Naingia kwenye kufuga kuku chotara (Saso)

Naingia kwenye kufuga kuku chotara (Saso)

KUHUSU hydroponic ni shule ndefu kidogo jitahidi kutafuta Uzi humu unaelezea vizuri Sana kuhusu hiyo.

Jambo moja ambalo Uzi zote haujaeleza ni kwamba hydroponic folder kwa ajili ya kuku ni vizuri isizidi siku nne ili iweze kumeng'enywa kirahisi na kuleta matokeo chanya katika afya ya kuku.

Pia hydroponic kwa ajili ya kuku lazima ichukue nafasi isiyozidi 40% ya chakula chote cha Kila siku ili kuleta uzalishaji wenye tija kwa kuku wa mayai na nyama.
Vip kuhusu azola
 
Mrejesho 1

Tarehe 26/04/2022 nilichukua box mbili za vifaranga vya sasso kutoka makota Iringa kila box lilikuwa na vifaranga 102 ivyo ikafanya idadi na kuwa 204

Maandalizi ni kama yafuatayo

1 Chakula (Nilitengeneza mm mwenyewe kama ifuatavyo)

starter inabid iwe na 20-18 % ya Digestible Crude Protein ( DCP) ili kufanya kifaranga kiote manyoya haraka ili kujikinga na baridi, Chakula hichi watakula kwa miezi miwili then nitabadilisha mfumo wa kuchanganya


Mahindi yalio balazwa 65 Kg
Mashudu yalio balazwa 22 kg
Uduvi ule mdogo wa langi ya red-silver 8 kg
Diphosphate calcium (DCP) 1 kg
Chokaa ya kuku 2.50 kg
Mifupa 1 kg
Chumvi ya jikon 500 g

Nilitengeneza 100 kg Kwa awamu ya kwanza lengo la kufanya ivyo ili chakula kisikae muda mlefu kikawa na Sumukuvu maana huwa inasababisha kuku kufa

Ili kupata Mahindi na mashudu yalio balazwa inabidi uende mashineni wanapo saga unga wa ugali then unamwambia yule operator atoe ile chekeche kwenye machine ya kusagia then akipitisha ayo Mahindi zinatokea chenga chenga ambazo kifaranga kitaweza kula vizuri

2 Jiko
Nilinunuwa Yale majiko special kwa ajili ya vifaranga yapo kama chungu ivi lkn kina matundu pembeni na mfuniko juu
Ivyo kama moto ukiwaka tayali nafunika juu na ule mfuniko ivyo joto linaweza kudumu kwa muda wa masaa 5-6 endapo ukifunika lkn ukiacha wazi 2-3 masaa tayali joto linapotea

3 Sehemu vifaranga vinapo shinda
Nilinunuwa magazeti kilo 3 na board moja, mbao ya 2 by 4 na mapumba ya mpunga ( rice husk )

Mapumba ya mpunga nilitandika chini ili kuzuia unyevu usipande juu na kunyonya maji endapo yakimwagika

Magazeti kwa ajili ya kutandika chini maana inabid utandike matabaka 3 ya magazeti then kila siku lile tabaka la juu unalitoa then unaweka lingine

Board kwa ajili ya kutengeneza round ili vifaranga wasife maana wanatabia ya kujikusanya kwenye Kona kwa pamoja ivyo ukutumia board sio lahisi kupata Kona

Mbao 2 by 4 izi ni kwa ajili ya kuunganisha board moja na nyingine ivyo nilizichana kidogo katikati ili kukutanisha board mbili na kutengeneza round

Eneo nililo tumia kwa hatua za mwanzo ni 1.5 m kwa 1.5 ili vifaranga wapate joto na muda mwingi watumie kula na kupumzika kuliko kutembea lkn baada ya week ya pili nitaongeza ukubwa wa eneo

4 Vyombo vya kulia
Nilinunuwa dinker 4 na feeder 6 Kwa awamu ya kwanza lkn kwa upande wa feeder natumia kile kisahani tuu

5 Mpangilio wa kimiminika ( Maji)

Ile siku nilio waleta ( hii siku sio siku ya kwanza maana siku inakuwa na masaa 24 ivyo inakuwa Zero day) niliwapa maji yenye mchanganyiko wa Glucose na Vitamin kwa masaa mawili kabla sija wapa chakula lengo la kufanya ivyo ni kuwapatia nguvu kutokana na uchovu wa safari na kufungua mfumo wa kumengenya chakula

