Naibu Spika Dkt. Tulia: Jesca Kishoa hii kauli yako either uifute, ofisi ya Spika haina taarifa ya wewe kuondolewa kwenye chama chako

Naibu Spika Dkt. Tulia: Jesca Kishoa hii kauli yako either uifute, ofisi ya Spika haina taarifa ya wewe kuondolewa kwenye chama chako

Ukiwa muongo unapaswa kuwa na kumbukumbu sana (Liars must have a good memory). Bibi Tulia anadaia hajapata barua kutoka Chadema inayoonesha kuwa wanawake 19 walioko bungeni, walifukuzwa uanachama. Anasema wangekua wamefukuzwa wasingepaswa kuwepo bungeni maana ni kinyume cha Katiba.

Sasa tumemsaidia kumkumbusha kwamba barua ilitumwa na ilipokelewa ofisi ya Spika tarehe 1/12/2020 tena kwa dispach. Pia nakala ilitumwa NEC na kupokelewa kwa diapatch siku hiyohiyo 1/12/2020 saa saa 7:12 mchana.

Kwa kuwa Tulia ametamla kwamba ikiwa akina Kishoa wamefukuzwa uanachama hawapaswi kuwepo bungeni, basi apitie mafaili hapo ofisini ataona barua ya Chadema iliyotumwa 1/12/2020 halafu afanye maamuzi kwa mujibu wa Katiba.
Baada ya hapo jopo la wanasheria wa Chadema liwaburuze mahakamani Bwana Ndugai na Bibi Tulia kwa kutumia rasilimali za umma kulipa mishahara, posho na marupurupu kwa watu wasio wabunge kwa miezi 6. Huu ni uhujumu uchumi.!





Comment


Share
 
Hata baada ya CAG kutogundua ubadhirifu wowote kuhusiana na fedha husika,Takukuru ilipewa jukumu la kuchunguza upya uhalali na matumizi ya fedha hizo ambazo zilikuwa zinachangwa kwa mujibu wa katiba ya Chadema,lakini Takukuru inaelekea waligonga mwamba,maanake wako kimya mpaka leo.

Hata ww boss wako anaweza tu kusema nakupa kazi na kila salary yako lazima unipe laki tano na akaandika kwenye mkataba kufanya ni halali while ni haramu
 
Kituko! Mhemiwa kishoa ni sawa na mtuhumiwa anaekiri kosa mahakamani kuwa nimeiba, na Mheshimiwa naibu spika naye ni sawa na hakimu anaemwambia mkosaji mwizi, usiseme nimeipa!

Hakuna shida yoyote, tuache wivu wa maendeleo, wale wamepata acha wale
 
Mimi naona bunge lote lingevunjwa tu! Ili mishahara na posho zao, serikali itumie kuwakopesha wajasiriamali, wakulima na wafanyakazi kwa riba ndogo!

Maana hata hao wabunge walio wengi wa ccm na wale wawili wa upinzani, wameingia humo bungeni kwa magumashi tu.
 
Huyo mbunge hajielewi, kawaida adhabu inapotolewa kinachofuatia ni utekelezaji, rufaa hukatwa ambapo huwa mtu anaendelea kutumikia adhabu yake, sasa kama hawa wabunge walivuliwa uanachama inamaana wamepoteza sifa ya kuendelea kukaa bungeni, kama itatokea washinde rufaa yao ndio watarudi bungeni kupitia chama chao.

Spika anajua hili kwani alishalifanya kwa wengine, Naibu spika nae anajua hili, ila wameamua kupindisha sheria makusudi kwa manufaa yao binafsi, unless otherwise tuambiwe kama Chadema hawakuandika barua kuijulisha ofisi ya Spika juu ya uamuzi wao wa kuwavua uanachama hao wabunge, jambo ambalo nitakuwa mgumu kuliamini.
Maskini!!!!!!!!, Betina anatafuta aibu tupu.
Tumeuona MKONO wa Mungu tulipokuwa tunapita katika bonde la uvuli wa mauti.
Nyakati za ubabe mbuzi zimekwisha na kwenda nae mkuu wa takataka hizo.
Bunge sio mali binafsi ya Spika wala aliyekalia au kukalishwa kwenye kiti hicho.
AMEN
 
