Naibu Waziri Viwanda ataka wahitimu waache kulalamika, wajiajiri

Naibu Waziri Viwanda ataka wahitimu waache kulalamika, wajiajiri

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Naibu Waziri Exauds Kigahe amewataka Wahitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kutumia elimu waliyoipata kujiajiri ikiwemo kuanzisha biashara badala ya kuwa sehemu ya kulalamikia ukosefu wa ajira.

Amesema “Ni jukumu la kila mhitimu kuukubali na kuuchangamkia zaidi msukumo wa Sayansi na Teknologia kuliko misukumo mingine iliyozagaa kwenye mitandao ya kijamii".

Kwa mujibu wa taarifa ya Sekretarieti ya Ajira ya Desemba 17, 2018, maombi ya Ajira Serikalini kati ya Novemba 2015 na Desemba 2018 yalikuwa 594,300, lakini waliopata kazi ni watu 6,554.

======================

Wahitimu wa kada mbalimbali wametakiwa kutumia elimu waliyoipata kujiajiri ikiwemo kuanzisha biashara badala ya kuwa sehemu ya kulalamikia ukosefu wa ajira.

Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Exauds Kigahe amesema badala ya kulalamikia ajira wahitimu hao wakawe suluhisho la ukosefu wa ajira kwa kuwa wabunifu na kuajiri Watanzania wengine.

Akizungumza leo Jumamosi Novemba 26, 2022 katika mahafali ya 57 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) na ya 15 kwa Kampasi ya Mwanza, Naibu Waziri huyo amewataka pia wahitimu kuchangamkia msukumo wa sayansi na teknolojia ili kuleta maendeleo yao binafsi na ya nchi.

“Ni jukumu la kila mhitimu kuukubali na kuuchangamkia zaidi msukumo wa sayansi na teknologia kuliko misukumo mingine iliyozagaa kwenye mitandao ya kijamii.

“Ikumbukwe maendeleo hayaji kwa lele mama, bali kwa mchakato unaohitaji kujitoa, kujinyima kwa faida ya kesho na kila mmoja anafaa akumbuke methali isemayo ‘mchumia juani, hulia kivulini,” amesema Kigahe.

Amepongeza uongozi wa CBE kampasi ya Mwanza kwa usimamizi mzuri wa mapato ya ndani, akisema yamewezesha kuwaendeleza watumishi kielimu, kuboresha miundo mbinu ya ufundishaji, kuanzisha program mpya za chuo, kuandaa mitaala atamizi za biashara na kuanzisha mafunzo ya uanagenzi.

MWANANCHI

RECAP:

Rais Samia Suluhu Hassan, alipozungumza na vijana jijini Mwanza Juni 15, 2021, aliweka wazi kuwapo upungufu mkubwa wa vijana walioko kwenye ajira, ilhali uwezekano wa kuongezeka bado uko gizani.

Kwa mujibu wa Rais Samia, hadi sasa Tanzania kuna jumla ya vijana milioni 20.7 wenye umri kati ya miaka 15 na 35, lakini ndani ya kundi hilo, asilimia 11.4 ya wenye sifa za kuajiriwa, hawako kazini.
 
Graduates tokeni daslam acheni kuona aibu, zama vijijini na mijini, fursa yoyote itakayoibuka mbele yako deal nayo, tumia elimu yako kufanya mambo yako yawe ya kipekee.

mkuu mpwayungu village, ulisema waweke tai chini waingie shamba!
naongezea: weka vyeti vyako chini, ingia mtaani..

ndg zangu, ajira hazipo, hazipo, hazipo na huu ndio ukweli ambao wenzenu tuliujua tangu hapo zamani.
 
Graduates tokeni daslam acheni kuona aibu, zama vijijini na mijini, fursa yoyote itakayoibuka mbele yako deal nayo, tumia elimu yako kufanya mambo yako yawe ya kipekee.

mkuu mpwayungu village, ulisema waweke tai chini waingie shamba!
naongezea: weka vyeti vyako chini, ingia mtaani..

ndg zangu, ajira hazipo, hazipo, hazipo na huu ndio ukweli ambao wenzenu tuliujua tangu hapo zamani.

Wanayoyasema haya wengi wao WAMEAJIRIWA..

#YNWA
 
Yuko sahihi..ajira za serikali sio tena kimbilio.

