Naishauri Azam inunue timu ya Pan Africa na jina liwe Azam Pan Africa

Naishauri Azam inunue timu ya Pan Africa na jina liwe Azam Pan Africa

SHIGOTTO

Senior Member
Joined
Sep 4, 2018
Posts
156
Reaction score
282
Ndugu wanamichezo wenzangu, nimefikiria na kuja na wazo kuhusu timu ya Azam, kama itawezekana basi viongozi wa Azam wafikirie kuinunua timu ya Pan Africa na jina la timu iwe Azam Pan Africa.

Sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kwamba Pan Africa bado ipo na ina mvuto lakini uwezo wa kujiendesha hadi kufikia kiwango cha juu ni mdogo sana.

Ikumbukwe kuwa Pan bado ina wapenzi wengi, kwa upande wa Azam wao wana uwezo wa kupata mahitaji yote lakini wanakwama sana katika kufikia malengo na kupata wapenzi kindakindaki.

Kwa hivyo basi muunganiko wa Pan na Azam utaifanya timu kuwa na uimara na hasa katika uwakilishi na kuchukua ubingwa mbalimbali.

Napenda kuwakilisha.
 
Niliwahi waza hivyo. Kwa jina lao Azam hawatakuja kupata mashabiki. Napendekeza wajiite Dar Football club. Watapata mashabiki. Hata wangejiita Temeke football club wangekuwa na mashabiki wa kutosha. Kama kujitangaza watajitangaza kwenye hizo jezi nk.
 
Niliwahi waza hivyo. Kwa jina lao Azam hawatakuja kupata mashabiki. Napendekeza wajiite Dar Football club. Watapata mashabiki. Hata wangejiita Temeke football club wangekuwa na mashabiki wa kutosha. Kama kujitangaza watajitangaza kwenye hizo jezi nk.
Kweli kabisa
 
Hili jina la AZAM niliwahi kumwambia mtu kuwa si wazo zuri kutumia kwa timu ingawa kibiashara linaonekana ni zuri maana linasaidia kubrand biashara nyingine za AZAM.

Ila hilo ulilopendekeza ukumbuke timu ya Pan African ilitokea Yanga.
 
Ndugu wanamichezo wenzangu, nimefikiria na kuja na wazo kuhusu timu ya Azam, kama itawezekana basi viongozi wa Azam wafikirie kuinunua timu ya Pan Africa na jina la timu iwe Azam Pan Africa.

Sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kwamba Pan Africa bado ipo na ina mvuto lakini uwezo wa kujiendesha hadi kufikia kiwango cha juu ni mdogo sana.

Ikumbukwe kuwa Pan bado ina wapenzi wengi, kwa upande wa Azam wao wana uwezo wa kupata mahitaji yote lakini wanakwama sana katika kufikia malengo na kupata wapenzi kindakindaki.

Kwa hivyo basi muunganiko wa Pan na Azam utaifanya timu kuwa na uimara na hasa katika uwakilishi na kuchukua ubingwa mbalimbali.

Napenda kuwakilisha.
Wao wenyewe wanashindwa kujiendesha ndio itakuwa Pan?
 
Hili jina la AZAM niliwahi kumwambia mtu kuwa si wazo zuri kutumia kwa timu ingawa kibiashara linaonekana ni zuri maana linasaidia kubrand biashara nyingine za AZAM.

Ila hilo ulilopendekeza ukumbuke timu ya Pan African ilitokea Yanga.
Yeah ni kweli lakini sidhani kama itasumbua sababu hata simba ilitokea kwa Yanga
 
Mimi nashauri ainunue toto afrkan ya mwanza na aiite Azam toto African
Sababu kwa mkoa wa mwanza kwa sasa hauna timu ya ligi kuu na mwanza Ina mashabiki hatari wa mpira
Kwa wanaokumbuka enzi za biashara ya mwanza na pamba .kipindi pamba ni pamba ya moto enzi za kina hamza mponda,fumo, George masatu.
Niishie hapo tu azam ainunue toto
 
Mimi nashauri ainunue toto afrkan ya mwanza na aiite Azam toto African
Sababu kwa mkoa wa mwanza kwa sasa hauna timu ya ligi kuu na mwanza Ina mashabiki hatari wa mpira
Kwa wanaokumbuka enzi za biashara ya mwanza na pamba .kipindi pamba ni pamba ya moto enzi za kina hamza mponda,fumo, George masatu.
Niishie hapo tu azam ainunue toto
ni wazo zuri pia Ila miundo mbinu yake yote ikiwemo uwanja viko dar bado haitaleta raha sana kwa wasukima
 
Niliwahi waza hivyo. Kwa jina lao Azam hawatakuja kupata mashabiki. Napendekeza wajiite Dar Football club. Watapata mashabiki. Hata wangejiita Temeke football club wangekuwa na mashabiki wa kutosha. Kama kujitangaza watajitangaza kwenye hizo jezi nk.
Wewe angalau umeupiga mwingi ila sio mtoa mada!
 
Back
Top Bottom