Naipongeza serikali kwa kuanzisha kodi hii ya nyumba na sehemu za biashara kwa wamiliki

Hiyo kodi ipo kitambo sana, TRA huwa wanawa-tight sana wale wanaofungua biashara kwa kuwataka kuleta mkataba wa upangishaji ili wakate chao ambacho 10% pamoja na zile nyumba zinazopangisha makampuni na mashirika maana mashirika na makampuni mengi lazima yataomba receipt hivyo lazima mkataba utaonyesha na kodi.

Kwa makazi wameamua kupotezea kiaina maana wame-assume kama support kwa Watanzania wanyonge maana ukiwa-bana wapangishaji watakaoumia ni wapangaji
 
Nyie waleteni hao mawakala wenu na makalai sijui makarani wa sensa, sie hatusumbuki, tutawapa data za uongo[emoji1787][emoji1787][emoji1787].

Sio kwamba hatuipendi nchi ila acha tuwadanganye ili kulinda kodi zetu ambazo wanasiasa na machawa mngezikusanya na kuzichakachua na ndugu zenu huko.

Mtabuni kila njia ila ukwepaji hautokwisha kamwe, na hautokwisha mpka pale wananchi watakaporidhika na kasi ya maendeleo kulingana na kodi zao...
 
Unaweza kuthibitisha hili?
 
labda niongezee tu kwa siku za hivi karibuni kumezuka watu wananunua maeneo halafu wamekuwa wakiyarasimisha kwa kukata viwanja vingi tu wakati mwingine mpaka 60 na huwa wanaviuza kwa kusaidiana na wanavijiji kama njugu bila Kuwepo hata kwa stamp duty ya serekali mtu anapatiwa tu karatasi la ubluu gumugumu limesainiwa analipa hapo million 2 biashara imekwisha.
 
Ipende Nchi yako na kuwa mzalendo kwa kulipa Kodi kwa maendeleo ya Nchi.
Wewew ni ndizi mzuzu kabisa ........wanasema malipo ya serikali bure lakini kuna Ada .....SASA sijui hiyo Ada ajalipa Nani mpaka niwekewe Mimi......bado Tu unataka niipende serikali,nyumba yangu nimejenga Kwa akili zangu useme serikali inataka Kodi kwenye vyumba vya kupangisha HUO ni wazimu mkubwa kama haziwatoshi za tozo kwenye Kira muamala basi wakasuuzwe na mabepari huko
 
Serikali inaacha kutengeneza vitega uchumi na miundombinu madhubuti ikiwemo mifumo imara.
Wanakimbilia kuweka kodi kwenye vitu vidogo kabisa visivyo na msingi na kuanza kunyonya huku ikiacha mafisadi na wala rushwa kwenye miladi mkibwa wakipeta na kuharibu mifumo kila siku.

Bado kodi za kukata nywele na ndevu, mwisho kabisa watataka na kodi ya kulala na mkeo.
Keep going.
 
Kinachotakiwa hapo ni ka percentage kadogo ili uchongewe barabara, usogezewe nguzo ya umeme na huduma ya maji, hapo ulipo idadi yenu baada ya kuhesabiwa ikifikia watu 750 mtahitaji zahanati, shule na mengine mengi tu.
Ona mfano kwa kodi hizi ndipo serikali inapata pesa za kulipia vijana watakaokuja kukuhesabu hapo kwako kwa manufaa yako ya hapo baadae.
 
But we should also note that overtaxing economy is a very counterproductive economy. If all incomes are taken from consumers, disposable income will be ruined and people may not consume to a standard level. Consequently, production will go down, retrenchments will be everywhere and the economy will run in recession. Only IMF will come to rescue the situation with a huge burden to the public. My take, taxing shall go in hand with profits, particularly, that earned through production.
 
Mnawakusanyia wanasiasa tu ilhali wananchi wanazidi kuwa fukara!
 
Kinachobakia hapo ni ka percentage kadogo ili uchongewe barabara, usogezewe nguzo ya umeme na huduma ya maji, hapo ulipo idadi yenu baada ya kuhesabiwa ikifikia watu 750 mtahitaji zahanati, shule na mengine mengi tu
Nakubaliana name kwa 100%.
 
Ndugu yangu jino la mamba wewe ni mzalendo ila nauliza mfano mimi nina hostel mbili lakini hakuna wanafunzi kabisa huu mwaka wa pili kwa hiyo niwe nalipa kwenye hamna .
Wazo lako narudia ni zuri mno
 
Ili serikali iwezw kujiendesha na kutimiza wajibu wake lazima ulipe Kodi na tozo mbalimbali kwa mujibu wa sheria sasa hiyo unayotaka bure nani akupe Cha Bure wakati ni wajibu wa wewe kufanya Kazi na sehemu ya mapato yako yaende serikalini.
 
Kodi sio mpya sema walianza kuitekeleza miaka ya karibuni kila miaka nalipa hiyo kodi ya 10%..
 
Walipe kodi safi sana

Duniani hakunaga cha bure

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…