#MaendeleoHayanaChama
 
ndg zangu, ajira hazipo, hazipo, hazipo na huu ndio ukweli ambao wenzenu tuliujua tangu hapo zamani.
Ajira zipo ila sio Serikalini huko kumejaa wazee ambao hawataki kuachia viti na wanapeana viti wao, ndugu zao na watoto wao (nepotism haijawahi kuisha), km huna connection rudi bush ukalime mtoto wa mkulima na km wewe mtoto wa mchungaji nenda ukachunge ng'ombe na mbuzi
 
Naona amemsikia PM huko kwao vijana waliojiajiri kwa ujenzi na kupata tenda

Kwa kweli wanaweza maana wamesoma kila kitu ila nafikiri mpaka wanashindwa kuomba mikopo na kujiajiri basi vyeti vyao ni makaratasi na walikariri ila kwa vitendo hawawezi

Nasema hivyo kwa sababu mbona wengi wanashindwa kuamua moja la kujiajiri?
Wengi wanasubiri ajira miaka na wanatusumbua kuomba omba
Lini tutapata wavumbuzi na kuwa na bidhaa zetu wenyewe hata kuwauzia jirani?
 
Naibu Waziri Exauds Kigahe amewataka Wahitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kutumia elimu waliyoipata kujiajiri ikiwemo kuanzisha biashara badala ya kuwa sehemu ya kulalamikia ukosefu wa ajira.
Kulewa madaraka
 
Wanayoyasema haya wengi wao WAMEAJIRIWA..

#YNWA
Wanasema wanayoyaona huko ndani.
kama kulima, kalime~ kisomi

kama kufuga kafuge~ kisomi

biashara kafanye~ kisomi.

baada ya hapo utaanza kuwaonea huruma walioajiriwa na kuona wako utumwani.
 
Naibu Waziri Exauds Kigahe amewataka Wahitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kutumia elimu waliyoipata kujiajiri ikiwemo kuanzisha biashara badala ya kuwa sehemu ya kulalamikia ukosefu wa ajira.

Amesema “Ni jukumu la kila mhitimu kuukubali na kuuchangamkia zaidi msukumo wa Sayansi na Teknologia kuliko misukumo mingine iliyozagaa kwenye mitandao ya kijamii".

Kwa mujibu wa taarifa ya Sekretarieti ya Ajira ya Desemba 17, 2018, maombi ya Ajira Serikalini kati ya Novemba 2015 na Desemba 2018 yalikuwa 594,300, lakini waliopata kazi ni watu 6,554.

======================

Wahitimu wa kada mbalimbali wametakiwa kutumia elimu waliyoipata kujiajiri ikiwemo kuanzisha biashara badala ya kuwa sehemu ya kulalamikia ukosefu wa ajira.

Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Exauds Kigahe amesema badala ya kulalamikia ajira wahitimu hao wakawe suluhisho la ukosefu wa ajira kwa kuwa wabunifu na kuajiri Watanzania wengine.

Akizungumza leo Jumamosi Novemba 26, 2022 katika mahafali ya 57 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) na ya 15 kwa Kampasi ya Mwanza, Naibu Waziri huyo amewataka pia wahitimu kuchangamkia msukumo wa sayansi na teknolojia ili kuleta maendeleo yao binafsi na ya nchi.

“Ni jukumu la kila mhitimu kuukubali na kuuchangamkia zaidi msukumo wa sayansi na teknologia kuliko misukumo mingine iliyozagaa kwenye mitandao ya kijamii.

“Ikumbukwe maendeleo hayaji kwa lele mama, bali kwa mchakato unaohitaji kujitoa, kujinyima kwa faida ya kesho na kila mmoja anafaa akumbuke methali isemayo ‘mchumia juani, hulia kivulini,” amesema Kigahe.

Amepongeza uongozi wa CBE kampasi ya Mwanza kwa usimamizi mzuri wa mapato ya ndani, akisema yamewezesha kuwaendeleza watumishi kielimu, kuboresha miundo mbinu ya ufundishaji, kuanzisha program mpya za chuo, kuandaa mitaala atamizi za biashara na kuanzisha mafunzo ya uanagenzi.

MWANANCHI

RECAP:


Rais Samia Suluhu Hassan, alipozungumza na vijana jijini Mwanza Juni 15, 2021, aliweka wazi kuwapo upungufu mkubwa wa vijana walioko kwenye ajira, ilhali uwezekano wa kuongezeka bado uko gizani.

Kwa mujibu wa Rais Samia, hadi sasa Tanzania kuna jumla ya vijana milioni 20.7 wenye umri kati ya miaka 15 na 35, lakini ndani ya kundi hilo, asilimia 11.4 ya wenye sifa za kuajiriwa, hawako kazini.
Naunga mkono hoja,
Mimi kama kijana nlipomaliza masomo yangu 2020 ya Lab technician, nlijiajir na kuanza kutoa huduma nzuur Kwa patient.
Kwa ubora WA huduma nlipata wadau wengi WA client weng mno had baadh ya wadau WA afya KATIKA jamii hio kuanza kunifuatilia nmesoma wap na nimetoka wapi na nyuma yangu Kuna nani.
Anyway nlipata pesa kiasi nkanunua ka FANcargo kangu lainii(napenda kupush ndinga)
Kitu kingne nkajingiza kwenye viwanda vdogvdgo vya kutengeneza sabuni,( detergent) n.k
Of course nlipata pase.

