Naitwa Analyse, na hii ndio safari yangu ya maisha...

Naitwa Analyse, na hii ndio safari yangu ya maisha...

[emoji1] [emoji1] [emoji1] wakuu bhana "likes/thanks" ni kama motisha tu kujua kwamba kuna kundi kubwa la watu lipo nyuma yako likiku support kwa namna moja au nyingine.

NB: nimejibu kwa niaba ya mhusika.

Smart guy
Haya na wewe chukua hiyo [emoji23]
 
Kabisa mshua wa analyse

Anahtaji zawadi

Zawadi kubwa sana

Siku ya wababa ya leo , naiazimisha kwa baba yake analyse na kwa baba yangu

Advance nakumbuka nlsoma shule tatu

Primary shule tano

nlkua kivuruge sana , ila mzee hakuwahi nikatia tamaa

Teh ..


Heshima kwenu wadingi ...


Leo na mtoto anaitwa theodore ...

Nakumbuka huu msemo pia wa mama" mwanangu utakuja kuwa na watoto

Teh ...

Juzi kaiba penseli za wenzake wote

Kesi bado sijaimaliza
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Mwanangu akimaliza Analyse ni zamu yako
 
.... Tofauti na wengi wanafikiria, leo hii ukiniuliza shujaa wangu ni nani katika dunia hii,au ni nani namkubali sana katika ulimwengu huu, kwa kujivunia kabisa nitasema "BABA YANGU" . Huko mbele nitakwambia kwanini au hata wewe utagundua sababu.

Msimu wa kilimo ulipofika, sikuwa na hela ya kutosha kusema iniwezeshe kulima eneo kubwa sana. Nilifanya ushirikiano na jamaa mwingine mmoja, kwa pamoja tukafanikisha kulima heka tano za mbaazi. Shamba tulipata eneo moja lipo manispaa ya Songea, linaitwa Mlilayoyo. Tuliweka juhudi zote na usimamizi wa hali ya juu. Zao lilistawi vizuri sana. Naweza sema kati ya watu wote tuliokuwa tumelima maeneo ya pale, mimi na jamaa ndio tulikuwa na matokeo mazuri. Nakumbuka wakati tunaanza kilimo, bei ya mbaazi ilikuwa juu na nzuri. Kilo moja kuna sehemu ilikuwa inafika hadi 2500.

Msimu wa mavuno wakati unakaribia, ndio zikaja zile tetesi za kushuka kwa mbaazi. Tetesi zikawa kweli, soko likapotea. Ikafika kipindi kisado kinauzwa shillingi 500. Tukashauriana na jamaa tusivune, tusubirie hadi soko likae vizuri kwanza. Siku zikaenda, soko halikai sawa, mpaka mbaazi zetu zikakutana na msimu mpya wa kilimo. Gharama ya kuzivuna ilikuwa kubwa kuliko hata hela ambayo ingepatikana baada ya kuuza, achilia mbali gharama za kuendesha shamba mpaka kufikia hapo.

Mwenye shamba lake anatuuliza, tunampango gani msimu ujao? Tunalikodi tena shamba lake au la? Kama hatukodi, basi tuvune mbaazi tumuachie ardhi yake. Mshirika wangu ananiuliza, tunafanyaje? Nikamwambia me sina cha kufanya , we amua chochote utakachoona nakuachia shamba lote, siwezi kuingia tena gharama za kuvuna. Jamaa nikatemana nae kwa mtindo huo. Nikarudi ghetto pale moonlight.

Kwavile hela niliingiza zote kwenye kilimo, nikawa nimefulia tena. Hapo nilipata somo kuwa kama bajeti ya unachotaka kufanya ni laki 3,alaf na wewe una laki 3 hiyo hiyo, acha. Tulia kwanza mpaka upate hela ya ziada walau mara mbili ya hiyo au hata nusu yake, vinginevyo utakuja kuona watu wanakuchawia huko mbeleni.

Nilianza upya vibarua, hapo nipo choka mbaya. Baada ya kudunduliza na kupata hela kadhaa, sikutaka kujiuliza mara mbili wala kuzurura sana mitaani maana naweza nikakutana na mtu mwingine akanipa fursa. Nikaamua kurudi nyumbani.


