Naibu Waziri: Poleni Wakazi wa Kitunda kwa changamoto ya umeme, kuna hitilafu zinazojitokeza katika Miundombinu

Naibu Waziri: Poleni Wakazi wa Kitunda kwa changamoto ya umeme, kuna hitilafu zinazojitokeza katika Miundombinu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-11-04 at 13.49.46_20ef25ac.jpg
Muda mfupi baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kulalamika kuwa Mtaa wa Kitunda - Machimbo kuna kero ya Umeme kuwa unakatika zaidi ya mara tatu kwa siku, Serikali imetoa ufafanuzi na kuwapa pole Wananchi wanaopitia kadhia hiyo.

Mwanachama huyo alidai Wananchi wanapata wakati mgumu ikiwemo hasara katika biashara zao wakati upande wa pili, Kitunda Center wao hawana shida ya umeme na kwamba wakipiga Simu wanaambiwa “Umeme utarejea katika hali ya kawaida baada ya muda.”

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amejibu kwa kusema: Nimpe pole Mdau na Wananchi wa Kitunda kwa changamoto hiyo.

“Kukatika kwa umeme kitunda kunatokana na hitilafu zinazojitokeza katika miundombinu lakini pia laini ya umeme inayolisha Kitunda imetembea na laini nyingine 2 kwenye nguzo moja, hivyo kunapotokea hitilafu kwenye laini moja inaathiri laini zote 3.”

“Kwa sasa tunajenga line kutokea kituo kidogo cha kupoza umeme cha Gongolamboto ili kuweza kutenganisha line hizi 3, Laini hii inatarajiwa kuwashwa hivi karibuni hivyo itasaidia sana kupunguza tatizo.”

Kusoma hoja ya Mdau, bofya hapa ~ Mtaa wa Kitunda - Machimbo tuna kero ya umeme, unakatika zaidi ya mara tatu kwa siku, TANESCO hawatupi majibu ya kueleweka
WhatsApp Image 2024-11-04 at 13.49.46_7b3545c5.jpg
 
Uungwana. Huyu mmatengo wampe uwaziri. Naona anajitahidi kuwa karibu na wananchi na kuwapa faraja.
 
Back
Top Bottom