Naibu Waziri Hamad Chande akumbushia usimamizi wa fedha zinazotolewa kwa ajili ya kusimamia Maadiliko ya Tabianchi

Naibu Waziri Hamad Chande akumbushia usimamizi wa fedha zinazotolewa kwa ajili ya kusimamia Maadiliko ya Tabianchi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Wataalamu wa mazingira kutoka Nchi 10 za Afrika na wenzao kutoka mataifa ya Ulaya wamekutana Jijini Arusha kujadili namna bora ya uwajibikaji kwenye matumizi ya fedha zinazotolewa na Wahisani kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya utunzaji mazingira ikiwemo mabadiliko ya Tabianchi.

Mkutano huo wa Kimataifa wa Uwazi na Uwajibikaji (International Transparency and Accountability Conference - ITAC) umefatika Septemba 28 na 29, 2023 ukiwa na lengo la kutoa elimu na kuibuka utatuzi wa changamoto za mazingira unatarajiwa kushirikisha Wadau 300 kutoka Nchi sita.

Akizungumza na Wadau mbalimbali walioshiriki kwenye mkutano huo hilo, Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Hassan Chande amesema:

“Tanzania kwa sasa ipo katika kiwango kizuri jinsi inavyoshirikiana na taasisi mbalimbali juu ya kupambana na mabadiliko ya Tabianchi.”

Ameongeza kuwa “Madhara ya Tabianchi tunayaona kama hakuna usimamizi mzuri wa fedha na kuwajibika katika kupambana na Mabadiliko ya Tabianchi.”

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya WAJIBU, Ludovic Utoah amesema utaratibu wa kushughulikia maafa sio mkubwa, ili tufanikiwe tunahitaji fedha na hizo fedha zinapotikana basi zitumike kama ilivyopangwa, kwa uwazi na uwajibikaji.”

Video: Azam TV
 
Back
Top Bottom