*** **** **** **** ****

Nilifika nyumbani majira ya usiku. Kabla sijaingia kwenye himaya ya nyumbani kabisa, nilipaangalia kwa muda mrefu sana. Kwa muonekano palikuwa panavutia na maisha hayakuwa mabaya. Nikagonga mlango baada ya kuvuka fensi ya maua na geti kubwa la mbao. Baba ndio alifungua mlango, alivyoniona akaniambia karibu. Yani hakuonesha kama ameshangaa, amefurahi au kushtuka, kiufupi alichukulia kama nilienda dukani sasa ndio narudi.

Asubuhi ya siku hiyo, naskia mama alijichoma na msumali wakati anapalilia maua pale nyumbani, toka hapo hakuweza kukanyaga vizuri chini, alikuwa anachechemea, ila aliponiona nahisi alipata ganzi ya mguu, maana sio kunikumbatia tu, bali pamoja na ndevu zangu alinibeba. Nikapata faraja niliyoitaka, faza nikampotezea. Pale mezani alikuwa ndio anamtengea mzee chai na maandazi (siku zote baba hupenda kunywa chai usiku hata awe ameshiba vipi). Basi ile chai akanipa mimi, Mzee anauliza vipi mbona unagawa chai yangu? Mama hana hata habari nae. Mara kaniletea hiki, mara kile, ilimradi ukarimu. Nilipoenda kulala, kila mara anakuja kunichungulia. Sina uhakika kama yeye alilala usiku ule.

Asubuhi ndio tuliweza kuongea vizuri kama familia. Hapo mama ameshawaambia ndugu zangu wote kuwa nimerudi. Baada ya chai ndio niliweza kukaa na kuongea na mzee. Kitu cha kwanza kuniuliza "Umefata ada?". Nikamwangalia kwa mshangao, ila kilichonishangaza zaidi nilipogundua kuwa hakuwahi kuwaambia nyumbani kuwa tulikutana Madaba, Songea. Ilo lilinishangaza.

Ila aliniambia, "Ulitaka nimwambie mama yako kuwa baada ya kupotea miaka mingi tulikutana ukiwa kibarua ambae maisha bado yamekupiga? Au baada ya miaka mingi kutoonekana, tumeonana ila bado ukaniomba hela? . Nilijua hutorudi ndio maana sikumwambia chochote mama yako kwa kipindi kile, na pia sitoshangaa kama utaondoka tena. Najua tulipoachana maisha yako yaliendelea kuwa magumu na ndio maana hata hela niliyokutumia wala hukunirudishia. Nikajiuliza hela gani alinitumia huyu mzee? Nahisi alijua ninachowaza, akaniambia siku tuliyoachana alichukua namba yangu toka kwa wale vibarua niliokuwa nafanya nao, na alipoona imepita zaidi ya miezi 6 sijaonekana nyumbani alinitumia laki 3 kwenye simu. Nikakumbuka kuna siku iliingia hela, nikajua mtu kakosea kutuma, nikaitoa kwa wakala alaf nikakausha. Mtumaji nae hakunicheki tena. Niliona aibu kichizi.


Baba akaniambia "Ikitokea leo hii Mama yako aseme nyie wote 7 sio wanangu, nitakubaliana nae kwa hao 6 wengine lakini wewe nina uhakika wa asilimia zote ni mwanangu. Mimi na wewe ni mapacha tuliozaliwa katika miaka tofauti, kwa kifupi ww ni mimi". Maneno ya mzee yalinigusa sana kwa mbali machozi yakawa yananilenga hivi. Faza akaniambia "Kama unalia nenda jikoni kwa mama yako" . Mzee wangu kauzu kichizi yani,kwanza toka nakua sijawahi kumuona anasikitika. Nikabaki nashangaa tu maneno yake. Akazidi kuniambia " Tofauti ya ww na mimi, ni kwamba mimi nilirudi baada ya safari yangu kuelekea mwishoni,nilirudi nikiwa shujaa. Wewe ni shujaa lakini safari yako haijaisha,umerudi ikiwa kati"

Kuna mengi sana hatuyajui kuhusu wazazi wetu ambayo yangetufunza na kutujenga, hii inatokana na kwamba tuko bize sana kiasi tunakosa muda wa kuzungumza nao. Misukosuko tunayokutana nayo leo hii, majibu yote yapo kwenye maisha waliyopitia wazazi wetu. Tunatafutaga majibu, lakini majibu sahihi yapo tulipotoka. Baba yangu ni Shujaa wangu,Mimi ni Baba yangu,na Baba yangu ni Mimi, unajua kwanini? Ni kutokana na stori fupi ya safari ya maisha yake aliyonisimulia.


