Najutia kufuata ushauri mlionipa kumuonea huruma muuza duka auze bidhaa zake, wachache mlionishauri niweke huruma pembeni mnajua biashara


Biashara ndio ubepari wenyewe.
Huwezi Fanya Biashara kama sio bepari.
Biashara unazungumzia Faida. Faida unazungumzia unyonyaji
 
Anauza nn
 
Kosa lake huyo msaidz wako ni kuacha mali zake adharani bila kuficha, alijiamini sana.

Hilo daftar angefaa atembee nalo mfukoni kwakuwa ndyo uzima wake, hajui msemo "ukila na kipofu, usimshike mkono". Ona sasa.......
 
Akijiongeza atakua mshindani wako na atatafuta site jirani hapo hapo na kwa sababu ana wateja na anafahamiana nao Ngoma itakugeuka ,
Namkaribisha ajue maana halisi ya biashara

Frem - Laki 8 minimum miezi 6 ( laki 5 ni kwetu wachache tulioziwahi)
allowance ajilipe kutoka kwenye faida
tra na jiji alipe mwenyewe
n.k.

Biashara ukiifanya bila kujua gharama ni rahisi
 
ujinga ni kuwa na huruma kwenye biashara,...wakati unamruhusu awe na biashara yake, hukujua kuwa biashara ZINAKUA?... kama ulijua, ULIJIANDAAJE?.....,..umechelewa kujua ni kwann waajiri wengi, wanapendelea kuwaajiri watu ambao wana madeni au majukumu mazito nyuma yao, suala la qualifications baadaye,.....
 
Sijasoma uzi wote. Ila pole. Kua makini siku nyingine.


..Ni Hayo Tu
 
Ndio maana watu wenye roho mbaya za bznes wanafanikiwa.kuliko wenye roho nzr za bznes.
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Kwanza kabisa wewe mkuu, Mimi nakulaumu, unajua Kwa Nini?

Huwezi na huoni ni biashara Gani itakuingizia faida kubwa katika frem/duka lako.

Assume ungekuwa unauza hizo bidhaa zinazompatia faida mfanyakazi wako na Yeye akawa anauza hizo uuzazo!!!

Bila shaka usingeleta bandiko humu.

Sasa mfanyakazi wa aina hiyo kamwe usimfukuze kazi Bali muajiri muda mrefu, alafu muongezee majukumu ya kumuweka busy.


Utaona kuwa mbegu ulizootesha wewe hazikutoa mazao mazuri, lakini alizootesha Yeye zimeleta mazao mazuri...

Unaweza ukamuuliza hapa au sehemu flani tuuze bidhaa zipi na zipi?

Utashangaa jambo Hilo litafanikiwa sana...
 
Matajiri waliofanikiwa kwenye biashara hawana huruma mkuu ndio dunia tuliyopo...lengo kuu la biashara ni kutengeneza faida, haijalishi maisha ya wangapi yataharibika
 
Matajiri waliofanikiwa kwenye biashara hawana huruma mkuu ndio dunia tuliyopo...lengo kuu la biashara ni kutengeneza faida, haijalishi maisha ya wangapi yataharibika
Capitalist wanapigania mitaji sio?. Niliwah kuwepo kazin kisiwa kimoja hivi unguja kuna siku mashine ya boti ilitumbukia majini. Alivyokuja meneja akasema kwamba bora angeingia boti man akafia humo kuliko mashine ya watu milion 9 ipatikane tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…