Kuna uzi niliweka humu jamiiforums Nilimruhusu msaidizi auze bidhaa zake ndogo ila zinamlipa kuzidi mshahara wake. Je, nifanye maamuzi gani?
Summary / Muhtasari:
Msaidizi aliniomba aanze kuuza bidhaa zake, Sina uzoefu sana kwenye biashara niliona nitakuwa kauzu nikimkatalia, nilitaka kuonekana nipo "fair", NIKAMRUHUSU !
Niliweza kupata mbinu ya kujua hesabu zake, kuna kidaftari huwa anakificha sehem flani, nikiona hayupo nakipiga picha fasta
Mshahara naomlipa ni 150,000 + allowance ya matumizi elf 70, jumla 220,000 kila mwezi
Kwa upande mwengine biashara yangu imeshuka sana, Mwezi wa 10 faida ilikuwa laki 3, Mwezi wa 11 faida laki 2 na 15, mwezi huu laki 2 na 40
Gharama za biashara jumla ni 870,000 kila mwezi
Nikafungua uzi humu jamiiforums niombe ushauri nichukue hatua zipi, nilishambuliwa sana kwamba nina ROHO MBAYA nimuache niwe na HURUMA. Ndicho nilichofanya !!
Matokeo yake
Kwa upande mwengine wala simkatazi awe na biashara yake, Itapendeza zaidi apate ukomavu na uzoefu zaidi kwa kuanza kujilipia gharama za biashara, mfano frem laki 8 (minimum miezi 6), umeme, tra, jiji, n.k.
Kuna wadau mmenishauri nitafute muuza duka mwengine, ikiwa kuna dalili za kuto kuelewana au usumbufu nitafanya hivyo.
Summary / Muhtasari:
Msaidizi aliniomba aanze kuuza bidhaa zake, Sina uzoefu sana kwenye biashara niliona nitakuwa kauzu nikimkatalia, nilitaka kuonekana nipo "fair", NIKAMRUHUSU !
Niliweza kupata mbinu ya kujua hesabu zake, kuna kidaftari huwa anakificha sehem flani, nikiona hayupo nakipiga picha fasta
- Mwezi wa 10 kapata faida 183,500
- Mwezi wa 11 kaingiza faida 413,000
- Mwezi wa 12 alianza kutunza mzigo mpaka stoo, Mwezi haujaisha ila faida inakaribia 700,000
- Mwezi wa 11 katikati nilipata taarifa kauza simu yake laki 2 na kitu, kwa hesabu za fasta aliingiza kwenye mtaji.
Mshahara naomlipa ni 150,000 + allowance ya matumizi elf 70, jumla 220,000 kila mwezi
Kwa upande mwengine biashara yangu imeshuka sana, Mwezi wa 10 faida ilikuwa laki 3, Mwezi wa 11 faida laki 2 na 15, mwezi huu laki 2 na 40
Gharama za biashara jumla ni 870,000 kila mwezi
- frame - 500,000 ( ni kwetu wachache tulioziwahi, wengine ni laki 8)
- mshahara na allowance - 220,000
- Tra, Jiji, umeme, maji, usafi, n.k. - 50,000
Nikafungua uzi humu jamiiforums niombe ushauri nichukue hatua zipi, nilishambuliwa sana kwamba nina ROHO MBAYA nimuache niwe na HURUMA. Ndicho nilichofanya !!
Matokeo yake
- Anajali zaidi biashara yake kuzidi yangu, Hapo zamani alikuwa ananipa mwendendo wa biashara , hesabu, n.k. sikuhizi kaacha kabisa, ni mpaka nimkumbushe.
- mara kadhaa nimefika dukani hayupo, nilifuatilia na kugundua anaenda kujumua mzigo wake.
- Namlipia frem, kodi, jiji, usafi, chakula, n.k. lakini bado anaendelea kuchukua allowance ma mshahara licha ya kwamba biashara yangu inachechemea huku yake inanawiri bila gharama zozote.
- Mwaka huu naongeza bidhaa hizo anazouza, Kwa location nilipo kuna wateja wengi
- Biashara zote zinazofanyika dukani zitakuwa mali ya duka, Ikiwa muuza duka kanipa idea nitamkadiria comission.
Kwa upande mwengine wala simkatazi awe na biashara yake, Itapendeza zaidi apate ukomavu na uzoefu zaidi kwa kuanza kujilipia gharama za biashara, mfano frem laki 8 (minimum miezi 6), umeme, tra, jiji, n.k.
Kuna wadau mmenishauri nitafute muuza duka mwengine, ikiwa kuna dalili za kuto kuelewana au usumbufu nitafanya hivyo.