*** *** *** *** *** ***

Kwa ufupi tu ilikuwa hivi. Anasema "Sikuwa na uwezo mkubwa wa kuelewa darasani, shule niliishia elimu ya msingi hata mtihani wa mwisho sikufanya, nilifukuzwa kwa kosa la kuchoma ofisi ya walimu. Tokea hapo nilikuwa naonekana kama mtoto mtukutu nyumbani, babu yako aliniwekea zamu ya kuchunga kila siku, alaf nyumbani sikuwa napewa upendeleo wowote. Kuna siku nilienda kuchunga,jioni nikarudisha ng'ombe ila nikasepa na mbuzi wote. Nikauza na kufanya mtaji. Heri yako unaondoka nyumbani umepewa hela, tena tukijua kuwa utaondoka. Sijui msoto uliopitia ww, lakini msoto niliopitia mimi baba yako ndani ya miaka minne ya mwanzo nadhani ww ungekufa. Ndani ya hiyo miaka minne ya mwanzo kuna siku niliamua kabisa kurudi kwa babu yako nikaombe msamaha, nilifika mpaka pale, nikaiangalia sana nyumba ila nikaona siwezi kurudi nikiwa hivi, nikageuza na kuondoka. Ndio maana sikuile tuliyokutana Songea, nilijisemea kimoyo moyo, kama huyu ni mwanangu hatorudi nyumbani.

Tokea ile siku niliyogeuza, nilijituma sana kiasi kwamba siku niliyorudi nyumbani, nilirudi na idadi ile ile ya mifugo niliyoondoka nayo ila badala ya mbuzi nilirudi na ng'ombe. Ila pamoja na hayo babu yako aligoma kunisamehe hadi kikafanyika kikao na wazee wa kijiji, ndio nikasamehewa,tena baada ya kuchapwa bakora pamoja utu uzima wangu.

Aliendelea kunisimulia vitu vingi sana, hapo ndio nikajua nilidhani nimesota na kupitia tabu nyingi sana, kumbe ningezifananisha na za mzee, basi zangu zingekuwa ni utangulizi tu. Mgodini niliposhindwa kwenda, yeye alishaenda na alishawahi kufukiwa hadi na kifusi. Baba yangu akitembea huwa anachehemea,mguu mmoja ni kama mfupi. Ananiambia ule ulishavunjika mara mbili kutokana na mbilinge za migodini.

Tokea siku hiyo, kila nnapopitia ugumu wowote, lazima nijiangalie kwenye kioo. Baba yangu ni kioo changu.

*** **** *** *** ****

Kurudi kwangu kulirudisha furaha sana nyumbani. Usiku kabla ya kulala, mshua aliniuliza "Una watoto wa ngapi mpaka sasa? Nikamjibu mmoja wa kiume. Akasema namuhitaji, fanya mpango aje hapa nyumbani.

Najua kuna wadau watashangaa kuona nimesema nina mtoto mmoja wa kiume, wakati katika stori yote sijawahi kuongelea ili swala. Katika hii stori ya safari yangu, nimegusa baadhi ya matukio ya kwenye maisha yangu ila sio yote. Na sijagusia mapenzi kwasababu yamenitesa kichizi, nadhani mwanaume akiwa hana hela mwenendo wake wa mapenzi unajilikana tu,mapenzi yanatesa sana Me kuliko Ke. Kuna msemo mmoja nimeuona juzi kuwa "Mwanaume kama huna hela, kazi ya kulinda mahusiano yako muachie Mungu" hii ni kweli kwa asilimia zote. Kwa ufupi kwenye hii safari yangu, mtoto ninae tena wa kiume.


Nikafanya mpango na taratibu zote, nikapewa yule mtoto. Sasa hivi anaishi na babu yake.

Siku ambayo mtoto alifika pale nyumbani, kesho yake mzee aliniita tukawa na mazungumzo ya hapa na pale. Kisha akatoa bahasha na kunikabidhi, kuhesabu ni milioni mbili. Nikamuuliza za nini. Akasema "Babu yako alinipokea baada ya kufanya kikao na wazee kisha nikachapwa bakora,nimekupokea nyumbani ila sitokuchapa...Safari yako bado haijaisha, nenda kapambane". Nilimwangalia yule mzee sikummaliza.

Wiki moja badae nilikuwa ndani ya bus naelekea Songea. Nikarudi rasmi kwenye kilimo. Safari hii nikalima tangawizi..