Siku ya kwanza hadi ya Tano
Niliwapa maji yenye mchanganyiko wa Antibiotic lengo la kufanya ivyo nikukausha vitovu ili wasipate tatizo choo kuganda ( Constipation )

Siku ya sita ambayo ni Leo
Niliwapa maji ambayo ayana mchanganyiko wa kitu chochote kile

Siku ya Saba ambayo ni kesho
Nitawapa chakula then baada ya masaa manne nitawapa maji yenye mchanganyiko wa dawa ya kideli (Newcestle) kwa masaa mawili tuu then baada ya hapo nitawapa maji ya kawaida


Mafanikio

✓Hadi sasa akijafa ata kifaranga kimoja

✓Akuna kifaranga kilicho pata ulemavu

✓Asilimia 75 ya vifaranga mabawa Yao tayali yamefunikwa na manyoya ivyo inaonyesha chakula ni kizuri kwa hatua za mwanzo za ukuaji

✓Vifaranga vinakula sana mida ya asubuhi kuliko mchana ivyo inaonyesha afya Yao ni nzuri na mfumo wa umengenyaji umekaa vizuri

✓Akuna kifaranga aliye pata tatizo la choo kigumu


Changamoto

✓Kila baada ya masaa manne inabidi niwepo bandani ivyo inakuwa vigumu kufanya ivyo maana nakuwa nipo kwenye majukumu memgine kwaiyo inabid kila baada ya masaa sita ndio niwepo bandani

✓Kuamka usiku inakuwa ni tatizo maana sijazoea ivyo Kuna bahadhi ya siku huwa napitiliza hadi asubuhi

✓Vifaranga vinapendelea sana uduvi kuliko Mahindi na mashudu ivyo inabid nisubilie kwanza then ndio wanaanza kula Mahindi na mashudu


Mwisho

Mrejesho 2 nitauleta tena jumatatu ijayo Yani siku ya 13
View attachment 2208838View attachment 2208839View attachment 2208840
Hawa jamaa walienda wap mbn hawatuletei tena mrejesho au hali tete
 
Mwenye mayai ya sasso au kroiler nahitaji trey tatu ,!
NB: yasiwe na mda mrefu naitaji kutotoresha!!
 
Mrejesho nitaleta mapema tarehe za mwanzoni za mwezi huu. Majukumu ni mengi sana na muda ni mchache.

Tunaowapa nafasi ya kutusaidia wanakuwa sehemu ya kukwamisha mapambano.
 
Baada ya mvua za msimu huu kuwa za kusita na kupoteza mbegu kwa kupanda zaidi ya Mara mbili na kuungua na jua, huku nyanya nazo zikiwa zinachechemea, nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara Aina ya sasso wakati tunaendelea kusubiri neema ya mvua Kama itatuwezesha kuvuna.

Mpango ni kufikisha kuku 1000 na zaidi mpaka mwisho wa mwaka huu 2022.

Kwa Sasa nimeanza na kuku 25 (mitetea 20 na majogoo 5) ambao nimewanunua December 26 wakiwa na miezi miwili.

Malengo makuu ni kusubiri kuku wafike umri wa kutaga kuanzia march 2022 (wakiwa wamefikisha miezi 5) ili nitotoleshe mayai.

Kuku wakianza kutaga nategemea kupata wastani wa mayai 10 kwa siku (kwa uchache) sawa na mayai 100 Kila baada ya siku 10. Hii inamaana Kila baada ya siku 10 nitapeleka mayai 100 kutotolesha.

Baada ya siku 120 ambayo ni wastani wa miezi 4 kuanzia mwezi March sawa na mwezi July 22 nitakuwa nimetotolesha mayai 1200 ambayo kwa wastani nitapata vifaranga 1000 na kidogo (hayo mayai 200) naasume baadhi yatakuwa hayajatotoleshwa au vifaranga watakaoshindwa kuvuka nursery stage.

Kwahiyo mpaka inafika December 2022(insha_Allah) nitakuwa na kuku 1000 ambao ukiachana na parent 25 nilionza nao kutakua na wakubwa wenye miezi 6,5,4(watakua wameanza kutaga) size ya Kati na wadogo kabisa batch ya mwisho miezi miwili.

Baada ya kufikisha idadi hiyo nitaanza kuuza mayai au kutotolesha vifaranga kwa ajili kuuza au kwa ajili kufuga wa nyama.

KUHUSU GHARAMA
Kuku nimenunu 8000 Kila mmoja sawa na 200,000 kwa kuku wote.

