenga nyumba 2 za vyumba viwili vyenye sebule na jiko na ukazipangisha

Kiwanja sijaongelea kwa kuwa bei inategemea na sehemu

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
50m unatoa nyumba ya vyumba vitatu vya kulala tena hapa hapa DSM.

Mie nina nyumba za kupangisha nyingi mjini na ninazijenga chini ya hiyo hela.

Kuna sehemu watu mnakosea ktk ujenzi. Nyumba ya kupanga haina mbwembwe nyingi kama hizi tunazoishi wenyewe. Mfano geti la nyumba yangu ya kuishi pamoja na kipaa cha kulifunika ilinicost mil 6 lakini nyumba za kupanga geti linagharimu laki 5 tu.

Milioni 50 unaweza jenga nyumba 2 za vyumba viwili vyenye sebule na jiko na ukazipangisha

Kiwanja sijaongelea kwa kuwa bei inategemea na sehemu

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
Yaani ukitaka urudishe hiyo pesa yako kwa hapa mjini Dar kiwanja tu hata hiyo 50M ina weza isitoshe
sijazungumzia kuhusu kuanza ujenzi hapo.

Labda ukajenge nje ya mji ambako una weza kupata kiwanja kwa 20M au 10M kitu ambacho hata ukijenga nyumba hela yako ita chukua muda mrefu sana kurudi maana kodi ya chumba kimoja tu si dhani kama ita zidi 50k kwa maeneo ya nje ya mji.

Ndio maana na kwambia kuwekeza 50M kwenye nyumba za kupanga hapa mjini ni hasara waste of time mzee wangu ni bora kufanya kitu kingine tofauti na hiyo plani ya kujenga.

Kuwekeza kwenye nyumba ya kupanga hapa mjini ili ikulipe vizuri na kwa kipindi kifupi ina hitaji uwekezaji wa pesa kubwa kuzidi hiyo 50M sijui nimeeleweka kweli.
 
Kama uko serious, tafuta ardhi Kama ekari tatu maeneo yabayofaa pembezoni mwa jiji la Dar. Utalipata eneo kwa nusu ya hiyo pesa then fanya mpango uwekewe bicon za wizara ya ardhi then unajenga fence au kuepuka gharama unaweka Kona za matofali yaliyojengewa. Baada ya muda mfupi litakuwa na thamani kubwa saana unaweza kuliuza au kulitumia.
 
Yaani ukitaka urudishe hiyo pesa yako kwa hapa mjini Dar kiwanja tu hata hiyo 50M ina weza isitoshe
sijazungumzia kuhusu kuanza ujenzi hapo.

Labda ukajenge nje ya mji ambako una weza kupata kiwanja kwa 20M au 10M kitu ambacho hata ukijenga nyumba hela yako ita chukua muda mrefu sana kurudi maana kodi ya chumba kimoja tu si dhani kama ita zidi 50k kwa maeneo ya nje ya mji.

Ndio maana na kwambia kuwekeza 50M kwenye nyumba za kupanga hapa mjini ni hasara waste of time mzee wangu ni bora kufanya kitu kingine tofauti na hiyo plani ya kujenga.

Kuwekeza kwenye nyumba ya kupanga hapa mjini ili ikulipe vizuri na kwa kipindi kifupi ina hitaji uwekezaji wa pesa kubwa kuzidi hiyo 50M sijui nimeeleweka kweli.
Mie inanilipa kwa kweli na sijutii kuwa na nyumba za kupangisha. Nilianza na moja ila kwa sasa ninazo za kutosha na hela ya ujenzi inatoka humo humo kwenye kodi kwa sasa. Nafikiria siku moja nijenge kijiji kisha nyumba niziuze na nyingine nipangishe

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Kama uko serious, tafuta ardhi Kama ekari tatu maeneo yabayofaa pembezoni mwa jiji la Dar. Utalipata eneo kwa nusu ya hiyo pesa then fanya mpango uwekewe bicon za wizara ya ardhi then unajenga fence au kuepuka gharama unaweka Kona za matofali yaliyojengewa. Baada ya muda mfupi litakuwa na thamani kubwa saana unaweza kuliuza au kulitumia.
Wazo zuri pia naunga mkono

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Biashara ambayo haitaji usimamizi mkubwa ni nyumba za wapangaji.
Hata nyumba zinahitaji usimamizi ndugu usipokuwa mfuatiliaji na msimamizi utakuta kila siku milango inavunjwa,rangi zinachafuliwa.
Bila kusahau wapangaji wabishi kulipa kodi ambao wanarudi kulala kwa kuvizia usiku wa manane kisha saa kumi na moja alfajiri wanaamka na kutembea mbele.
Biashara ambayo haina usimamizi kwa kweli hakuna usimamizi ni lazima,labda kidogo kuwekeza kwenye hisa za makampuni na kuiweka hela kwenye fixed akaunti lakini shida yake faida yake ni kidogo mno
 
Back
Top Bottom