TANZIA Naibu Waziri wa Elimu Mstaafu Mzee Nazar Nyoni afariki dunia

TANZIA Naibu Waziri wa Elimu Mstaafu Mzee Nazar Nyoni afariki dunia

Ofisi za Elimu mkoa zamani kwa chini ile road alikuwa anakaa hapo zamani.
Ubinafsi ulianza zamani sana,Ukifuatilia alijimikikisha hilo eneo,na watoto wake akaforce waingine kazini no matter what.Uzalendo umeanza kufa Zamani.
 
Naibu Waziri wa Elimu wa zamani wa Serikali ya Tanzania wa Awamu ya Kwanza, Mzee Nazar Nyoni, amefariki dunia jana tarehe 19/07/2024 majira ya saa 3 asubuhi nyumbani kwake Morogoro baada ya kuugua kwa muda mrefu. Mzee Nyoni amefariki akiwa na miaka 95.

Marehemu aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Elimu wa Tanzania kati ya mwaka 1975 hadi 1980 na ametoa mchango mkubwa katika sekta ya elimu nchini Tanzania. Alifanya kazi kwa karibu na serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Hayati Julius Nyerere.

Mazishi yatafanyika Jumatatu tarehe 22/07/2024 Kola, huko Morogoro.


Chanzo cha taarifa hii ni mwanafamilia. Tunatoa pole kwa familia, marafiki na wote walioguswa na msiba huu.
Ushimen sorry for the loss of your classmate
 
kabla sijatoa pole alikuwa ccm au chama gani niseme RIP
Inaelekea hujui kuwa kabla ya CCM kulikuwa na TANU na ASP ? Apumzike kwa amani Mzee Nyoni. Kila nikikumbuka viongozi wa awamu ya kwanza huwa naguswa sana na uzalendo na uadilifu wao na walivyokuwa wakiitwa NDUGU.
kabla sijatoa pole alikuwa ccm au chama gani niseme RIP
 
Inaelekea hujui kuwa kabla ya CCM kulikuwa na TANU na ASP ? Apumzike kwa amani Mzee Nyoni. Kila nikikumbuka viongozi wa awamu ya kwanza huwa naguswa sana na uzalendo na uadilifu wao na walivyokuwa wakiitwa NDUGU.
Kwa amani gani kaacha walimu na shule bado zipo vibaya yeye watoto wake wamesoma shule nzuri
 
Mkuu Ushimen , marehemu ni 95 ni classmate wako kweli au umekosea?, how old are you?.
P
Nilikua nakuona wakati unakua kwenye kotaz za polisi.

Nilikushudia ukiwa kijana miaka ya 90'z hadi unapata ajali na honda yako by da way.....
Ulikua kijana sana miaka ileee... na ulikua unajipena pia ulikua jasiri zaidi ya leo.
R.i.P ISP Mayala
 
Sio kila mtoto wa mkubwa, but watoto wa mawaziri karibu wote wa Nyerere walisoma hapo,
Primary yangu ni O/Bay tulikuwa na
Watoto wa Malecela akiwa VP II na PM mmoja darasa moja.
Watoto wa Kawawa,
Watoto wa Warioba
Watoto wa mawaziri karibu wote
Watoto wa waserikali karibu wote wakiwemo Watoto wa Jaji Mkuu, Nyalali mkewe ni mwalimu wetu, na Watoto wa Prof. Sarungi, Isaac Sepetu, na wakubwa serikalini enzi hizo.
Huyu Dr. Mwinyi alinitangulia madasa mawili Primary.
Mimi mwenyewe baba na mama walikuwa serikalini.

Sekondari nikaenda Tambaza huko nikasoma na mtoto mmoja wa kwa Nyerere pale Msasani, na mtoto wa Mkapa darasa moja, A level kulikuwa na Mtoto wa Malecela akipiga PCM, akaja binti Malecela form V akipiga PCB, darasa moja na Husein Mwinyi.

A Level nikaenda Ilboru, darasa moja na mtoto wa Warioba.

UDSM sheria nikakutana na Riz1.

Mtoto wa Mkapa alihamia US, hivyo nilipokwenda US, akaniconnect na Mshure wake.

One good thing about me na watoto wa wakubwa, nawaona ni watu wa kawaida sana, sijipendekezi kwao kutaka favours zozote kwa wazazi wao.

Nime interact na Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na Samia by virtue of my journalistic professional na sio kwasababu nimesoma na watoto wao na sijawahi ku lobby uteuzi kwa yeyote!.
P.
Mayala ulikuwa nyuma yangu hapo Oysterbay, ukikaa maflat mimi nikiishi miikoroshoni ya mwanzon kariba na maflati, ingawa sikukufahamu wakati nasoma hapo Obay ill classmate zako akina Mwinyi niliwafahamu labda kwa sababu ya majina ya baba zao wakati huo
 
Naibu Waziri wa Elimu wa zamani wa Serikali ya Tanzania wa Awamu ya Kwanza, Mzee Nazar Nyoni, amefariki dunia jana tarehe 19/07/2024 majira ya saa 3 asubuhi nyumbani kwake Morogoro baada ya kuugua kwa muda mrefu. Mzee Nyoni amefariki akiwa na miaka 92.

Marehemu aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Elimu wa Tanzania kati ya mwaka 1975 hadi 1980 na ametoa mchango mkubwa katika sekta ya elimu nchini Tanzania. Alifanya kazi kwa karibu na serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Hayati Julius Nyerere.

Mazishi yatafanyika Jumatatu tarehe 22/07/2024 Kola, huko Morogoro.


Chanzo cha taarifa hii ni mwanafamilia. Tunatoa pole kwa familia, marafiki na wote walioguswa na msiba huu.
Ok
 
Back
Top Bottom