Kosa lake nn? Unadhan kakurupuka? Au anaelewa in and out kuhusu kutokua na chama. Hivi mikutano ya kisiasa ikianza watasimama majukwaani kama wabunge wa chama gani? Na je watavaa sare za chama gani? 🤣🤣🤣🤣👇👇! Think about it
Mbunge hajielewi kabisa
 
Kishoa ushaambiwa huwa chama humo sepa !! Nchi hii ina vituko aisee..huwezi amini. Huyo mwingine na yeye aliyetolewa gelezani usiku wa manane kuwahi saa mbili asubuhi kuuapia Ubunge - katulia as if nothing illegal happened.
Ndugai ameharibu sn hii nchi
 
Mbunge Kishoa kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amelalamikia kunyimwa nafasi ya kufanya mikutano ya kisiasa kabla hajaondolewa kwenye chama chake. Naibu spika akalazimika kuingilia kwa kusema haihitaji kuwa naye bungeni kama hana chama cha Siasa kwani ni takwa la kuwemo bungeni.

"Mheshimiwa Naibu spika sitaki sana kubishana na kiti chako lakini niseme mimi ni miongoni mwa wahanga wakubwa sana wa suala hili la mikutano ya hadhara, nikiwa kama katibu mkuu wa Baraza la wanawake CHADEMA wakati huo kabla sijaondolewa kwenye chama changu...'' Alisema Kishoa

Spika alimkatisha na kusema, "Mheshimiwa Kishoa hii kauli yako either uifute, ofisi ya spika haina hiyo taarifa ya wewe kuondolewa kwenye chama chako, kama umeondolewa kwenye chama chako usingekuwa humu ndani kwa sababu wabunge waliokuwemo humu ndani wote wana vyama vya siasa ndivyo katiba yetu inavyosema na ndiyo katiba yetu inavyosema ile katiba hairuhusu mbunge ambae hana chama"

Kishoa: Mheshimiwa Spika hatujaondolewa kwenye chama, bado mimi ni mwanachama wa CHADEMA kwasababu tuko kwenye taratibu na tumekata rufaa na taratibu zinaendelea

Tulia: Mheshimiwa ngoja, waheshimiwa wabunge taarifa rasmi za Bunge ni kumbukumbu, umezungumza kabla ya sentesi yako ya sasakwamba kabla hujaondolewa kwenye chama chako, futa hiyo kauli kwanza halafu umalizie mchango wako kwasababu ndani ya bunge hili tutakuwa tunavunja katiba kama tutakuwa na wewe humu kama umeshaondolewa na chama chako

Kishoa: Mheshimiwa naibu spika nimefuta

Hoja ya Mbunge Jesca ilianzia kwenye haki ya kufanya mikutano ya kisiasa na kukumbana na miongozo mingi kutoka kwa wabunge wakimtaka afute kauli. Kishoa amesema nchi ikiongozwa kwa matamko badala ya katiba itapotea.

Akifafanua kuhusu mikutano ya vyama vya kisiasa, Naibu spika amesema mikutano hiyo ipo kwenye katiba za vyama vya siasa na hufanyika kwa vipindi na sio ya hadhara akitolea mfano mkutano mkuu wa CCM uttakaofata utafanyika JK Convection centre na huo ndio unaitwa mkutano wa CCM lakini Rais akienda mahali unakuwa mkutano wa Rais na si CCM.



MY TAKE:

Je, CHADEMA haijatarifu bunge kuhusu kuwavua uanachama Wabunge 19 wa CHADEMA?

Zaidi soma: John Mnyika amuumbua Spika kwa kutoa ushahidi wa Ofisi ya Spika kupokea barua ya CHADEMA kuwavua ubunge wanachama wake

That was a Freudian slip.

La uvundo halina ubani.
 
Mjue wale wameapa mbele ya spika, na tume ya uchaguzi ndio ilipeleka majina kwa spika,

Na wale wako bungeni ni kwa because sababu zilizotumika kuwavua uanachama hazina mashiko

Ni sawa na ambavyo Mbowe Aliamua kuwatoa wabunge wote bungeni kisa ni corona wakati bunge linaendelea
Ungefahamu kuwa hauna HOJA ungejipumzikia tu. Bahati mbaya buku 7 zinakuswaga.
 