Nitarudi kukwambia jambo zuri lililotokea. Katika maisha,Baraka za wazazi ni kila kitu.

....

Analyse #Baharia wa nchi kavu.
Sasa Hata ukiishi hapa poa!!! Nimekuheshimu bro! Na vimachozi vimenitoka! Baba yako ni mwanaume kama ulivyo wewe!! Ila safari bado itaendelea!! Thanks man
 
Nlmuhamishia shule nyingine

Aisee

Et anawaambia walimu wake

" i was too smart for the teacher of that school "[emoji28]

Teh yupo la nne
Mm wangu alikuwa mpole sana, ila alikutana na wakongwe waliomfundisha ubabe. Sasa yeye ndio kawa mbabe zaidi yao. Walimrudisha darasa ila jamaa yuko vzr kichwani hd walimpandisha tu.

This time nikasema wacha apumzike na masomo ya likizo, mtu mwenyewe ndio yuko class one tu. Ijmaa mwl wake alinipigia anasema mwanangu ni mtundu ila anachangamsha sana darasa km itawezekana nimruhusu wiki ijayo aanze kwenda shule.
 
Kusema ukweli wanaume wanaosoma hii story Tunatakiwa kuwa kama mshua wake Analyse..yule baba ni watofauti sana sana.

Kwanza hakumlazimisha mtoto kwenda shule hilo ni jambo zuri sana kama mzazi (tukubali tukatae)

Pili baada ya kutomlazimisha hakumfukuza tu kama mbwa nyumbani kama wafanyavyo wazazi wetu wengine,ila alimpa analyse ADA yake atakayoitumia Shule aende AKAILE MWENYEWE (hapa mzee alinawa mikono)

Baada ya kumpa Ada alimwambia achague mawili..kwenda shule au Kujitegemea (analyse alichagua kujitegemea) kwa mtaji wa ADA YAKE(sitegemei kuja kuona analyse anamlaumu baba yake hata kidogo)

Hiyo haitoshi wamekuja kukutana tena na mshua macho kwa macho Mshua akampa tena BAKI iliyobaki kwenye ile ADA YAKE (huyu baba nimemkubali kwa asilimia 5000000)

Kwa simulizi hiiii pamoja na mapito ya kujifunza kupitia analyse ila kuna BABA ANALYSE huyu mzeee nina uhakika leo hii analyse anasimulia haya ila anampenda BABA YAKE kwa kipimo kisichopimika(au uongo Analyse )

Endelea mkuu na simulizi..sema nini mwambie mshua wako (ambae ni baba yangu pia) Kuna mwanae asiejulikana anamkubali vibaya mno,kwa kudhihirisha hilo naomba unambie mtandao wa simu anaotumia mshua (sio namba ya simu) nataka kujua tu mtandao anaotumia kuwasiliana. (ukishafanya hivyo nina zawadi yake nitakutumia PM) tafadhali MFIKISHIE KAMA NITAKAVYOKUTUMIA WEWE.

#Tuendelee #na #story #mkuu
Nilishakir mapema huko juu, ni role moadal wangu huyu mzee.
 
Kabisa mshua wa analyse

Anahtaji zawadi

Zawadi kubwa sana

Siku ya wababa ya leo , naiazimisha kwa baba yake analyse na kwa baba yangu

Advance nakumbuka nlsoma shule tatu

Primary shule tano

nlkua kivuruge sana , ila mzee hakuwahi nikatia tamaa

Teh ..


Heshima kwenu wadingi ...


Leo na mtoto anaitwa theodore ...

Nakumbuka huu msemo pia wa mama" mwanangu utakuja kuwa na watoto

Teh ...

Juzi kaiba penseli za wenzake wote

Kesi bado sijaimaliza
Hilo jina la mtoto wako asije akawa mtukutu kama T-bag wa prison break.T bag (Theodore)
 
Aisee the same to me.
Kilichonikuta mwaka huu n balaaa
Nimekodi nimekodi sehemu kubwa sana ya kulima mpunga kwa pesa nyingi jumlisha walimaji wapandaji daaaa kilichonikuta,
Jua limepiga mpunga ote kwisha yan sijavuna hata gunia moja aisee.
Kilimo sikia tu mwenzio amelima amepiga gunia 50.
Mwaka huu hakuna aliyepata mkuu si mpunga tu hata mahindi, karanga nk jua limepiga hasa.
 
Back
Top Bottom