Najutia kufuata ushauri mlionipa kumuonea huruma muuza duka auze bidhaa zake, wachache mlionishauri niweke huruma pembeni mnajua biashara

Najutia kufuata ushauri mlionipa kumuonea huruma muuza duka auze bidhaa zake, wachache mlionishauri niweke huruma pembeni mnajua biashara

Ubepari sio kitu cha kushabikia mana hauna huruma. Kwa muktadha huo jamaa aweke conditions ambazo zitamuamsha tena jamaa kuwa yukona biashara ya mtu anatakiwa auze. Mana nina hakika hiyo karatas aliyoiona hapo ndani ndo anaona dogo anafaidi. Akimtoa hapo bila kuona muelekeo mzuri atamuharibia maisha kabisa

Biashara ndio ubepari wenyewe.
Huwezi Fanya Biashara kama sio bepari.
Biashara unazungumzia Faida. Faida unazungumzia unyonyaji
 
Kuna uzi niliweka humu Nilimruhusu msaidizi auze bidhaa zake ndogo ila zinamlipa kuzidi mshahara wake. Je, nifanye maamuzi gani?

Summary:

Msaidizi aliniomba aanze kuuza bidhaa zake, nilimruhusu

Niliweza kupata mbinu ya kujua hesabu zake, kuna kidaftari huwa anakificha sehem flani, nikiona hayupo nakipiga picha fasta au naweza kumtuma aninunulie vocha nakipiga picha fasta.

  • Mwezi wa 10 alikuwa na faida ya 183,500
  • Mwezi wa 11 kaingiza faida ya 413,000
  • Mwezi wa 12 alianza kutunza mzigo mpaka stoo, kwa movement zilizopo najua faida itakuwa 700,000

Mshahara naomlipa ni 150,000 kwa mwezi, allowance ya matumizi yake elf 70, jumla 220,000

Meanwhile biashara yangu imeshuka sana Mwezi wa 10 faida ilikuwa laki 3, Mwezi wa 11 faida laki 2 na 15, mwezi huu laki 2 na 40

Gharama za biashara

  • frame - 500,000
  • mshahara na allowance - 220,000
  • Tra, Jiji, umeme, maji, usafi, n.k. - 50,000

Ni mwezi wa 11 nilifungua uzi humu kipindi hicho hesabu zake hadi tarehe 13 faida inasoma 186,500 niombe ushauri nichukue hatua zipi, nilishambuliwa sana kwamba nina ROHO MBAYA nimuache niwe na HURUMA.

Ndicho nilichofanya, Matokeo yake

  • Anajali zaidi biashara yake kuzidi yangu, Hapo zamani alikuwa ananipa mwendendo wa biashra , hesabu, n.k. sijgizi kaacha kabisa.
  • Biashara yake kwanza yangu baadae, mara kadhaa nafika dukani hayupo, nilifuatilia na kugundua anaenda kujumua mzigo wake.
  • Namlipia frem, kodi, jiji, usafi, chakula, n.k. lakini bado anaendelea kuchukua allowance licha ya kwamba anaingiza pesa nyingi.
Siku ya jana nimemuambia haya
  • Mwaka huu naongeza bidhaa hizo anazouza, Kwa location nilipo kuna wateja wengi mno.
  • Biashara zote zinazofanyika dukani zitakuwa mali ya duka, Ikiwa muuza duka kanipa idea nitamkadiria cha juu ama tutakuwa tunaenda kwa percent.
Najua fika kabisa mtu alieanza kuzoea faida za laki 7 ukijumlisha na allowance ya laki 2 ni ngumu kukubali kushuka upya, Kwa saikolojia ya binadamu najua atatafuta mbinu, Nilichofanya ni kuweka cctv Camera tarehe 17 mwezi huu na kumuacha aendelee na biashara yake, Lengo la hiocamera ni kumchunguza nikianza kuweka mzigo wangu.
Anauza nn
 
Kosa lake huyo msaidz wako ni kuacha mali zake adharani bila kuficha, alijiamini sana.

Hilo daftar angefaa atembee nalo mfukoni kwakuwa ndyo uzima wake, hajui msemo "ukila na kipofu, usimshike mkono". Ona sasa.......
 
Akijiongeza atakua mshindani wako na atatafuta site jirani hapo hapo na kwa sababu ana wateja na anafahamiana nao Ngoma itakugeuka ,
Namkaribisha ajue maana halisi ya biashara

Frem - Laki 8 minimum miezi 6 ( laki 5 ni kwetu wachache tulioziwahi)
allowance ajilipe kutoka kwenye faida
tra na jiji alipe mwenyewe
n.k.

Biashara ukiifanya bila kujua gharama ni rahisi
 
ujinga ni kuwa na huruma kwenye biashara,...wakati unamruhusu awe na biashara yake, hukujua kuwa biashara ZINAKUA?... kama ulijua, ULIJIANDAAJE?.....,..umechelewa kujua ni kwann waajiri wengi, wanapendelea kuwaajiri watu ambao wana madeni au majukumu mazito nyuma yao, suala la qualifications baadaye,.....
 
Kuna uzi niliweka humu Nilimruhusu msaidizi auze bidhaa zake ndogo ila zinamlipa kuzidi mshahara wake. Je, nifanye maamuzi gani?

Summary:

Msaidizi aliniomba aanze kuuza bidhaa zake, nilimruhusu !