Mbunge Kishoa kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) amelalamikia kunyimwa nafasi ya kufanya mikutano ya kisiasa kabla hajaondolewa kwenye chama chake. Naibu spika akalazimika kuingilia kwa kusema haihitaji kuwa naye bungeni kama hana chama cha Siasa kwani ni takwa la kuwemo bungeni.

"Mheshimiwa Naibu spika sitaki sana kubishana na kiti chako lakini niseme mimi ni miongoni mwa wahanga wakubwa sana wa suala hili la mikutano ya hadhara, nikiwa kama katibu mkuu wa Baraza la wanawake CHADEMA wakati huo kabla sijaondolewa kwenye chama changu...'' Alisema Kishoa

Spika alimkatisha na kusema, "Mheshimiwa Kishoa hii kauli yako either uifute, ofisi ya spika haina hiyo taarifa ya wewe kuondolewa kwenye chama chako, kama umeondolewa kwenye chama chako usingekuwa humu ndani kwa sababu wabunge waliokuwemo humu ndani wote wana vyama vya siasa ndivyo katiba yetu inavyosema na ndiyo katiba yetu inavyosema ile katiba hairuhusu mbunge ambae hana chama"

Kishoa: Mheshimiwa Spika hatujaondolewa kwenye chama, bado mimi ni mwanachama wa CHADEMA kwasababu tuko kwenye taratibu na tumekata rufaa na taratibu zinaendelea

Tulia: Mheshimiwa ngoja, waheshimiwa wabunge taarifa rasmi za Bunge ni kumbukumbu, umezungumza kabla ya sentesi yako ya sasakwamba kabla hujaondolewa kwenye chama chako, futa hiyo kauli kwanza halafu umalizie mchango wako kwasababu ndani ya bunge hili tutakuwa tunavunja katiba kama tutakuwa na wewe humu kama umeshaondolewa na chama chako

Kishoa: Mheshimiwa naibu spika nimefuta

Hoja ya Mbunge Jesca ilianzia kwenye haki ya kufanya mikutano ya kisiasa na kukumbana na miongozo mingi kutoka kwa wabunge wakimtaka afute kauli. Kishoa amesema nchi ikiongozwa kwa matamko badala ya katiba itapotea.

Akifafanua kuhusu mikutano ya vyama vya kisiasa, Naibu spika amesema mikutano hiyo ipo kwenye katiba za vyama vya siasa na hufanyika kwa vipindi na sio ya hadhara akitolea mfano mkutano mkuu wa CCM uttakaofata utafanyika JK Convection centre na huo ndio unaitwa mkutano wa CCM lakini Rais akienda mahali unakuwa mkutano wa Rais na si CCM.



MY TAKE:

Je, CHADEMA haijatarifu bunge kuhusu kuwavua uanachama Wabunge 19 wa CHADEMA?

Zaidi soma: John Mnyika amuumbua Spika kwa kutoa ushahidi wa Ofisi ya Spika kupokea barua ya CHADEMA kuwavua ubunge wanachama wake

Wakati Katiba inaongelea uhuru wa kukutana, sio vikao tu, bali hata mikutano ya hadhara, sheria ya vyama vya siasa inafafanua kwamba vyama vina haki ya kufanya mikutano ya hadhara, maandamano, na kuipinga serikali iliyoko madarakani.

Sasa Naibu Spika anapopotosha makusudi, ana maanisha kusema nini haswa? Ni AIBU kubwabkwa mwanasheria wa kiwango chake kupotosha taifa na kulidanganya bunge mchana kweupe.

Na kwa hili suala la wabunge 19 wa "Changamoto ya upumuaji" a.k.a. covid-19, Inajulikana wazi kwamba hao wapo bungeni kwa mgongo wa Magu, aliyemwamrisha Spika. Ndugai peke yake asingemudu kuipika hiyo pilau. Swali ni je, Tulia anataka kusema ule mgongo wa Magu ume eksipaya?
 
Back
Top Bottom