Banda lilikuwepo linalowatosha kuku hao 25.

Kwa kuku watarajiwa Banda lao natarajia kuanza kuhangaika nalo baada ya kuku kuanza kutaga. Ambalo nitalijenga kwa awamu nne (Kila awamu nitakamilisha sehemu ya kuku 300) makisio ya gharama za ufundi kwa Banda la kisasala kuku 1000 na zaidi ambalo nimeandaa eneo la (20x10)m nimepata ni shilling 3.5M kwa materia ya eneo nililokuwepo.

KUHUSU CHAKULA
Kutokana nimewanunua wakiwa wakubwa nimetengeneza mchanganyiko wangu wa chakula ili kupunguza gharama. Ambapo gharama za debe moja(baada ya kuchanganya) ni chini ya 3000 na kuku wote 25 wanakula debe 1 na nusu kwa mwezi. Na nimeanza mchakato wa kutengeneza funza na hydroponic folders na baadae nitaandaa bwawa la azola.

Baada ya kufikisha kuku 1000 makadirio ya chakula kwa siku ni kilo 130 ambazo ni sawa kwa mchanganyo wangu wa chakula + hydroponic ni 500 kwa kilo. Sawa na sh 65,000 kwa siku

KUHUSU MATARAJIO YA FAIDA
kwa mwaka huu wote wa 2022 silengi kupata faida, nahitaji mradi ujisogeze na uwe stable. Kwa maana mpaka inafika December 2022 mradi uwe umerudisha gharama zangu japo kwa uchache na uwe inaweza kujiendesha kwa kuuza mayai au kuku.

Baadaya ya mwaka huu nategemea kupata faida Kama ifuatavyo.

1. Kwa kuwa natarajia kwenye kuku 1000 kuwe na mitetea isiyopungua 800 hivyo nategemea kukusanya mayai yasiopungua 510 kwa siku(kwa makadirio ya chini. Sawa na tray 17 kwa siku .

Tray 1ni sawa na tsh10,000 kwa mayai ya chotara (Bei za nilipo) sawa na tsh 170,000 kwa siku

NB: Mradi huu nitausimamia mwenyewe kwa asilimia 100 hivyo hakuta kuwa na gharama za ziada za mfanyakazi.

Hivyo ndivyo nitavyoiishi 2022.

Nakaribisha maoni.
Hujasema gharama za chanjo na dawa zingine,pia vipi kuhusu ubora Wa mchanganyiko wa chakula,pia ukusanyaji wa mayai Kwa siku kumi Ili uweze kutotolesha,ni mazingira yapi ya joto ya baridi au,je vipi gharama za kutotolesha na ubora Wa mayai na mashine ya kutotolesha,?
 
Hongera sana mkuu. Ni mawazo mazuri sana. Kwa kusimamia mwenyewe hakika utafanikisha malengo yako na Mungu wetu wa mbinguni akutangulie. Ulishawahi kufuga before? Mimi pia hadi sasa nafanya kama unachofanya, nimeanza mwaka jana September na maendeleo siyo haba. Mimi ninafuga almost ndege (Wafugwao) wote wanaopatikana mazingira ya Tz.

Sasa nina haya machache nadhani yanaweza kukufaa;
1. Kwa idadi ya hao matetea unaweza kukomaa ukatotolesha kwa kutumia kuku wenyewe (sina hakika kama sasso wanaatamia). Kwa maoni yangu ni bora kuliko mashine. Ndicho nachofanya. Nilishawauzia watu mashin sana kabla sijaamua kuanza kufiga. Mashine zina changamoto sana ya efficiency. Unaweza peleka mayai 100 ukaambiwa yametotolewa 15. Unaweza zimia au ukahisi umeibiwa. Kuku ukimwekea mayai 13 atakupa walau vifaranga 10. Kuna maelezo mengi sana hapa ya kuelezea. Tuishie hapa kwa sasa.

2. Vifaranga wakitotolewa hakikisha wanakaa juu na poop inadondoka chini. Yaani jenga kitu kama chanja hivi ili huduma zao zote wapate wakiwa juu. Ukifuga hii staili ya siku zote vifaranga wakakaa chini/kwenye maranda utaumia sana. Utachukia ufugaji. Ukifanya hii staili nakuhakikishia hatakufa kofaranga yeyote kwa ugonjwa.

3. Hakikisha unajipanga kwa chanjo zote za muhimu za kuku. Japo kwa hiyo staili ya ukaaji hapo juu (2) niliyosema hata ukiamua usichanje watakua vizuri tu. But no need to risk kwa project kubwa. Wapige chanjo zote muhimu.