Turudi kweye mada.
Nikwamba baada ya kupata vihela DLT WA wilaya hio akawa anafanya ukaguzi,
Na mwsho WA siku akaangukia Kwangu na nlikua na Go ahead letter ya kuendelea kutoa huduma kutoka kwake ila alinikataa na Kusema ni MAABARA bubu, ooh my god nilipata taabu na ikafika sehm nkapelekw kituoni kifupi nlizuiliwa na kupigwa faini ya 2M
Oooh baadae nkaja fanya uvhunguzi kumbe Kuna Dispensary moja pale kwenye hicho Kijiji, mwenyw ni mtumishi mkubwa pale wilayani na nilimpiga BAO sana japo mm ilkua ni Lab only..

So nkaacha na kurudisha vifaa hom kwanza nidicus niwap naenda kianza upya.
Nashukuru nlikua na biashara ya sabuni ndo iliniweka mjini had now.

Nachotaka Kusema ni kwamba Vijana tunapenda kijiajir lkn sera na ukandamizaji uliopo ni hatar Kwa Vijana hasa ukipata mafanikio kidogo tu.

Haohao wakubwa ndo wanaoziba fursa za Vijana na kuwaambia mjiajiri kama kitimiza wajibu tuu,

Sisi watoto WA maskini tujikaze tu Allah atatuona tu
 
Naibu Waziri Exauds Kigahe amewataka Wahitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kutumia elimu waliyoipata kujiajiri ikiwemo kuanzisha biashara badala ya kuwa sehemu ya kulalamikia ukosefu wa ajira.
Tuanze na yeye, amejiajiri au ameajiriwa?
Wanasiasa kuwaamini unatakiwa uwe na akili ndogo sana!
 
Ili mtu aweze kujiajiri; Serikali inatakiwa kufanya kazi 80 percent kutengeneza mazingira na mhitimu 20 percent. Ukiona watu wanashindwa kujiajiri fahamu kuwa serikali imeshindwa kutengeneza mazingira ya kujiajiri.
 
Naunga mkono hoja,
Mimi kama kijana nlipomaliza masomo yangu 2020 ya Lab technician, nlijiajir na kuanza kutoa huduma nzuur Kwa patient.
Kwa ubora WA huduma nlipata wadau wengi WA client weng mno had baadh ya wadau WA afya KATIKA jamii hio kuanza kunifuatilia nmesoma wap na nimetoka wapi na nyuma yangu Kuna nani.
Anyway nlipata pesa kiasi nkanunua ka FANcargo kangu lainii(napenda kupush ndinga)
Kitu kingne nkajingiza kwenye viwanda vdogvdgo vya kutengeneza sabuni,( detergent) n.k
Of course nlipata pase.

Turudi kweye mada.
Nikwamba baada ya kupata vihela DLT WA wilaya hio akawa anafanya ukaguzi,
Na mwsho WA siku akaangukia Kwangu na nlikua na Go ahead letter ya kuendelea kutoa huduma kutoka kwake ila alinikataa na Kusema ni MAABARA bubu, ooh my god nilipata taabu na ikafika sehm nkapelekw kituoni kifupi nlizuiliwa na kupigwa faini ya 2M
Oooh baadae nkaja fanya uvhunguzi kumbe Kuna Dispensary moja pale kwenye hicho Kijiji, mwenyw ni mtumishi mkubwa pale wilayani na nilimpiga BAO sana japo mm ilkua ni Lab only..

So nkaacha na kurudisha vifaa hom kwanza nidicus niwap naenda kianza upya.
Nashukuru nlikua na biashara ya sabuni ndo iliniweka mjini had now.

Nachotaka Kusema ni kwamba Vijana tunapenda kijiajir lkn sera na ukandamizaji uliopo ni hatar Kwa Vijana hasa ukipata mafanikio kidogo tu.

Haohao wakubwa ndo wanaoziba fursa za Vijana na kuwaambia mjiajiri kama kitimiza wajibu tuu,

Sisi watoto WA maskini tujikaze tu Allah atatuona tu
Hongera!! vijana hata kabla ya kukandamzwa, ni waoga kuthubutu
 
Sipendi kuwaambia vijana mambo ya kujiajiro wkt wao na watoto wao wamekali viti na kutoka hawataki.
 
Back
Top Bottom