Najuta kuwekeza kwenye kiwanja na nyumba ya mwanamke

Najuta kuwekeza kwenye kiwanja na nyumba ya mwanamke

Ila za wanawake sio za kupigia hesabu otherwise ziwe chini yako yaani atoe aweke mezani mjue Cha kufanya Kwa pamoja
Afadhali wew alikushirikisha kununua kiwanja kunawenzio wakezao Wana nyumba Hadi 3 za maana na waume hawajui
Hiyo nzuri kuna wanaume ni wabishi sana, kila kitu yeye ndiye kichwa cha familia ushauri wa mke hataki anapokea ushauri wa marafiki, dawa zao ndiyo hizo hakuna nyingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila mimi hakifikia hatua ya kunifukuza kwa nguvu tutagawana majengo ya serikali. Hapa ninaondoka ila sio kwa kuniforce na naondoka kwa sababu anaona nategemea kuishi kwenye nyumba yake kana kwamba mi sina uwezo wa kwenda kupanga chumba.

Maana nimehamia hapa baada ya yeye kuforce nitoke kwenye kupanga ila sikua na mpango napo japo nimechangia kujenga hapa ilikua plan iwe nyumba ya wapangaji sasa nashangaa saa hivi ananiletea ubinafsi wa juu sana
Vip mzigo anakupa kweli? Kama anakubania na mzigo.. hapo jua kuna njemba inapiga... ashaota mapembe huyo mpandishe cheo awe mke wa kwanza
 
Ila za wanawake sio za kupigia hesabu otherwise ziwe chini yako yaani atoe aweke mezani mjue Cha kufanya Kwa pamoja
Afadhali wew alikushirikisha kununua kiwanja kunawenzio wakezao Wana nyumba Hadi 3 za maana na waume hawajui
Sasa kama ni hivi si bora usioe
 
Kumbe hata kiwanja huna? Mmmh😂😂😂 ndoa zina mambo mengi. Pole sana mwana jf
Mkuu kiwanja aliandika jina lake maana yeye ndo alikopa hela ya kununua mimi nimechangia kwenye ujenzi lakini leo hii ananiambia sijachangia chochote hela yote ya kodi za wapangaji anakula pekeake so sitaki kuforce umiliki ila inaniuma tu pesa zangu nlizotupa hapa bora ningeenda kutafuta kiwanja changu hata kijijini huko
 
Ila
We ni mjinga iwapo umejenga nyumba hiyo ukijua no ya kwake na hamjajenga nyumna yoyote kwa pamoja au ya kwako.

Mimi nimeoa mke wa pili nikamwambia anunue kiwanja na ajenge boma mimi nitamalizia akafanya hivyo na mimi namalizia anakaa na watoto wake na kwa security yake na watoto wake.

Tumeweka makubaliano nyumba alizonikuya nazo na mke mkubwa hazimhusu basi mambo yanasonga na hati zote ninazo mimi.

Mwisho tumeweka mou kuwa naweka nguvu zangu kwenye nyumba hiyo yenye jina lake kwa faida yetu sote na haiuzwi na mmoja wetu
na nyie mnaooa wanawake wawili wawili mnanishangazaga sana
 
Kipindi nnanunua eneo la kujenga mzee aliandika jina lake baada ya langu
Siku naenda kufata ile hati ya mauziano nakuta jina lake...nkasema tu ah mzee aje au alisahau ...anyway nkapotezea zangu



Ila sasahiv naelewa Na pengine service zote nkatumia majina yake...

Unapotaka kuowa mkuu make sure una kitu mkononi na unajiweza kidogo kiuchumi
Kitu pekee nnachoweza kukuambia mkuu ni hiki

Asikudanganye mtu eti kuna mwanamke atakupenda wewe et umekaa tu ndani
Fedha ndio hasa heshima ya mwanaume
Tafuta fedha jijenge mwenyewe
Wale wanawake wakusema tuowane tutajenga pamoja
Wa mwisho kufanya hivyo alikua ni mama yako pekee
Hawa wengine wanataka uwe na kitu
Duuh
 
Back
Top Bottom