4. Hakikisha maji na chakula wanapata ipasavyo na kwa wakati. Bila kusahau usafi wa vyombo. Usicheze na usafi kabisa.

5. Jipe muda wa kukaa na kuku bandani na kiwaangalia, wasome tabia zao. Hii itakusaidia kujua kama kuku anaumwa au la. Kuna muda ugonjwa unaweza ingia usifahamu ukachelewa kuwapa dawa halafu ukakuumiza.

6. Vifaranga hakikisha wanakula super starter (pellet) kwa wiki 2 za mwanzo. Pia katika wiki hizi mbili za mwanzo ukiweza wanyweshe maji yenye multvitamin, OTC 20, Trimazine, Amplorium.

7. Hakikisha hizo dawa hapo juu plus fluban muda wote uko nazo ndani.

8. USAFI wa banda ni muhimu muda wote kama kuku wenyewe walivyo muhimu!

Anyway, yapo mengi ya kuelezea. Muhimu FOCUS.

Kila la heri mkuu!

Dongbei.


*
Dah kaka darasa lako zuri
 
Hongera sana mkuu. Ni mawazo mazuri sana. Kwa kusimamia mwenyewe hakika utafanikisha malengo yako na Mungu wetu wa mbinguni akutangulie. Ulishawahi kufuga before? Mimi pia hadi sasa nafanya kama unachofanya, nimeanza mwaka jana September na maendeleo siyo haba. Mimi ninafuga almost ndege (Wafugwao) wote wanaopatikana mazingira ya Tz.

Sasa nina haya machache nadhani yanaweza kukufaa;
1. Kwa idadi ya hao matetea unaweza kukomaa ukatotolesha kwa kutumia kuku wenyewe (sina hakika kama sasso wanaatamia). Kwa maoni yangu ni bora kuliko mashine. Ndicho nachofanya. Nilishawauzia watu mashin sana kabla sijaamua kuanza kufiga. Mashine zina changamoto sana ya efficiency. Unaweza peleka mayai 100 ukaambiwa yametotolewa 15. Unaweza zimia au ukahisi umeibiwa. Kuku ukimwekea mayai 13 atakupa walau vifaranga 10. Kuna maelezo mengi sana hapa ya kuelezea. Tuishie hapa kwa sasa.

2. Vifaranga wakitotolewa hakikisha wanakaa juu na poop inadondoka chini. Yaani jenga kitu kama chanja hivi ili huduma zao zote wapate wakiwa juu. Ukifuga hii staili ya siku zote vifaranga wakakaa chini/kwenye maranda utaumia sana. Utachukia ufugaji. Ukifanya hii staili nakuhakikishia hatakufa kofaranga yeyote kwa ugonjwa.

3. Hakikisha unajipanga kwa chanjo zote za muhimu za kuku. Japo kwa hiyo staili ya ukaaji hapo juu (2) niliyosema hata ukiamua usichanje watakua vizuri tu. But no need to risk kwa project kubwa. Wapige chanjo zote muhimu.

4. Hakikisha maji na chakula wanapata ipasavyo na kwa wakati. Bila kusahau usafi wa vyombo. Usicheze na usafi kabisa.

5. Jipe muda wa kukaa na kuku bandani na kiwaangalia, wasome tabia zao. Hii itakusaidia kujua kama kuku anaumwa au la. Kuna muda ugonjwa unaweza ingia usifahamu ukachelewa kuwapa dawa halafu ukakuumiza.

6. Vifaranga hakikisha wanakula super starter (pellet) kwa wiki 2 za mwanzo. Pia katika wiki hizi mbili za mwanzo ukiweza wanyweshe maji yenye multvitamin, OTC 20, Trimazine, Amplorium.

7. Hakikisha hizo dawa hapo juu plus fluban muda wote uko nazo ndani.

8. USAFI wa banda ni muhimu muda wote kama kuku wenyewe walivyo muhimu!

Anyway, yapo mengi ya kuelezea. Muhimu FOCUS.

Kila la heri mkuu!

Dongbei.


