Naibu Spika wa Bunge Musa Zungu alaumu tozo kukataliwa. Wananchi, makampuni ya simu na benki zahusishwa

Naibu Spika wa Bunge Musa Zungu alaumu tozo kukataliwa. Wananchi, makampuni ya simu na benki zahusishwa

Benki wanakata sababu Kuna huduma wanaotoa Kwa mteja kutunza na kuhamisha pesa.

Serikali Kuna nn imefanya istahili Kutoza tozo kwenye transaction ya mtu aliekatwa Kodi ya vat tayar???
 
Huo mshahara tunaouweka benki tayari serikali ameshachukua mgao wake. Hizo pesa ambazo benki anakata kufidia gharama za kukutunzia pesa zako, serikali itapata mgao wake. Nikitoa pesa ili nikanunue kitu, serikali ina mgao wake. Sasa huyu anaionea wivu benki ambayo inatoa huduma wakati tunalipa kodi serikalini ili ijenge hayo madarasa!

Na mbaya zaidi serikali inachukua mikopo kwa ajili ya kutoa huduma, mikopo ambayo italipwa na hao hao wananchi. Au yeye kwa sababu halipi kodi haoni maumivu ya wananchi? Kwa nini asidai yeye na wenzake wawe wanalipa kodi ili kuwapungunzia mzigo wananchi ambao ndio wanaomlipa mshahara na marupurupu mengine?

Amandla...
Mzee kama fidia ya kukuwekea pesa yako, monthly bank Charges za nini tena si wakate charges zao kwenye miamala tu?? Umewaza kindezi kinyama.
 
uyu kweli hana akili japokuwa mtu mzima je pesa inayochukua benki haina vat haikatwi kodi je pesa iyo ambayo ni kodi je haijengi madarasa hawa watu wanafikiri kutumia nini hawa [emoji24]
Watu kama hawa tuna takiwa kumuomba Mungu awapumzishe kwa atakavyo ona inafaa.
Watu tuna lalamika serikali ina fanya double taxation yeye ana angalia makato ya mara moja ya provider. Amesha sahau hata hizo bank au simu wanazo chukua kwetu pia wao serikali wana pata huko tena kodi zao. ?? Nyumbu hawezi kuwa nyati.
 
Mwanangu Mpendwa Mwigulu,hoja ya Kaka yangu Mpendwa Zungu muende mkaitizame wewe na timu yako wizarani.

Anaanzaga hivi, halafu naibu spika aliliongelea hili la tozo vizuri hivo mwanangu mwigulu mkakae na wataalamu wako mlitizame vizuri na hili jengine kama litawashinda mtuletee serikalini,
 
"Wananchi wengi wanalalamikia kodi iliyowekwa na Serikali, hawatizami mapato yanayokatwa na benki, hawatizami mapato yanayokatwa na kampuni za simu. Lazima iwe regulated [idhibitiwe].”

"Benki unatuma pesa wanachukua pesa nyingi zaidi ya Serikali kwa asilimia kubwa sana, lakini Serikali inayojenga madarasa ndiyo inalaumiwa. Kwa hiyo kuna kizingiti ambacho kinatengenezwa kuipiga dongo Serikali wakati pesa wanachukua watu wengine."

-Naibu Spika Mussa Zungu.
Uyu nae aendezake HUKO ,yeye anafikili kipato Chake na wananchi wa kawaida ni sawa, ? Huyu Mzee vipi au sio mtanzania nini? That's anaitwa zungu, anajiona amefika kupata unaibu wa mchongo
 
Mzee kama fidia ya kukuwekea pesa yako, monthly bank Charges za nini tena si wakate charges zao kwenye miamala tu?? Umewaza kindezi kinyama.
Na wewe unaona gharama zao ni hizo tu za kukutunzia pesa yako ty? Uzuri ni kuwa ukiona wanazengua una haki ya kuhama benki lakini hauna uwezo wa kusema mshahara wako upokee pesa taslimu kama ilivyokuwa zamani.

Amandla...
 
Anaanzaga hivi, halafu naibu spika aliliongelea hili la tozo vizuri hivo mwanangu mwigulu mkakae na wataalamu wako mlitizame vizuri na hili jengine kama litawashinda mtuletee serikalini,
Oya kweli Mkuu 🤣🤣🤣🤣
 
Hivi naibu spika anakatwa tozo/kulipa kodi?

Ova
 
Back
Top Bottom