Hao kuku wanaokuambia roho mbaya ukute hawajawahi hata kufanya biashara...
Ngoja nikuambie, Mimi kitambo nilikua nauza duka la mtu, hivyo hivyo nikaanza kuweka bidhaa zangu kisiri siri(MALENGO), akija mteja nachukua namba, nampigia namuelekeza duka letu jingine(ROHO MBAYA), sehemu niliyokua nauza mimi kodi ilikua chini hivyo Bei ikawa ipo chini pia, ila pale kwa Boss sababu ni potential nikawa napatumia kutangaza biashara yangu ila delivery nyingi zinafanyika kupitia kwangu, (ROHO MBAYA PLUS).
Baada ya hapo mauzo yakawa yapo chini, ila kwa sababu bado ile sehemu naihitaji, lakini pia nisimzunguke 100% mtu alieniamini, bila yeye kujua nikamshauri tuweke mzigo wa jumla, ambao najua mimi sina uwezo nao..
Akazama mfukoni tukashusha Kontena
BIASHARA IKAPANDA, akanishukuru sana kwa idea ile na Mimi nikapanda,
WIN WIN..
Wewe usihangaike na faida yake, hangaika na mauzo/faida yako, jipe muda, ukigundua inashuka sababu ya biashara yake Fukuza au Mlipe kwa %,, ukiona inapanda(ilishuka kwa sababu nyingine) muache, hata akiingiza faida kama yako, kuna watu wana vismati, as long wote mnakula basi sawaaaaa..
Sasa wewe wasikilize hao ngiri eti roho mbaya, kesho ufunge biashara uje hapa wakugeuke...
Yaani nilipe kodi ya 500k, nikulipe 220k, nitoke kwenye faida ya 800k nije 300k, kwa sababu YAKO, nikuache eti kisa na wewe unatafuta? Nani asiyemtafutaji???
Kila mtu ashinde mechi zake.
Balance mambo yako twende sawa.