*
1. SASSO hawatamii
2. Mashine kama ni nzuri inatotoresha kwa ufanisi kuliko hata kuku mwenyewe
3. Kwa ufanisi vitamini ni suala endelevu
 
Kaka hicho kiwanda kiko wapi mana na mimi niko kahama labda unaweza kutusaidia kwenye swala la soko
 
Baada ya mvua za msimu huu kuwa za kusita na kupoteza mbegu kwa kupanda zaidi ya Mara mbili na kuungua na jua, huku nyanya nazo zikiwa zinachechemea, nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara Aina ya sasso wakati tunaendelea kusubiri neema ya mvua Kama itatuwezesha kuvuna.

Mpango ni kufikisha kuku 1000 na zaidi mpaka mwisho wa mwaka huu 2022.

Kwa Sasa nimeanza na kuku 25 (mitetea 20 na majogoo 5) ambao nimewanunua December 26 wakiwa na miezi miwili.

Malengo makuu ni kusubiri kuku wafike umri wa kutaga kuanzia march 2022 (wakiwa wamefikisha miezi 5) ili nitotoleshe mayai.

Kuku wakianza kutaga nategemea kupata wastani wa mayai 10 kwa siku (kwa uchache) sawa na mayai 100 Kila baada ya siku 10. Hii inamaana Kila baada ya siku 10 nitapeleka mayai 100 kutotolesha.

Baada ya siku 120 ambayo ni wastani wa miezi 4 kuanzia mwezi March sawa na mwezi July 22 nitakuwa nimetotolesha mayai 1200 ambayo kwa wastani nitapata vifaranga 1000 na kidogo (hayo mayai 200) naasume baadhi yatakuwa hayajatotoleshwa au vifaranga watakaoshindwa kuvuka nursery stage.

Kwahiyo mpaka inafika December 2022(insha_Allah) nitakuwa na kuku 1000 ambao ukiachana na parent 25 nilionza nao kutakua na wakubwa wenye miezi 6,5,4(watakua wameanza kutaga) size ya Kati na wadogo kabisa batch ya mwisho miezi miwili.

Baada ya kufikisha idadi hiyo nitaanza kuuza mayai au kutotolesha vifaranga kwa ajili kuuza au kwa ajili kufuga wa nyama.

KUHUSU GHARAMA
Kuku nimenunu 8000 Kila mmoja sawa na 200,000 kwa kuku wote.

Banda lilikuwepo linalowatosha kuku hao 25.

Kwa kuku watarajiwa Banda lao natarajia kuanza kuhangaika nalo baada ya kuku kuanza kutaga. Ambalo nitalijenga kwa awamu nne (Kila awamu nitakamilisha sehemu ya kuku 300) makisio ya gharama za ufundi kwa Banda la kisasala kuku 1000 na zaidi ambalo nimeandaa eneo la (20x10)m nimepata ni shilling 3.5M kwa materia ya eneo nililokuwepo.

KUHUSU CHAKULA
Kutokana nimewanunua wakiwa wakubwa nimetengeneza mchanganyiko wangu wa chakula ili kupunguza gharama. Ambapo gharama za debe moja(baada ya kuchanganya) ni chini ya 3000 na kuku wote 25 wanakula debe 1 na nusu kwa mwezi. Na nimeanza mchakato wa kutengeneza funza na hydroponic folders na baadae nitaandaa bwawa la azola.

Baada ya kufikisha kuku 1000 makadirio ya chakula kwa siku ni kilo 130 ambazo ni sawa kwa mchanganyo wangu wa chakula + hydroponic ni 500 kwa kilo. Sawa na sh 65,000 kwa siku

KUHUSU MATARAJIO YA FAIDA
kwa mwaka huu wote wa 2022 silengi kupata faida, nahitaji mradi ujisogeze na uwe stable. Kwa maana mpaka inafika December 2022 mradi uwe umerudisha gharama zangu japo kwa uchache na uwe inaweza kujiendesha kwa kuuza mayai au kuku.

Baadaya ya mwaka huu nategemea kupata faida Kama ifuatavyo.

1. Kwa kuwa natarajia kwenye kuku 1000 kuwe na mitetea isiyopungua 800 hivyo nategemea kukusanya mayai yasiopungua 510 kwa siku(kwa makadirio ya chini. Sawa na tray 17 kwa siku .

Tray 1ni sawa na tsh10,000 kwa mayai ya chotara (Bei za nilipo) sawa na tsh 170,000 kwa siku

NB: Mradi huu nitausimamia mwenyewe kwa asilimia 100 hivyo hakuta kuwa na gharama za ziada za mfanyakazi.

Hivyo ndivyo nitavyoiishi 2022.

Nakaribisha maoni.
Sasa mwaka umetimia vipi umefanikiwa?
 
Back
Top Bottom