Niliweza kupata mbinu ya kujua hesabu zake, kuna kidaftari huwa anakificha sehem flani, nikiona hayupo nakipiga picha fasta au naweza kumtuma aninunulie vocha nakipiga picha fasta.

  • Mwezi wa 10 alikuwa na faida ya 183,500
  • Mwezi wa 11 kaingiza faida ya 413,000
  • Mwezi wa 12 alianza kutunza mzigo mpaka stoo, Mwezi haujaisha ila faida inakaribia 700,000

Mshahara naomlipa ni 150,000 kwa mwezi, allowance ya matumizi yake elf 70, jumla 220,000

Meanwhile biashara yangu imeshuka sana Mwezi wa 10 faida ilikuwa laki 3, Mwezi wa 11 faida laki 2 na 15, mwezi huu laki 2 na 40

Gharama za biashara

  • frame - 500,000 (Gharama hii ni kwetu wachache tulioziwahi, wengine ni laki 8)
  • mshahara na allowance - 220,000
  • Tra, Jiji, umeme, maji, usafi, n.k. - 50,000

Ni mwezi wa 11 nilifungua uzi humu kipindi hicho hesabu zake hadi tarehe 13 faida inasoma 186,500 niombe ushauri nichukue hatua zipi, nilishambuliwa sana kwamba nina ROHO MBAYA nimuache niwe na HURUMA.

Ndicho nilichofanya, Matokeo yake

  • Anajali zaidi biashara yake kuzidi yangu, Hapo zamani alikuwa ananipa mwendendo wa biashra , hesabu, n.k. sijgizi kaacha kabisa.
  • Biashara yake kwanza yangu baadae, mara kadhaa nafika dukani hayupo, nilifuatilia na kugundua anaenda kujumua mzigo wake.
  • Namlipia frem, kodi, jiji, usafi, chakula, n.k. lakini bado anaendelea kuchukua allowance licha ya kwamba anaingiza pesa nyingi.
Siku ya jana nimemuambia haya
  • Mwaka huu naongeza bidhaa hizo anazouza, Kwa location nilipo kuna wateja wengi mno.
  • Biashara zote zinazofanyika dukani zitakuwa mali ya duka, Ikiwa muuza duka kanipa idea nitamkadiria cha juu ama tutakuwa tunaenda kwa percent.
Najua fika kabisa mtu alieanza kuzoea faida za laki 7 ukijumlisha na allowance ya laki 2 ni ngumu kukubali kushuka upya, Kwa saikolojia ya binadamu najua atatafuta mbinu, Nilichofanya ni kuweka cctv Camera tarehe 17 mwezi huu na kumuacha aendelee na biashara yake, Lengo la hiocamera ni kumchunguza nikianza kuweka mzigo wangu.

Kwa upande mwengine wala simkatazi awe na biashara yake, atapata ukomavu zaidi kwa kuanza kujilipia gharama za biashara, mfano frem laki 8 (minimum miezi 6), umeme, tra, jiji, n.k. (Faida = mapato - gharama)
Sijasoma uzi wote. Ila pole. Kua makini siku nyingine.


..Ni Hayo Tu
 
Ndio maana watu wenye roho mbaya za bznes wanafanikiwa.kuliko wenye roho nzr za bznes.
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Kwanza kabisa wewe mkuu, Mimi nakulaumu, unajua Kwa Nini?

Huwezi na huoni ni biashara Gani itakuingizia faida kubwa katika frem/duka lako.

Assume ungekuwa unauza hizo bidhaa zinazompatia faida mfanyakazi wako na Yeye akawa anauza hizo uuzazo!!!

Bila shaka usingeleta bandiko humu.

Sasa mfanyakazi wa aina hiyo kamwe usimfukuze kazi Bali muajiri muda mrefu, alafu muongezee majukumu ya kumuweka busy.


Utaona kuwa mbegu ulizootesha wewe hazikutoa mazao mazuri, lakini alizootesha Yeye zimeleta mazao mazuri...

Unaweza ukamuuliza hapa au sehemu flani tuuze bidhaa zipi na zipi?

Utashangaa jambo Hilo litafanikiwa sana...
 
Ubepari sio kitu cha kushabikia mana hauna huruma. Kwa muktadha huo jamaa aweke conditions ambazo zitamuamsha tena jamaa kuwa yukona biashara ya mtu anatakiwa auze. Mana nina hakika hiyo karatas aliyoiona hapo ndani ndo anaona dogo anafaidi. Akimtoa hapo bila kuona muelekeo mzuri atamuharibia maisha kabisa
Matajiri waliofanikiwa kwenye biashara hawana huruma mkuu ndio dunia tuliyopo...lengo kuu la biashara ni kutengeneza faida, haijalishi maisha ya wangapi yataharibika
 
Matajiri waliofanikiwa kwenye biashara hawana huruma mkuu ndio dunia tuliyopo...lengo kuu la biashara ni kutengeneza faida, haijalishi maisha ya wangapi yataharibika
Capitalist wanapigania mitaji sio?. Niliwah kuwepo kazin kisiwa kimoja hivi unguja kuna siku mashine ya boti ilitumbukia majini. Alivyokuja meneja akasema kwamba bora angeingia boti man akafia humo kuliko mashine ya watu milion 9 ipatikane tu
 
Back
Top Bottom