Naipongeza serikali kwa mfumo wa NEST japo bado una changamoto kubwa

Naipongeza serikali kwa mfumo wa NEST japo bado una changamoto kubwa

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Huu mfumo wa manunuzi serikalini kidigitali (National e-Procurement System of Tanzania) kwa kifupi NEST ni mfumo mzuri ambao utasaidia kupunguza upigaji na kuleta fair play kwenye kutoa tenda za serikali.

Ni kitu kizuri kuwahi kufanywa na serikali. Wajasiriamali wenye kampuni ndogondogo wataambulia chochote kitu toka serikalini badala ya wachache kutafuna wenyewe.

Pia serikali itapata huduma na bidhaa kwa bei nzuri kwasababu ya ushindani uliopo. Gharama zitapungua sana kwa upande wa serikali. Kupitia hizi Tsh 10k wanazolipa wafanyabiashara kama fee ya tenda serikali itakusanya sana.

Pamoja na kusifu bado mfumo wa NEST una changamoto nzito mno. Kwanza ni mfumo mzito mno kuufungua.

Yaani hiyo tovuti ya NEST kufunguka inachukua muda mno. Hadi ujaze tenda na ku-submit lazima uwe na uvumilivu wa hali ya juu.

Na hapo naongelea kwa sisi wa mijini ambapo network haisumbui sana. Sasa mtu wa huko Wampembe sijui inakuwaje? Inasikitisha.

Lakini kwa upande wa taasisi za serikali zinazo-upload tenda documents nao wanapitia wakati mgumu kutokana na uzito wa mfumo. Ninajiuliza wakuu wa shule hasa za vijijini wanapitia hali gani toka huu mfumo uanze kutumika?

Ninawasihi wahusika wa NEST wachukue hatua za haraka kutatua haya matatizo kwenye mtandao wao. Hii hali ikiendelea nao watakuwa kwenye kundi la wahujumu wa jitihada za serikali.
 
Huu mfumo wa manunuzi serikalini kidigitali (National e-Procurement System of Tanzania) kwa kifupi NEST ni mfumo mzuri ambao utasaidia kupunguza upigaji na kuleta fair play kwenye kutoa tenda za serikali. Ni kitu kizuri kuwahi kufanywa na serikali. Wajasiriamali wenye kampuni ndogondogo wataambulia chochote kitu toka serikalini badala ya wachache kutafuna wenyewe. Pia serikali itapata huduma na bidhaa kwa bei nzuri kwasababu ya ushindani uliopo. Gharama zitapungua sana kwa upande wa serikali. Kupitia hizi Tsh 10k wanazolipa wafanyabiashara kama fee ya tenda serikali itakusanya sana.

Pamoja na kusifu bado mfumo wa NEST una changamoto nzito mno. Kwanza ni mfumo mzito mno kuufungua. Yaani hiyo tovuti ya NEST kufunguka inachukua muda mno. Hadi ujaze tenda na ku-submit lazima uwe na uvumilivu wa hali ya juu. Na hapo naongelea kwa sisi wa mijini ambapo network haisumbui sana. Sasa mtu wa huko Wampembe sijui inakuwaje? Inasikitisha. Lakini kwa upande wa taasisi za serikali zinazo-upload tenda documents nao wanapitia wakati mgumu kutokana na uzito wa mfumo. Ninajiuliza wakuu wa shule hasa za vijijini wanapitia hali gani toka huu mfumo uanze kutumika?

Ninawasihi wahusika wa NEST wachukue hatua za haraka kutatua haya matatizo kwenye mtandao wao. Hii hali ikiendelea nao watakuwa kwenye kundi la wahujumu wa jitihada za serikali.
Mfumo ni wa kihuni wala hakuna haja ya kuweka unafiki na inaonekana mfumo huu umetengenezwa na unexperienced programmers kwa kuwa una makosa mengi sana ya kiufundi ambayo kutokana na umuhimu wake hayakutakiwa kuwepo kabisa

Kwanza kabisa mfumo hauna accurate filters, mfumo hauna errors feedback, mfumo bado sio automotive maana bado ili kuweka mambo sawa lazima uonane na mzabuni kwa bargain nje ya mfumo(upigaji bado upo hapo)mfumo ni too complicated na sio user friendly, unahitaji expert zaid tofauti na hali halisi za watumiaji , jumlisha uzito na ukono kono wa mfumo, nasema hivi wazawa watumike kutengeneza vimifumo vidogo kwanza vya taasisi ili wapate uzoefu mkubwa , lakini hii mifumo mikubwa na yenye matumizi ya kitaifa ,hapana serikali itumie wataalamu wenye uzoefu mkubwa.

Nashauri kwa mifumo sensitive kama huu wa NEST bora serikali itumie experienced programmers ili kupunguza usumbufu kwa watumiaji na si kama ilivyo sasa kwenye NEST na mifumo mingine kutoka kwa hawa wahuni wa E-ga uwezo bado wa kutengeneza mifumo mikubwa ya kitaifa kama nest
 
Kuna watu wa IT pale juu kwa host wa mfumo wanajua kuchezesha mambo kwenye zile tenda kubwa kubwa ili kuwafaidisha watu fulani wanaojua kufanya lobbying kwa kutumia pesa chafu.
 
Mfumo ni wa kihuni wala hakuna haja ya kuweka unafiki na inaonekana mfumo huu umetengenezwa na unexperienced programmers kwa kuwa una makosa mengi sana ya kiufundi ambayo kutokana na umuhimu wake hayakutakiwa kuwepo kabisa

Kwanza kabisa mfumo hauna accurate filters, mfumo hauna errors feedback, mfumo bado sio automotive maana bado ili kuweka mambo sawa lazima uonane na mzabuni kwa bargain nje ya mfumo(upigaji bado upo hapo)mfumo ni too complicated na sio user friendly, unahitaji expert zaid tofauti na hali halisi za watumiaji , jumlisha uzito na ukono kono wa mfumo, nasema hivi wazawa watumike kutengeneza vimifumo vidogo kwanza vya taasisi ili wapate uzoefu mkubwa , lakini hii mifumo mikubwa na yenye matumizi ya kitaifa ,hapana serikali itumie wataalamu wenye uzoefu mkubwa.

Nashauri kwa mifumo sensitive kama huu wa NEST bora serikali itumie experienced programmers ili kupunguza usumbufu kwa watumiaji na si kama ilivyo sasa kwenye NEST na mifumo mingine kutoka kwa hawa wahuni wa E-ga uwezo bado wa kutengeneza mifumo mikubwa ya kitaifa kama nest
Mfumo ni mzuri tofauti umekuwa rushed wakati bado haukuwa complete. Hili mhe wazir analojia, tatizo si experienced programmers tatizo ni deployment, wanachokifanya sasa ni ouendelea ku develop wakat umeshakuwa deployed lazima ilete shida kwa users
 
Mfumo ni mzuri tofauti umekuwa rushed wakati bado haukuwa complete. Hili mhe wazir analojia, tatizo si experienced programmers tatizo ni deployment, wanachokifanya sasa ni ouendelea ku develop wakat umeshakuwa deployed lazima ilete shida kwa users
Kama wewe ni mtu wa programing na umeutumia huo mfumo basi utakuwa umenielewa
 
"Failed to Issues Intention to Award"

Shida inaweza kuwa nini hapo?
 
Back
Top Bottom